Msaada DST: Kuunganisha kifurushi bila kupiga huduma kwa wateja

tajirijasiri

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
2,864
3,851
Wanabodi.
Naomba msaada jinsi ya kuunganisha kifurushi cha DSTV cha juu kuliko kile cha Mwanzo bila kupiga Huduma kwa wateja. Mfano, Mwanzo ulilipia kifurushi cha Compact Tsh 82,500 kikaisha muda wake, baadae ukanunua Compact Plus 122,500/-. Je, utawezaje kukiunganisha moja kwa moja pasipo kupiga Huduma kwa Wateja. Nimejaribu Reset lakini zunaonesha channel za Compact pekee yake na sio Compact plus. Nimejaribu njia zote ikiwemo Self Service ya internet, nimejaribu *150*46# Clear error wapi, nimejaribu RESET SMARTCARD# kwenda 15727 bila mafanikio. In short nimejaribu kila njia mpaka nimepiga customer care lakini najibiwa na mashine eti jamaa hawafungui Xmass.

USHAURI: Kama kuna mhusika wa DSTV atasoma ujumbe huu, Tafadhali namuomba sana awashauri mabosi wake hasa wa IT waiboreshe DSTV, uhusiano wa malipo na activation yenu mko manual sana. Yaani mtu analipa halafu anaanza kuhangaika kweli kweli.
 
Back
Top Bottom