Mrema aitolea uvivu CHADEMA

Mnajibishana na mwehu jamani;;...huyu wa kuombea sana mungu else hii miaka mitano mtazika wabunge wengi kwelii na sijui kama ataifika!!
 
Hongera kwa kusema ukweli, tunajua CDM wana chuki nawe kwani Uenyekiti wa kamati ya bunge ya serikali za mitaa CDM wali ililia muda mrefu sana, bunge kwa kutumia busara wakawachinjia baharini. Sasa wamebakia na uwaziri kivuli ambao bungeni hauna meno.

vilaza at work. LOL!!
 
Ww mwenyewe hapo una chuki na Mrema pamoja na chama chako ! kwani Mrema hata km kuna jema kama hili analisema, ww unapinga kwa husuda zenu za kutaka madaraka

hivi kumbe hata wewe diabets yako imeathiri hata ubongo wako kama ilvyomuathir mrema? Pole sana.
 
Njaa tu jamani,anaishi kwa fadhila za wadhamini wake,kazi anayofanya ni sehemu ya kujihakikishia mkate wa kila siku
 
Hongera kwa kusema ukweli, tunajua CDM wana chuki nawe kwani Uenyekiti wa kamati ya bunge ya serikali za mitaa CDM wali ililia muda mrefu sana, bunge kwa kutumia busara wakawachinjia baharini. Sasa wamebakia na uwaziri kivuli ambao bungeni hauna meno.

...and you really think yourself as Genius???? What a discredit to the word!
 
Wadau,

Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema ameyalaani vikali maandamano ya Chadema yanayoanza kesho nyanda za juu kusini. Mrema anadai kwamba CHADEMA wanaandamana kudai mambo ambayo tayari serikali inayafanyia kazi..ametoa mfano wa katiba mpya.

Mrema ameenda mbali zaidi na kusema kwamba CHADEMA wanataka kuvuruga amani na kuleta uchochezi ili nchi isitawalike. Amewasihi polisi wawazuie CHADEMA na kuvuruga mikutano na maandamano yao.

Mrema anajidai kusema kwamba eti yeye ndiye mwenye uchungu na nchi hii na ndio maana anakamata viongozi wa halmashauri wanaoendekeza vitendo vya ufisadi.

Hakika kila mtu aliyemsikia Mrema amejiuliza mara mbilimbili yeye ni nani hata aisemee serikali????

...Aliposema matatizo ya hali ngumu ya Uchumi yanaletwa na ukame na kwamba tusimlaumu Kikwete kwa hilo, karibu nitoe chozi kwa kumuonea huruma mzee huyu kwamba hapa ndipo alipojifikisha...Pa kulamba viatu vya wakubwa. Poor him.

 
Wadau,

Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema ameyalaani vikali maandamano ya Chadema yanayoanza kesho nyanda za juu kusini. Mrema anadai kwamba CHADEMA wanaandamana kudai mambo ambayo tayari serikali inayafanyia kazi..ametoa mfano wa katiba mpya.

Mrema ameenda mbali zaidi na kusema kwamba CHADEMA wanataka kuvuruga amani na kuleta uchochezi ili nchi isitawalike. Amewasihi polisi wawazuie CHADEMA na kuvuruga mikutano na maandamano yao.

Mrema anajidai kusema kwamba eti yeye ndiye mwenye uchungu na nchi hii na ndio maana anakamata viongozi wa halmashauri wanaoendekeza vitendo vya ufisadi.

Hakika kila mtu aliyemsikia Mrema amejiuliza mara mbilimbili yeye ni nani hata aisemee serikali????

Unajua huyu ni mtu mkubwa sana amashakuwa Waziri wa MAMBO YA NDANI,
Kwahiyo anajua vizuri ni nini kazi za jeshi la POLISI,
Kwa hiyo sio bbbahati mbaya kusema POLISI wafanya kazi ya KUVURUGA.
 
Hivi Mrema alifulia kidogo kufa eeh? lakini asijipendekeze mpaka akahatarisha maisha ya Bosi wake, huko kusini hatii mguu, na polisi nao wasitafute ushujaa kusini sio arusha na zanzibar walikopiga watu wakaachwa.
 
Wadau,

Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema ameyalaani vikali maandamano ya Chadema yanayoanza kesho nyanda za juu kusini. Mrema anadai kwamba CHADEMA wanaandamana kudai mambo ambayo tayari serikali inayafanyia kazi..ametoa mfano wa katiba mpya.

Mrema ameenda mbali zaidi na kusema kwamba CHADEMA wanataka kuvuruga amani na kuleta uchochezi ili nchi isitawalike. Amewasihi polisi wawazuie CHADEMA na kuvuruga mikutano na maandamano yao.

Mrema anajidai kusema kwamba eti yeye ndiye mwenye uchungu na nchi hii na ndio maana anakamata viongozi wa halmashauri wanaoendekeza vitendo vya ufisadi.

Hakika kila mtu aliyemsikia Mrema amejiuliza mara mbilimbili yeye ni nani hata aisemee serikali????

Mrema ana wivu kwa vile ameisha kisiasa na hana mvuto tena.
Anahangaika na matawi ya ufisadi wakati Slaa anang'oa mizizi ya ufisadi.
 
WADAU HII IMEKAAJE?

Mrema aitolea uvivu Chadema

Saturday, 25 June 2011

NA PETER ORWA, DODOMA

MBUNGE wa Vunjo, Augustino Mrema,(TLP), ameiomba serikali kuwadhibiti wanasiasa wanaochochea wananchi kuandamana, kwa kuwa kufanya hivyo hakuna tija kwa taifa.

Pia, amesema, wanasiasa wanaoendeleza maandamano na ghasia kama njia ya kutimiza malengo yao ya kisiasa, wanahatarisha usalama wa nchi, na hilo lina ushahidi duniani kote.

Ingawa Mrema hakutaja chama wala jina la mwanasiasa, Chadema imekuwa ikihamasisha maandamano, na baadhi ya viongozi wake kutoa kauli za uchochezi zenye kuashiria kuvuruga amani na utulivu nchini.

Katika mchango wake katika hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu, iliyowasilishwa juzi bungeni na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Mrema alisema, haamini kwamba muafaka wa kijamii na kisiasa unaweza kupatikana kwa maandamano na ghasia.

Mrema alisema, athari zake hazina mipaka ya vyama, na alionya wanasiasa kwamba vitendo hivyo ni vya hatari dhidi ya amani ya nchi. Aliwasihi kuunga mkono hotuba hiyo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliyewataka wasitumie ghasia na maandamano kwa ajili ya kutimiza malengo yao ya kisiasa.

"Nataka kumuunga mkono waziri mkuu kwa hili la amani, halina chama tawala wala upinzani. Tusichezee vurugu na hasa maandamano," alisema Mrema. Alisema, historia inaonyesha kuwa, vitendo vya maandamano mara zote vimeishia katika mikakakati ya kutaka kupindua serikali, kitendo kinachoonyesha hakina tija, zaidi ya vurugu, na wananchi wanaoandamana sio wanaotwaa madaraka.

Mrema aliwaponda wanasiasa hao bila kuwataja majina kwamba, kufurukuta kwao na kufanya vitendo vya ghasia, kumeonyesha havina tija kwani hawajawahi kufikia kupata kiwango cha asilimia 28 ya kura alizopata yeye alipogombea urais mwaka 1995 kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi.

"Nawaomba wanasiasa wa pande zote mbili, wote ni wadau. Tusitumie malengo yetu ya siasa kuchochea vurugu na hasa maandamano," alisema Mrema aliyetumia mifano ya athari za ghasia katika nchi mbalimbali zikiwemo za Kenya, Madagascar, Misri na Sudan.

Katika hatua nyingine, Mrema ameiomba serikali ianze kumlipa mshahara kama naibu waziri mkuu mstaafu, wakati wa uongozi wa serikali ya awamu ya pili. Mrema alisema, ingawa cheo hicho hakipo katika stahiki za kikatiba, lakini kwa vile ulikuwa ni uamuzi rais kumteua kushika wadhifa huo, basi ni stahili yake.

"Mbona haki yangu haipatikani? Nipatieni japo asilimia 20. Msione simba kanyeshewa mkadhani ni nyani. Ili niendelee kutetea mambo mengi ninayoyajua, naomba haki yangu," alisema na kusababisha wabunge kuangua kicheko.

Lowassa awaponda
MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa, ameitaka serikali kuwa jasiri kwa kufanya maamuzi magumu katika masuala yanayohusu maendeleo. Pia, Lowassa ambaye alijiuzulu nafasi ya waziri mkuu, Februari 6, 2008, amekemea watu wanaobeza mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa serikali ya CCM katika miaka 50 ya Uhuru.

Alisema ili taifa lipate mafanikio makubwa kiuchumi, viongozi hawana budi kuthubutu katika maamuzi. "Serikali ya CCM imefanya imefanya mambo mengi tangu Uhuru," alisema Lowassa.

Alisema hayo alipochangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu, iliyosomwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi, ambapo pamoja na mambo mengine aliisifu kuwa ni nzuri.

Alianisha maeneo ambayo serikali inapaswa kuyafanyia kazi katika dhana hiyo ya kuthubutu kuwa ni kukopa fedha kutoka nje kwa kutumia dhamana ya akiba ya gesi iliyopo ukanda wa Mtwara, ili kufadhili maendeleo kitaifa.

"Eneo mojawapo la kuthubutu ni reli kati ya Dar es Salaam na Kigoma. Tunaweza na wala tusiogope," alisema.

Lowassa aliyekuwa akishangiliwa na wabunge wakati akitoa mchango wake huo, alitaja reli ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia Tanzania (TAZARA), kuwa ni sehemu nyingine muhimu ya kuhuishwa kwa fedha za mkopo ili kuboresha uchumi.

Alisema miradi itokanayo na fedha zitakazokopwa, ziwekewe utaratibu maalumu wa kuwa na manufaa kwa wananchi vijijini ambako ndiko kwenye Watanzania wengi. Pia, aliishauri ofisi ya waziri mkuu ipunguziwe majukumu, ili ifanye kazi kwa umahiri ambapo alipendekeza Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ijitegemee.

"TAMISEMI ni kubwa ni kila kitu, ipunguzwe maana ni kila kitu 'bureaucracy' (urasimu) ni kubwa katika muundo wake," alisema na kutaja idara na ofisi nyingine zilizoko chini ya ofisi ya waziri mkuu kuwa ni za maafa, baraza la uwezeshaji, na uratibu na bunge.

Lowassa aliwasifu viongozi waliotangulia katika awamu tatu zilizopita za uongozi wa nchi kwamba, wana mchango mkubwa katika kujenga msingi wa mafanikio. Alitumia fursa hiyo kuwakemea wanaobeza hatua ya maendeleo iliyopigwa kutokana na uongozi wa serikali ya CCM katika miaka 50 ya Uhuru, akiorodhesha mafanikio kama ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kwa gharama ya sh. trilioni moja, asilimia 95 ya watoto wenye umri wa kwenda shule kuhudhuruia elimu ya msingi na wingi wa sekondari za kata.

Alitaja hatua zingine za maendeleo ni mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda mkoani Shinyanga, miradi ya uchimbaji gesi Mtwara, na ukuaji wa uchumi hadi kufikia kiwango cha asilimia saba kwa sasa.

"Kwa waliokuwepo wakati huo, nakumbuka katika miaka 10 ya kwanza ya Uhuru, Mwalimu Nyerere alisema, mtu akija kwa jeuri na fedhuli, akikuuliza Tanzania mna nini, wewe mjibu kiungwana, tuna amani," alisema Lowassa. Pia, ameiomba serikali kutoa msaada wa chakula ili kuwanusuru njaa wananchi wa Monduli.


Source: UHURU
 
Mkuu look about the source,kwa taarifa mimi nimeahirisha kuisoma hiyo habari baada ya kuona kuwa inatokea kwenye chama cha magamba
lete habari za maana tulisongeshe......achana nao hao
 
Mkataa kwao ni mtumwa,Mrema badala kukaa na kujenga chama chake anadiriki kuponda Chadema,ameamua kuwa ka-vuvuzela ka ccm.Wacha apige mayowe,hajui mgogoro TLP ni mkubwa sana na bwana mkubwa anatakiwa kuachia ngazi!CDM mwendo mdundo,watapiga kelele lakini mapambano bado yataendelea
 
Back
Top Bottom