Msaada: Boss wangu ameniambia nikasomee uchomeleaji

Msaada: Boss wangu ameniambia nikasomee uchomeleaji

John kirua

Senior Member
Joined
Dec 7, 2021
Posts
143
Reaction score
108
Taasisi yangu wanahitaji fundi mchomeleaji mwenye cheti cha long course ambayo ni miaka 2 na mimi kutokana na swala la ada kusomea kozi ya miaka 2 sina.

Ila nahitaji kujua kuchomelea na ufundi kwa ujumla kwanza napenda hiyo kazi je, nifanyaje au nitumie njia gani kuweza kujua maana miaka 2 ni mingi sana halafu ada yake ni kubwa sina hiyo ela ya kulipa
Na boss wangu anahitaji mtu anayechomelea tu.
 
Wewe kazi yako au taaluma yako ni nini hapo kwanza mpaka useme anahitajika mtu wakuchomelea.

Je hapo ulipo una experience yeyote katika kuchomelea hata kujua vitu vidogo vidogo vya kuchomelea?

Kozi ya uchomeleaji hakuna Short course ya muda mfupi kama uko tayari na hayo maarifa japo kwa uchache
 
Itabidi uachee kazi kwanza ndio uje ujifunze mtaani piaa ,maaana uwezi kujifunza ufundi uku unafanya kazi ..labda kazi ufanyee usiku ,mchana uingie kujifunza kuchomeleaa
 
Kwanza huja Sema Wewe kazi yako nini hapo kazin kwako

Kuchomelea ame kwambia ukasomee je wew unapenda taaruma iyo??

Ada ya veta sio kubwa ndugu yangu kama kweli Wewe mfanya kazi mana ni elf 60 kwa mwaka kama unatoka nyumban na 150,000 kwa wanao kaa hostel kwa vyuo vya selikal.

Ingawa Kuna garama nyingine ndogo ndogo hazi wez kuzid laki NNE kwa mwaka

Kama Lengo ni Kuchomelea je unatakiwa ujue unachomea nini je inahusiana na mambo ya kufanya ubunifu wa Saman au ni kuchoma kuunga tuu vyuma. Kama Lengo kuchoma tuu miez mitatu inatosha veta au mtaan una weza
 
Taasisi yangu wanahitaji fundi mchomeleaji mwenye cheti cha long course ambayo ni miaka 2 na mimi kutokana na swala la ada kusomea kozi ya miaka 2 sina.

Ila nahitaji kujua kuchomelea na ufundi kwa ujumla kwanza napenda hiyo kazi je, nifanyaje au nitumie njia gani kuweza kujua maana miaka 2 ni mingi sana halafu ada yake ni kubwa sina hiyo ela ya kulipa
Na boss wangu anahitaji mtu anayechomelea tu.
Unataka tukusaidie nini?
 
Nenda gereji ukawe nyokaa sema wale mafundi wanaroho mbaya kinyama ukiwa nyokaa wakati unachomelea wanakulazimisha uangalie moto wanakwambia angalia kazi, mziki ni usiku ukitaka kulala unahisi macho yamejaa mchanga
 
Taasisi yangu wanahitaji fundi mchomeleaji mwenye cheti cha long course ambayo ni miaka 2 na mimi kutokana na swala la ada kusomea kozi ya miaka 2 sina.

Ila nahitaji kujua kuchomelea na ufundi kwa ujumla kwanza napenda hiyo kazi je, nifanyaje au nitumie njia gani kuweza kujua maana miaka 2 ni mingi sana halafu ada yake ni kubwa sina hiyo ela ya kulipa
Na boss wangu anahitaji mtu anayechomelea tu.
hakuna short cut
 
Back
Top Bottom