Msaada: Fursa za kiuchumi Katoro Geita

Mkuu Mushi92 , habari ndugu.

Tangu zamani huwa nipo interested sana kutafuta riziki kupitia sector ya madini. Ni uhaba wa mtaji ndiyo umekuwa ukinikwamisha, ila pia kutokuyafahamu vizuri madini ni changamoto nyingine.

Mie nataka kufanya 'ukota' kwenye dhahabu tu! Naplan kuja Katoro, na kwenda kujikita pale Msasa kwaajili ya kufanya ukota. Najua ukota hauna limitation ya mtaji... hata mtaji wa gram 3 naweza anza.

Niwe muwazi na mkweli, SIIJUWI dhahabu. Dhahabu siifahamu kabisa!
  • Ombi... kama inawezekana upande wako mkuu, je waweza kuwa mwalimu wangu kunifundisha na kunipa uzoefu wa kuijua vizuri dhahabu ilivyo?
  • Ukota unaweza fanyika informally kienyeji? ama kuna taratibu za kisheria ambazo ni lazima kuzitimiza kwanza?
  • Ni vifaa (vitendea kazi) vipi vya lazima kuwa navyo ili kufanya ukota?
Natarajia kuja Katoro/Msasa siku ya Jmosi week hii kufanya kasurvey kuhusu suala hili.

Mambo yamekuwa taiti sana huku jijini, tunan'gang'ania kukaa mijini huku mifuko imetoboka haswa. Hatuna kitu. Kama kijana, nimeona sasa ni wakati kwenda popote kusaka maisha. Popote kambi.

Natanguliza shukrani.
 
Mkuu Mushi92 , habari ndugu.

Tangu zamani huwa nipo interested sana kutafuta riziki kupitia sector ya madini. Ni uhaba wa mtaji ndiyo umekuwa ukinikwamisha, ila pia kutokuyafahamu vizuri madini ni changamoto nyingine.

Mie nataka kufanya 'ukota' kwenye dhahabu tu! Naplan kuja Katoro, na kwenda kujikita pale Msasa kwaajili ya kufanya ukota. Najua ukota hauna limitation ya mtaji... hata mtaji wa gram 3 naweza anza.

Niwe muwazi na mkweli, SIIJUWI dhahabu. Dhahabu siifahamu kabisa!
  • Ombi... kama inawezekana upande wako mkuu, je waweza kuwa mwalimu wangu kunifundisha na kunipa uzoefu wa kuijua vizuri dhahabu ilivyo?
  • Ukota unaweza fanyika informally kienyeji? ama kuna taratibu za kisheria ambazo ni lazima kuzitimiza kwanza?
  • Ni vifaa (vitendea kazi) vipi vya lazima kuwa navyo ili kufanya ukota?
Natarajia kuja Katoro/Msasa siku ya Jmosi week hii kufanya kasurvey kuhusu suala hili.

Mambo yamekuwa taiti sana huku jijini, tunan'gang'ania kukaa mijini huku mifuko imetoboka haswa. Hatuna kitu. Kama kijana, nimeona sasa ni wakati kwenda popote kusaka maisha. Popote kambi.

Natanguliza shukrani.

Karibu Mkuu.
Andaa ela ya mzani ni laki 2.
Mtaji angalia iwepo kias ili usiwe unahangaika mwenda sonara kil mara..
Cha zaidi ni ujanja wako na mvuto......
 
Mashine inasaga Mawe.... Ule unga unaoshwa (process za kupata dhahabu kwa njia ya mercury) then mabaki inabaki nayo wewe ambayo yana 75%ya dhahabu. Yale mabaki unarundika unapata kifusi cha tani kadhaa baada ya muda mfan let say miez 6 unauza na Mashine zako bado mpya. Labda cha kubadili ni gololi hata za laki 3 znatosha
Mkuu maeneo ya kuweka Crusher yanapatikana??
 
Mkuu maeneo ya kuweka Crusher yanapatikana??
maeneo Ni mengi inategemea unataka kuset wapi.
Mfano hapo nyarugusu unakuta tayari baraka ashachukua maeneo....Ni lazima akutimue ikibidi akudhulumu kifusi
 
Njoo fungua sehem ya kusaga Mawe. Mtaj around 20mil. Unaweka makarasha mawil ya kusaga.....mambo yakienda sawa unauza kufusi after 6months unaeza pata 100mil kutegemea na PP
Mkuu, kama hautojali unaweza fafanua iyo 20m ya mtaji inafika vipi kwenye iyo amount?
 
Nataka kwenda Katoro kufungua sehemu ya kutengeneza Viatu vya Kimasai, M-PESA na Duka LA kuuza chupi za kike, na watoto vp inaweza piga hatua?????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom