Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Msaada: Gharama za nyumba ya vyumba viwili

Kuna rafiki yangu kajenga huo huo mtaa vyumba vitatu na sebule lakini mpaka sasa kaishia kwenye lenta
 
Me nakumbuka nilikuwa najenga chumba cha stoo simple nilitumia laki 9 jumla...so kama unataka ujenge simple,bati ulaze, mbao mirunda, choo cha pipa, milango bati...unaweza...!!!
 
Kama chumba na sebule,
Tofali 700
Cement 20
Nondo 2
Mchanga lory 1
Kokoto karai 50
Mbao 40
Bati 20
Fundi 300,000
Misumari kg 6
Na gharama zingine,

Utatoboa mkuu ila ujitahid kubana gharama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari wanajf,

Naomba wataalamu wa ujenzi wanikadirie hii gharama zake

Banda la vyumba viwili na sebule katikati sebule ndogo.
 
Habari zenu wakuu,

Kwenye shughuli zangu za hapa na pale nimepiga bingo nna milion mbili cash ndani nataka kuondokana na maisha ya kupanga nna kiwanja Goba-Mbezi, je nitaweza kujenga vyumba viwili nikaamia kwa gharama ya milioni2.

Msaada wenye uzoefu please
Unaelewa maana ya nyumba ya vyumba viwili? Afu acheni utani nn million 2?
 
Nataka kujenga nyumba ya vyumba viwili vya kulala, sebule, public toilet/bafu, jiko dogo, katika hivyo vyumba viwili kimoja kiwe na choo/bafu ndani.

Kiwanja tayari ninacho 20 *20. Ninaplan kujenga nyumba ya kuanzia maisha maana kwa usawa huu nimeona nikikimbilia kujenga nyumba kubwa haitoisha na nitaendelea kupanga kwa muda mrefu. Nikishaamia kwenye nyumba yangu ndio nitaanza kujenga nyumba kubwa maana naamini uwanja utabaki wa kutosha.

Msaada wa makadirio jamani, naamini kuna watu wanauzoefu na ujenzi humu.

GHARAMA = TOTAL SQM (FLOOR PLAN) X 500,000/=
 
Kuhamia using standard and not extravagant of very high end finishing materials.
Hiyo hiyo standard ndio nataka... Cha msingi tiles ac ipo basi sitaki mbwembwe nyingi
 
Mm nifundi lakini pia nimejenga kibanda chavyumba vitatu nimejifunza kwamba ukitaka kujenga kijumba kidogo Kama unakianziao weanza tu mahitaji yaujenzi yanabadilika wakati wowote ukianza kupanga bajeti lazima ukwame milioni moja ama mbili kwenye ujenzi nihela ndogo na wengi wanajidanga ama kudanganywa kwamba sehemu yacementi kumi unaweza kutumia Saba utajuta Kama uwezo mdogo nenda kwahatua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nataka kujenga nyumba ya vyumba viwili vya kulala, sebule, public toilet/bafu, jiko dogo, katika hivyo vyumba viwili kimoja kiwe na choo/bafu ndani.

Kiwanja tayari ninacho 20 *20. Ninaplan kujenga nyumba ya kuanzia maisha maana kwa usawa huu nimeona nikikimbilia kujenga nyumba kubwa haitoisha na nitaendelea kupanga kwa muda mrefu. Nikishaamia kwenye nyumba yangu ndio nitaanza kujenga nyumba kubwa maana naamini uwanja utabaki wa kutosha.

Msaada wa makadirio jamani, naamini kuna watu wanauzoefu na ujenzi humu.
Mawazo yako kama Mimi shida sijapata mtu wa kunishauli
 
Hii labda koromije,,,,,darslamu hili ni Banda la kuku.Milioni mbili nilijenga Banda la kuku na bati nilichukua Tazara veterinary.
Wewe tajiri utaliita banda la kuku. Na kwa matajiri wakubwa, mabanda yao ya kuku thamani yake ni ya sh. million 40. Hivyo hata wewe hiyo nyumba yako uliyoijenga kwa sh million 40 hao matajiri wakubwa wanaiona kama kakibanda ka kuku tu.

Watu wote hawako sawa. Mwache ajenge kakibanda chake kwa uwezo wake aachane na gharama za kupanga kichumba kidogo cha sh 30,000/ kwa mwezi ambacho kwako ni sawa na chumba cha mbwa wako! Maisha ni hatua kwa hatua. Masikini wa leo anaweza kuwa tajiri mkubwa wa kesho. Vivyo hivyo tajiri wa leo anaweza kuwa masikini wa kutupwa wa kesho. Mpangaji ni Mwenyezi Mungu. Cha muhimu ni kufurahia maisha ya hapa duniani. Na mara nyingi masikini wanafuraha zaidi hapa duniani kuliko matajiri.
 
Back
Top Bottom