Msaada huu wimbo wa Koffi Olomide

Msaada huu wimbo wa Koffi Olomide

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,367
Reaction score
9,118
Kuna huu wimbo wa huyu Gwiji wa miondoko ya Sukus, ambaye amejipachika majina lukuki, mara sijui Mopao Mokonzi, Sakozi n.k.

Huu wimbo nimeusikia ukichezwa jana kwenye Bar moja wakati tunafuatilia mechi ya Simba na Vita, baadhi ya mashairi husikika kama matusi akitamka "coomer inauma..coomer inauma",.

Ningetamani sana wajuzi wa mambo ya kilingala waniambie ni maneno gani haswa hutamkwa pale, na kama ni kiswahili ni ndicho haswa alichomaanisha Gwiji huyu?

olomide.jpg
 
Kwa wale wasioufahamu wimbo niaouzungumzia ni huu...sikiliza hizo sekunde 40 za mwanzo.
 
Sio huo

Sent from my SM-G920P using Tapatalk
Najua zi/upo mwingine ila hata huu hayo maneno yapo hapo mwanzoni...kuanzia kwenye sekunde ya 0:35 mpaka 0:50.
 
Labda ni maneno ya ki lingala ila yana sounda kama kiswahili.
 
Kuna huu wimbo wa huyu Gwiji wa miondoko ya sukus, ambaye amejipachika majina lukuki, mara sijui Mopao Mokonzi, Sakozi n.k....huu wimbo nimeusikia ukichezwa jana kwenye Bar moja wakati tunafuatilia mechi ya Simba na Vita,..baadhi ya mashairi husikika kama matusi akitamka "coomer inauma..coomer inauma",.

Ningetamani sana wajuzi wa mambo ya kilingala waniambie ni maneno gani haswa hutamkwa pale, na kama ni kiswahili ni ndicho haswa alichomaanisha Gwiji huyu?View attachment 1047397
Rond point albam ya mwaka 1999, kwenye huo wimbo hatukani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
BASATA wako wapi, Kofi Olomide anatukana wanamwangalia tu?
 
BASATA wako wapi, Kofi Olomide anatukana wanamwangalia tu?
Kabisa Mkuu, huu wimbo hau sound poa kabisa...yaani mkiwa familia mnaangalia chini.

Kuna Bar jana walikuwa wanaucheza, haswa baada ya Vita kutangulia, mpaka wakaamsha hasira za Mashabiki Wazalendo.
 
Back
Top Bottom