Mrema aitolea uvivu CHADEMA

Huyu Mrema kafulia kisiasa.......kunyamaza hawezi! anabaki kujikosha kwa serikali masikini!!

au uzee na maradhi ndo vinavyosababisha awe hivyo???

.......stage za utotoni zinajirudia tena, thinking capacity yake ni kwishney,!! MASIKINI MREMA!!!!
 
Hivi keshaamka?

mrema.jpg
 
Tatizo la mtoa hoja amesahau kuwa watz ni "wavivu" wa kusoma, ameandika gazeti zima!


sie wasomaji wa raia mwema na mwanahalisi tuna uwezo wa kusoma gazeti zima mpaka ukurasa wa michezo.....na sie wanafunzi wa chachage tumefundishwa kusoma kuanzia kitabu cha max volume ya kwanza mpaka ya mwisho ili ijubi swali moja la chachage....kusoma kwetu si tabu au adhabu ni kuongeza maarifa na ujuzi

kumbuka hakuna generalization....hakuna sisi 'watanzania wavivu' wa kusoma ......kuna mtanzania mmoja mmoja mvivu wa kusoma....siwezi kugeneralizi taarifa za kijiji kimoja tu sembuse taifa

mix with yours
 
It is unthinkable to be at the otherside while still playing a game of the this side whatch out cause the coach might deside never to select you at either side
 
hakika ndugu yangu mrema umemsoma vizuri sana, huyu ni zaidi ya kibaraka au msaliti!!! njaa inamsumbua sana, huyu ni yule mrema ambaye tulisukuma gari zake na pia tulimbeba juu kwenye maandamano alokuwa anaitisha na NCCR ili tupigwe mabomu na yeye apate mradi wake. huyu mrema atuambie leo ndo kajua kwamba maaandamano yanafanya nchi isitawalike?au kama alijua toka NCCR nini ilikuwa lengo lake mwehu huyu? kumbe ambacho wananchi hawakujuwa ni kwamba mrema alikuja upinzani ili kupata lift tu ya kwenda ikulu na sio uchungu na nchi yetu. sasa tunaamini hata yake makelele yake ya chavda na loliondo yaliletwa na kupunjwa cha juu tu na sio vinginevyo. wana jf msisahau pia kauli yake akiwa bado rasmi ndani ya ccm, alipobanwa na media alijibu loliondooooo loliondoooo, ya mama yenu.? we mrema utakufa kwa aibu mcharuko wewe
 
Mrema alikuwa yule wa 2005, huyu wa sasa ni uchakachuaji tu. anafuta mwenyewe historia aliyoiweka
 
Chadema wakichukua madaraka inaonekana ni wengi watajinyonga! Wa kwanza ni Zombe, na huyu bwana naona kama anataka kufuata mkumbo!
 
Nimesoma sociology....ninaelewa kuwa mwanadamu anaweza kuchange attitude towards jambo fulani lakini anapobadilika kuna mambo mawili ...kwanza kabisa kuna sababu iliyosababisha aamini jambo hilo na anapobadilika kuna jambo pia limetokea na kusababisha aamini kuwa alichokuwa anaamini awali kilikuwa na mapungufu kwaiyo haoni sababu ya kuendelea kuamini jambo hil katika mtazamo huo kwa iyo anaamua kubadilika.
Nikiwa kama mwanafunzi wa 'human geography' ninaamini pia katika role ya time and space katika maisha binadamu...kwa maana ya kuwa wakati fulani unaweza kukubaliana na jambo fulani na kundi fulani....lakini wakati mwingine unaweza kutokubaliana na watu wale wale hata ukiwa mahali palepale ila utategemea kwenye jambo gani...kama ni AJENDA ILE ILE uliyokubaliana nao awali then tunaweza kukuhoji sababu ya wewe kubadilisha mtazamo wako na itabidi uwe na majibu ya kutomung'unya ili tuelewe mwenzetu una ajenda gani.....kama utamung'unya mung'unya huwezi kuzuia watu kukuadhibu kwa kukupa label yaulichoonyesha .....

Nipo naangalia bunge hapa... Dr Augustine Mrema amepewa nafasi ya kuchangia katika hoja ya ujenzi...Mh mrema ametumia muda mwingi kuwalaumu watu wanaomuona kama kibaraka wa serikali....ametumia muda pia kujastifayi kwanini ana iunga mkono serikali and more specific JK...akitaja mazuri aliyotendewa katika jimbo lake nk. amesema pia si lazima awaunge mkono watu wa chama fulani na ajenda yao kuandamana kwa sababu yeye kwa uzoefu wake wa uwaziri/naibu waziri mkuu anajua athari ya uvunjifu wa amani....tena ameenda mbali zaidi kwa kudai kuwa hakutumwa na jimbo lake kutaka nchi isitawalike!!

Mh. Mrema ninaamini kuwa watanzania wanaokuita au kukuhisi kuwa kibaraka wa serikali hawafanyi hivyo from no where! wamekupima maneno na utendaji wako toka umekuwa kiongozi wa umma wa watanzania. Ukiwa kiongozi wetu ndani ya ccm uliweza kutetea watanzania kwa nguvu zako zote, bila woga wala TAHADHARI....ulisimama kidete kutetea rasilimali zetu mfano loliondo...ulileta msamiati wa WALAHOI kuonyeshwa kukerwa na gap ya umaskini kati ya walionacho na wasio nacho....ukiwa upinzani miaka ya mwanzoni pia uliendelea na mapambano...hukuchoka kusuta serikali na sisi hatukuchoka KUSUKUMA GARI LAKO KUKUUNGA MKONO....
Ni sisi wale wale tulikuwa tunakuona kama kimbilio ndio tunafikiri au zaidi ya yote kuamini kuwa umekuwa kibaraka kwani mtazamo wako juu yaleyale uliyokuwa unayakataa / SERIKALI ILIYO LIKIZO ISIYOTEKELEZA MAJUKUMU YAKE HATA RASILIMALI ZAKE KUIBIWA NA WANANCHI KUWA WALALAHOI UMEBADILIKA.......... LEO SOKOINE ANGEKUWEPO NA ANGEKUWA ANAWATETEA WAHUJUMU UCHUMI ALIOKUWA ANAWASAKAMA........AU LEO HII MWALIMU ANGEKUWEPO AKATETEA UBEPARI.. NA KUANZA KUELEZEA SEHEMU YA UZURI WAKE TUNGEHOJI...kwaninini...kwa sababu jambo lilelile waliokuwa wanalikataa na kubuni mbinu za kupambanana nalo usiku na mchana ...sasa wanalizungumza kwa kulitetea NA KUJARIBU KUTUONYESHA UPANDE WAKE MZURI BILA KUGUSA KABISA UPANDE WA HASARA YAKE.


Hata wanachama wa magamba wanasema hali si shwari (rejea, warioba, kitine)...hata mwl nyerere foundation wenye ccm yao wanatumambia si shwari...so haiwezi kuwa shwari kwa sababu ya vijineno vyako ...endelea kula ulichopewa kama vita ya mafisadi imekushinda waache wenye uwezo nao waitekeleze huna haja ya kuwasakama waache na sera zao…..
KWAME NKURUMA, MWALIMU NYERERE, SOKOINE, LUMUMBA,WARIOBA WATAENDELEA KUHESHIMIKA KAMA VIELELEZO VYA UZALENDO KWA MATAIFA YAO...HAKUNA KILICHOWATENGANISHA NA UPENDO WA MATATIFA YAO, IWE NJAA, IWE SHIBE, IWE NI WAKATI WAKIWA MADARAKAI AU LA, HAWAKUYUMBA WALICHOKIAMINI WALIKITETEA hata baadhi yao kuuawa
kwani walijua mwanadamu kula matapishi yake ni dalili ya uendawazimu hakuna jina lingine

UMEANDIKA HISTORIA KATIKA TAIFA LETU MREMA na ITAKUHUKUMU

Hongera kwa analysis ya ukweli.
 
Siku ya ukombozi wa pili wa Taifa letu ikifika, Mrema nawe tafuta pa kutokea maana kwani umjiatambulisha na mafisadi na wahujumu wa mama yetu Tanzania.
 
Huyu mzee anatafuta pa kufia tu, mara nyingi mtu akikaribia kukata roho anakuwa anahangaika na kusemasema ovyo, kikombe cha babu ndiyo hivyo kimedunda, afya inazidi kutetereka.
 
Chadema wakichukua madaraka inaonekana ni wengi watajinyonga! Wa kwanza ni Zombe, na huyu bwana naona kama anataka kufuata mkumbo!
Wakati wa uchaguzi aliwaomba wapiga kura wake wampigie kura AKAFIE BUNGENI- anadhihirisha kifo chake hapo alipo anaandaa utitili wa watu kutoka CCM wa kumzika.
 
Tatizo la mtoa hoja amesahau kuwa watz ni "wavivu" wa kusoma, ameandika gazeti zima!

Haishangazi. Wakina mrema mko wengi. Hii hali ya umaskini wa nchi yetu kwa sasa wengi watachanganyikiwa sana. Tutegemee kuona wengi wakiokota makopo barabarani na majalalani. Mtoa hoja ameandika kwa umahili mkubwa kwamba pamoja na kuandika "gazeti" uliloliona wewe
text and the contents kama alivyoeleza ndio ukweli wenyewe. HONGERA SANA MTOA HOJA achana na pumba pumba hizo zinazokejeli
 
Mrema amefika mahali leo anahoji eti kwanini watu wanamshangaa yeye ku attend mkutano wa taifa wa chama tawala....anashindwa kujiuliza kwanini watu hawakuwalaumu watu au wapinzani wengine waliohudhuria kikao hicho....mrema una historia ya kukataa kwenda ikulu ya mkapa kufanya nae mazungumzo kisa mkapa alisema kuwa ...kiongozi wa upinzani akitaka kuja kuniona sharti akatae hadharani dhana nzima maandamano yanayoleta fujo (hii ilikuwa ni baada ya Jan 27 cuf walipouawa znz, na pia akija awe na HOJA SI KUJA KUPIGA PICHA NA RAIS...mrema ulisema kamwe huwezi kuvumilia kejeli hizi za ben na hivyo huna haja ya kufika magogono kwa mazungumzo....muda mfupi baadae unaonekana kwenye mkutano uliojaa kila vijembe dhidi ya wapinzani na wewe ukainuka kuchangia kwa kujipendekeza....bado unataka tukusifi au tunyamaze kimya....unastahili kuitwa msalitiwa wa wapigania haki na maendeleo na sio kibaraka tu

mix with yours
 
hi Mrema anaJIKOMBA kwa JK ili arudishiwe marupurupu eti ya Naibu Waziri Mkuu! kama alivyorudishiwa Maalim Seif ya Waziri Kiongozi. hivyo "kubusu makalio ya Boss"( kiss your boss ass") ili apate ofa hiyo kwake ni Muhimu. Pia ana Wivu na wanaCDM kwa jinsi wanavyomwagiwa sifa na Walalahoi wa taifa hili. Mrema hana Jipya akafie zake huko anakojiKOMBA. Na haya marupurupu hatakaa apate hata akirudi CCM.
 
Huyu shuhuda wa babu wa loliondo sijui kwanini alipewa kikombe, hana haja ya kujinyonga atanyongwa na sukari. Ile ni kesi ukimkamata ukamlisha sukari kinaeleweka parapanda za kutosha tunawapelekea vunjo kichwa chao walichoona kinafaa kuwawkilisha bungeni.
 
PEOPLE..LEO MREMA AMEKULA CHUMVI NYIE HAMJALA.SASA AMEBAKIZA MIAKA MINGAPI??? NA NI KWA NINI AFE KWA PRESSURE SASA??MWACHENI MZEE WA WATU AFANYE AWEZAYO ILI MRADI ASIFE KWA AIBU.BADO NINAAMINI ANA AKILI YA KUEGEMEA PENYE UZITO KULIKO KUJISHIKA NA BUA. DO YOUR BEST MR MREMA You are very near to 7.00pm you must go sleep. Hakikisha wajukuu wana urith wa kutosha.MAY GOD BLESS YOU
 
Back
Top Bottom