Msaada: Jinsi ya kuvunja ndoa ya kikristo

Msaada: Jinsi ya kuvunja ndoa ya kikristo

Duuh... Sasa jamaa alioa ili iweje wakati mashine haifanyi kazi?🙌😂😂😂
 
Huyu mwanaume angemwambia huyo dada kabla ajue what to expect….. hivi hivi inashangaza atii
 
Sheria ya ndoa ya Kikristo inasema hivi, “without consummation, marriage is invalid” wao wanasema “ratum sed non consummatum” yaani ndoa huwa ni batili au tuseme hakuna ndoa kabisa iwapo tendo la ndoa halikufanyika baada ya kiapo cha ndoa, yaani yale zile process na mbwembwe zote za kanisani.
Hapo hakuna ndoa mkuu, kama ni Mkatoliki huyo binti aende aongee na Baba Paroko atamsaidia kwa kutumia sheria ya ndoa ndani ya sheria code ya canon 1983. Hiyo ni rahisi sana ndugu, au wewe ndo unataka ukamate chuma!
Ndio kaka natamani hata nimtoloshe maana ninapo ishi kunaumbar
 
Habari ndugu zangu, naishi Kigoma, nina lafiki yangu wa kike alifunga ndoa na mwanaume mmoja hivi toka wameona mwanaume hajawahi kushiriki tendo la ndoa na hana uwezo kabisa.

Wameishi miezi 3, hali hiyo imefanya binti arudi kwao. Kwa sasa anamiezi 2 na amepata mchumba mwingine, je, anawezaje kuvunja ndoa?

Naomba ushauri wapendwa.
Pengine hilo tatizo sio permanent (la kudumu) ithibitishwe kuwa hawezi kutibiwa ndio mambo mengine yafuate bado ni mke wake kihalali kabisa.
 
Hakumuonja kabla ya ndoa?.........................khaaa ona sasa hii hasara.
 
Habari ndugu zangu, naishi Kigoma, nina lafiki yangu wa kike alifunga ndoa na mwanaume mmoja hivi toka wameona mwanaume hajawahi kushiriki tendo la ndoa na hana uwezo kabisa.

Wameishi miezi 3, hali hiyo imefanya binti arudi kwao. Kwa sasa anamiezi 2 na amepata mchumba mwingine, je, anawezaje kuvunja ndoa?

Naomba ushauri wapendwa.
Hiyo inavunjika, atoe taarifa kwa viongozi wa dini, waitwe..
Baada ya hapo afungue shauri mahakamani apewe talaka.

Siku hizi zinavunjwa..
Ndoa sio cheti bali tendo la ndoa
 
Ndiyo inawezekana kuvunja hiyo ndoa. Jambo la kufahamu ambalo watu wengi hawafahamu ni kuwa hakuna ndoa isiyoweza kuvunjika sabbu ndoa zote ni mikataba, iwe imefungwa kidini, kimila au kiserikali.

Ifahamike pia kuwa ndoa zote halali zinavunjwa kwa misingi ya sheria ya ndoa, iwe ni yakidini, kimila au kiserikali.

Kwa huyo rafiki yako anayo sababu ya msingi kabisa kati ya sababu zilizotajwa kwenye sheria ya ndoa. KUSHINDWA SHIRIKI TENDO LA NDOA

Sasa kitu gani afanye?
Kwa maelezo yako ni wazi ndoa yao bado changa sana (chini ya miezi 5) na kwa sharti la sheria ni kuwa ndoa itavunjwa ikiwa ina miaka miwili au zaidi, labda itokee sababu nyinginezo za lazima sana.

Kwa huyo rafiki yako, anatakiwa kwanza kupita bodi ya usuluhishi wa masuala ya ndoa, inaweza ikawa Baraza la Kata likikaa kama Baraza la usuluhishi wa ndoa au Baraz la usuluhishi wa ndoa katika kanisa lao ila hapo ni lazima hilo baraz la kanisa liwe limesajiliwa kwa ajili ya shuhuli hiyo. Sio baraza ilimradi baraza hapana.

Hapo watasuluhishwa watapewa na ushauri pia, ikigoma sasa atapatiwa cheti/shahada ya kushindwa kusuluhishwa.

Hapo atakwenda Mahakamani kwa ajili ya kufanya mchakato wa maombi ya talaka sasa, hapo anaweza kwenda Mahakama ya Mwanzo eneo alilopo, huko ataweka sababu hiyo ya KUSHINDWA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA tangu ndoa ifungwe hadi wakati huo wa ombi la talaka.

Pia ataambatanisha nakala ya cheti cha ndoa, cheti/shahada ya kushindw kusuluhishwa pamoja na nyaraka zinginezo.

Hapo ataeleza pia kama kuna chumo/mali za pamoja hapa akumbuke kamwe hawezi kugawiwa mali alizomkuta nazo huyo mume wake has ukizingatia umri wa ndoa yao. Hatutegemei kuwepo na watoto hapo.

Basi watasikilizwa na Mahakama ikiridhika itatoa talaka.

Sasa baada ya kupatiwa talaka atatakiwa kwenda kwa msajili wa ndoa wilaya alimofungia ndoa na nakala ya maamuzi ya Mahakama yenye mhuri, pamoja.na cheti cha ndoa na nyaraka zinginezo, huko atakwenda kusajiliwa kama mtu asiye na ndoa.

Haya sasa arudi kwa mchepuko wake wakafanye jambo rasmi la kuoana.

Kila la kheri, japo hatupendi kuvunja ndoa zenu.
 
Ndoa ya kikristu ni balaa wakifuata utaratibu awatafute watu wote waliohudhuria siku ya ndoa wote waje kama walivyokuwa wamevaa kama walikuwa wajawazito waje na mimba zao.
Sio kweli,ndoa ya kikristo kwa sababu zilizowekwa hapo kuwa jogoo hapandi mtungi ina vunjwa asubuhi tu
 
Ndoa ya kikristo kwa kigezo hicho inavunjika .
Kuna Batili na Batilifu ,hivyo basi hii Ndoa ni Batilifu kwani ukamilifu wa ndoa ni tendo la ndoa
Pia hivi vitu vimeainishwa
Mf: ni mmmoja asiyewea kushiriki tendo Kama hivyo,
Mefunga Ndoa kabla ya ukamilifu/kushiriki tendo la ndoa mwinzio akakamatwa na polisi akala kifungo cha maisha basi hapo Ndoa hamna .
Ikiwa wangeshuriki tendo hata Mara moja angekuwa na kifungo.

Hivyo Basi waoneni viongozi wa Dini hili Ni Rahisi na halina upinzani ni halala na ataolewa na yoyote


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom