Msaada: Dawa kwa mtu aliyeng'atwa na tandu

Msaada: Dawa kwa mtu aliyeng'atwa na tandu

relis

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2015
Posts
3,429
Reaction score
5,470
Wakuu habari!,nimehamia makazi mapya huku mbezi, lkn toka niingie kwenye hii nyumba tabu tupu, karibu kila Siku lazima tuue tandu.

Msaada wenu wadau kwa ajili ya tahadhari. Nasikia mdudu tandu ana sumu Kali zaidi ya nyoka. Je, ikitokea akauma mtu ni lazima muhusika afikishwe hospitali au sumu itapoa yenyewe?

Na je aumapo mtu Tiba mbadala ni ipi msaada maana nimeua tandu watambao na Giza hili naona mmoja kaparamia neti yangu ya msaada.
 
Sumu yake sio kali kihivyo huku mtaani kuna imani kwamba akikuuma ukimuua halafu ukamchoma ukamsaga ukapaka majivu yake unapona lkn ukweli wake wanaujua waliojaribu
 
Sumu yake sio kali kihivyo huku mtaani kuna imani kwamba akikuuma ukimuua halafu ukamchoma ukamsaga ukapaka majivu yake unapona lkn ukweli wake wanaujua waliojaribu
Uliwahi ng'atwa mkuu au
 
Mkuu ondoa hofu nikweli ana sumu kali pia si mwepesi wa kupiga bite. Nadra sana ujue umejichanganya sana kwake.

Wa kumuogopa ni scorpion yaan huyo ukikatiza tu kwenye himaya yke unakula bite. Ila jihadhari na tandu ana sumu kali sana.

Huwa akikomaa anaota km mabawa hivi mkiani asee km sio kuzimia ni kudata
 
Niliwahi ng'atwa na huyo mdudu,maumivu yalikua makali ila yaliisha bila dawa
 
Wacha tu wakung'ate we kwanini uwachokoze kwa kuingilia makazi yao? [emoji30] [emoji30] ila mdau hapo juu kakushauri vyema ni kweli sio wadudu korofi ila akikupiga pini sumu yake ni hatari ni vyema ukachukua tahadhari mapema kwa kufanya fumigation na kuziba sehemu zenye nyufa ndani na pembezoni mwa nyumba kwani ndiko hasa wanakofanya makazi...
 
Huwa nasikia kuweka barafu eneo la jeraha inasaidia. Japo sijawahi kutana na case ya mtu kuumwa na tandu.

Pia tafuta mawe wanauza wamasai yapo vizuri kwa sumu za wadudu.

Kikubwa fanya fumigation maana balaa la tandu hata akikutembea tu kama unangozi laini unavimba
 
Sumu yake sio kali kama ya nyoka.Kawaida Tandu akikuuma maumivu yanakaa muda mrefu hata wiki inafika ila haiui lkn cha moto utakiona.Zipo dawa za kutuliza maumivu ukienda hospital
 
Wanasema uking'atwa wahi kumuaa, kadri anavyotembea ndio na maumivu hua makali zaidi

Uking'atwa pale alipokuuma pachanje na wembe miminia mafuta ya taa kidogo.

Nawaogopa hawa wadudu

Archduke
 
Hahaaaaa Karibu Mbezi Mkuu

Mimi niliumwa na tandu nadhani May mwaka huu mwezi mmoja tu tokea nihamie.
Maumivu yake acha kabisaaaaaa

Nilipanic hatari maana nilikuwa nikisikia sumu yake ni kali kuliko nyoka basi nikakiona kifo hiki hapa.
Bahati nzuri alikuwepo mtu karibu hivyo alivyoniuma tu yeye akamuona akamuwahi kumuua.

Sasa wakati anamuua mimi huku pressure juu like “Unataka nife? Yani badala uniwahishe hosp unahangaika kumuua?” Hapo najisikilizia ndio nakufa nini jamani? Hahaaaaa

Kwa hofu nilikimbilia ndani nikatafuta kitunguu swaumu kilipo nikakiponda harakaharaka nikasugua kwa nguvu juu ya jeraha maana palianza kuvimba (mimi hutumia kitunguu swaumu kama tiba nikiumwa na wadudu kama nyuki,nyigu n.k)
Nilifanya vile mara 3 kwa siku ile japo palikuwa panauma sana,baada ya hapo nikameza dawa za maumivu basi.

Maumivu yaliendelea hadi baada ya wiki yakapotea ila eneo aliloniuma ngozi ilibabuka.

Cha kufanya fanya fumigation ya nguvu hapo,zingatia na usafi pia.
Ila ondoa shaka,tandu haui.
 
Najuta hata kusoma. Huyo mdudu alishanifanya nitafute kijana mtaani anisaidie kumsaka ndani. Leo siku nzima naweza kaa najikung'uta hata nikishikwa na nguo sababu tu nimemsoma huyo mdudu
 
Hahaaaaa Karibu Mbezi Mkuu

Mimi niliumwa na tandu nadhani May mwaka huu mwezi mmoja tu tokea nihamie.
Maumivu yake acha kabisaaaaaa

Nilipanic hatari maana nilikuwa nikisikia sumu yake ni kali kuliko nyoka basi nikakiona kifo hiki hapa.
Bahati nzuri alikuwepo mtu karibu hivyo alivyoniuma tu yeye akamuona akamuwahi kumuua.

Sasa wakati anamuua mimi huku pressure juu like “Unataka nife? Yani badala uniwahishe hosp unahangaika kumuua?” Hapo najisikilizia ndio nakufa nini jamani? Hahaaaaa

Kwa hofu nilikimbilia ndani nikatafuta kitunguu swaumu kilipo nikakiponda harakaharaka nikasugua kwa nguvu juu ya jeraha maana palianza kuvimba (mimi hutumia kitunguu swaumu kama tiba nikiumwa na wadudu kama nyuki,nyigu n.k)
Nilifanya vile mara 3 kwa siku ile japo palikuwa panauma sana,baada ya hapo nikameza dawa za maumivu basi.

Maumivu yaliendelea hadi baada ya wiki yakapotea ila eneo aliloniuma ngozi ilibabuka.

Cha kufanya fanya fumigation ya nguvu hapo,zingatia na usafi pia.
Ila ondoa shaka,tandu haui.
Nashukuru ntakaribia hapo kwako unipe uzoefu,story za mtaani. kuhusu tandu unaona bora ung' atwe hata na koboko,shukran kwa faraja.
 
tandu nshalala nao sana rum asee ila amna ambae amewah ning'ata

btw madhara yao sio makubwa na si vizuri kuua viumbe hai mana hayo ndo makazi yao na we ndo umewaingilia
 
Pole kwa kuvamiwa na Tandu mkuu, fata ushauri wa wakuu hapo juu itakusaidia pia usiogope sana tandu hayupo kama anavyoelezewa mitaani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom