Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Habari zenu wakuu,,
kwenye shughuli zangu za hapa na pale nimepiga bingo nna milion mbili cash ndan nataka kuondokana na maisha ya kupanga nna kiwanja Goba-Mbezi je ntaweza kujenga vyumba viwil nikaamia kwa gharama ya mill2,,, msaada wenye uzoefu please
Nipe bei ya tofali na cement za huko unakotaka kujenga
 
unaweza japo litakuwa banda na sio nyumba ambayo inaweza kukusitiri unahitaji tofari zisizopungua 1200 vyatua mwenyewe kwa kila mfuko tofari 40 unaweza ukagushi mpaka 45 ila maji mengi baada ya kuzivyatua na pia unapojenga saruji iwe kali. mifuko 30 ya cement itahitajika amboyo ni sawa na 360,000/-
utahitaji lory tano za mchanga wastani wa lory moja 120,000/- sawa na 600,000/-
nondo mbili mm12 sina uhakika na bei lakini inaweza kuwa 40,000/-
saruji ya kujengea kila tofari 60 mfuko mmjoa mifuko 20 sawa na 240,000/-
malango weka wa bati kwa dharura na madilisha weka kwanza wa mbao rahisi kila dirisha 30,000 madilisha manne 120,000/-
kitu bati bwana! weka bati la mstaafu gaji 30 au 32 kama zipo kila bati ukizunguka vizuri linaweza kuwa 8000/- unahitaji baji kama 30 sawa 240,000/-
mbao tenga 200,000/-
inabaki laki mbili fundi zinamfaa kabisa mpaka kuezeka.

sasa mafundi karibuni kwa data sahihi ila kwa kifupi unaweza kukamilisha kwa zaidi ya asilimia 75.
 
anza na tathmini ulizia vifaa na mafundi, matofari kiasi gani yaani PLANNING
hata yesu alisema ni Mtu gani anayetaka kujenga, aanze kujenga kabla hajajua gharama asije akaishia njiani watu wakamcheka?(luka 14:28).

kijijini sawa tena na wewe uwe fundi au saidia fundi, ila mjini labda uanze na ya Miti.
Kwani, huyu Luka anaelewa chochote kuhusu Magomeni Quarters? Au ameotea tu?
 
unaweza japo litakuwa banda na sio nyumba ambayo inaweza kukusitiri unahitaji tofari zisizopungua 1200 vyatua mwenyewe kwa kila mfuko tofari 40 unaweza ukagushi mpaka 45 ila maji mengi baada ya kuzivyatua na pia unapojenga saruji iwe kali. mifuko 30 ya cement itahitajika amboyo ni sawa na 360,000/-
utahitaji lory tano za mchanga wastani wa lory moja 120,000/- sawa na 600,000/-
nondo mbili mm12 sina uhakika na bei lakini inaweza kuwa 40,000/-
saruji ya kujengea kila tofari 60 mfuko mmjoa mifuko 20 sawa na 240,000/-
malango weka wa bati kwa dharura na madilisha weka kwanza wa mbao rahisi kila dirisha 30,000 madilisha manne 120,000/-
kitu bati bwana! weka bati la mstaafu gaji 30 au 32 kama zipo kila bati ukizunguka vizuri linaweza kuwa 8000/- unahitaji baji kama 30 sawa 240,000/-
mbao tenga 200,000/-
inabaki laki mbili fundi zinamfaa kabisa mpaka kuezeka.

sasa mafundi karibuni kwa data sahihi ila kwa kifupi unaweza kukamilisha kwa zaidi ya asilimia 75.
ahsante sana mkuu umenifafanulia vizur umenipa mwanga kumbe nikisema nitengeneze chumba kimoja kwa hela hii naweza weka had tyres
 
Nyumbani ni nyumbani bwana! jenga hata kimoja uhamie utakuja kuongeza baadae kuliko ukae na hiyo hela alafu ije iishie kusikojulikana.
Warembo wameongezeka
Starehe zimeongezeka
Simu nzuri zimeongezeka
Laptop nzuri zimeongezeka na kadhalika ubosi umeongeseka.
ahsante mkuu nam nmeligundua hilo ndo natafuta mawazo mbadara niweze kuwa na kwangu niwe natafuta hela ya kula tu
 
Umemjibu vizuri sana. Kwanza hapo alipo unaweza kukata hata hiyo 2m kaishaipunguza kutokana na matamanio ya anasa ya siku hizi. Namshauri Leo au kesho asubuhi atafute mafundi wa mitaani wa bei rahisi kama ramani anayo wakachimbe msingi na kununua tofari 1000 kwasababu chumba cha kawaida ukianzia kwenye msingi chenye pembe 4 utumia tofari 300. Kwa 2 ni 600 zinazobaki 400 ni msingi na kozi mbili baada ya renta. Hiyo 1m inayobaki nunua mbao za kujengea na kuezekea na mabati ya bei rahisi! Mambo mengine piga sound uamie kwako.
 
ulizia kwanza mwenyewe maana humu kila mtu atatoa uzoefu wake.
ukubwa wa vyuma pia unachangia tofali ngapi.
choo vipi hujengi? hapo pia kuna gharama ya shimo.
mabati, pita uulizie mitaa ya tazara, huwa kuna mabati ya bei rahisi geji za ujanjaujanja.
mbao vipi au utatumia miti/mirunda ulaze bati.
misumari haihitajiki sana,
milango na madirisha vipi, au utatengeneza wa bati,
naona watu wanahamia kachumba kamoja na maisha yanaendelea. tafiti mwenyewe. no gain without pain.

ila ukianza tu kuchimba msingi utafanikiwa mkuu. anza mdogomdogo.
ahsante mkuu umenifungua macho zaid nilisahau kuhusu choo ngoja niweke mawazo kwnye chumba kimoja kwanza nahis ntafanikiwa
 
Tofari 1400@1000 ni1,400,000.inabaki laki sita .fundi bado,mchanga bado,kokoto bado,mbao bado,nondo bado,maji bado bati bado,misumari bado,kuchimba msingi bado,madirisha na milango bado ,fundi hajaiba kidogo.Labda ujenge mbavu za umbwa.
wakuu jamani. Tofali za vyumba 2 ni kma
tofali 600 sawa na 600,000
mchanga lori moja 120,000
kokoto 120,000
cement 20 = 280,000
nondo 15=300,000
misumari = 20, 000
mbao kukodi za linter =40,000
fundi = 350,000
Maji =100,000
Jumla =1,930,000

then Mbao 2*2 = 24*4000
mbao 4*2= 24*7000
Bati= bando moja = 285,000
Fundi = 200,000
Misumari = 50,000
 
Back
Top Bottom