Wadau,
Mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema ameyalaani vikali maandamano ya Chadema yanayoanza kesho nyanda za juu kusini. Mrema anadai kwamba CHADEMA wanaandamana kudai mambo ambayo tayari serikali inayafanyia kazi..ametoa mfano wa katiba mpya.
Mrema ameenda mbali zaidi na kusema kwamba CHADEMA wanataka kuvuruga amani na kuleta uchochezi ili nchi isitawalike. Amewasihi polisi wawazuie CHADEMA na kuvuruga mikutano na maandamano yao.
Mrema anajidai kusema kwamba eti yeye ndiye mwenye uchungu na nchi hii na ndio maana anakamata viongozi wa halmashauri wanaoendekeza vitendo vya ufisadi.
Hakika kila mtu aliyemsikia Mrema amejiuliza mara mbilimbili yeye ni nani hata aisemee serikali????
Mrema ana maoni gani kuhusu maandamano ya CCM jana huko Rukwa? Mrema na TLP wana maoni gani kuhusu katiba, kupanda kwa gharama za maisha, na kudorora kwa maadili kwa viongozi wetu? Ni aibu mno kwa mwanaume mzima kuaga familia kila siku asubuhi anaenda kazini kumbe kazi yenyewe ni u-kibaraka. total humiliation.