Mrejesho wa Pesa nilizozipata kwenye ATM

Mrejesho wa Pesa nilizozipata kwenye ATM

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2017
Posts
10,666
Reaction score
19,394
Majuzi nilileta uzi humu kwamba kuna pesa nimezipata kwenye ATM nilipokwenda kufanya muamala usiku. Pesa hizo ziliachwa na mtu ambaye naamini alikua amezidiwa na kilevi

Nilipata ushauri mwingi wa aina tofauti kuhusiana na ama kuzitumia au kumrejeshea pesa hizo muhusika ambaye kwakweli simjui hadi muda huu. Nimeuthamini sana sana ushauri wote niliopewa na wadau humu jukwaani na hata PM, na naomba Mola Awabariki wote waliotoa maoni kwani naamini walikua na nia njema hata wale walioniponda kwamba eti hii ni chai

Jana Jumatatu nilikwenda kuonana na Relationship Manager wangu na akaniambia wakati wanashughulikia hilo jambo niziweke hizo pesa kwenye account yangu wao wata zi block/hold na watu wa reconciliation watajua ni za wapi na kama kuna complain yoyote na mwisho wa siku watanijulisha
Nilipongezwa na kushukuriwa kwa hatua niliyochukua na kwamba imenijengea imani. RM wangu akanambia yapo matukio machache ya namna hiyo yanatokea na mara zote watu huwa wanasepa na pesa lakini huishia kujulikana na kuaibika maana camera na technolojia zingine zikitumika itajulikana tu. Akasema kuna Mbunge tena alishawahi kua Waziri miaka ya nyuma aliumbuka baada ya kuondoka kwenye ATM na pesa zisizokua zake!!!

Bado sijapigiwa simu wala kwenye simu yangu hakujaingia ujumbe wowote wa kuonyesha kufanyika kwa muamala wowote lakini nahisi nimeutua mzigo flani uliokua unanipa wasiwasi na shauku ambayo siwezi kuilezea

Mkuu uliyesahau pesa zako ATM tuwasiliane uweze kuzichukua - JamiiForums
 
We sio msamalia mwema bali ni mshamba tu, unarudishaje hela ya mlevi? mimi ningeenda kutoa kwa watu wenye mahitaji maalumu kama yatima, wenye ulemavu n.k, Huyo mlevi hata hajui kama siku hiyo alienda ATM. Ye anachojua pesa aliyokua nayo alihonga yote.
 
We sio msamalia mwema bali ni mshamba tu, unarudishaje hela ya mlevi? mimi ningeenda kutoa kwa watu wenye mahitaji maalumu kama yatima, wenye ulemavu n.k, Huyo mlevi hata hajui kama siku hiyo alienda ATM. Ye anachojua pesa aliyokua nayo alihonga yote.
Ushamba saa zingine unaokoa ndugu yangu, hata kama ningetumia hizo pesa ingejulikana wangekata kwenye akaunti yangu kiulaiiini kabisa mkuu
 
Ushamba saa zingine unaokoa ndugu yangu, hata kama ningetumia hizo pesa ingejulikana wangekata kwenye akaunti yangu kiulaiiini kabisa mkuu
Na kama isingejulikana? Kwa hiyo umerudisha kwa sababu unaogopa itajulikana? hivi kwanini watu huwa wanafikiria negatively kabla ya kujaribu jambo
 
Hongera mkuu siku zote uaminifu ni mtaji,haijalishi uwe tajiri au masikini ukiwa muaminifu basi umejenga mtaji wa kuaminiwa na watu.
Asante mkuu maana ningezitumia au hata kuzigawa ingenichafulia jina Bank na pia wangenikata kwenye akaunt yangu lakini kubwa zaidi dhamira yangu ingenisuta siku zote kua nimemuibia mtu jasho na haki yake
 
We sio msamalia mwema bali ni mshamba tu, unarudishaje hela ya mlevi? mimi ningeenda kutoa kwa watu wenye mahitaji maalumu kama yatima, wenye ulemavu n.k, Huyo mlevi hata hajui kama siku hiyo alienda ATM. Ye anachojua pesa aliyokua nayo alihonga yote.
Mkuu, mwenye pesa hapangiwi matumizi,
Hata kama ni wewe umetafuta pesa kwa bidii ni vema ukazitumia kwa namna yoyote unayoona inafaa ilimradi huvunji sheria,
Hata kama jamaa ni mlevi lakini haiondoi hiyo kama ni haki take, btw hujui ilikuwaje mpaka akanywa pombe cku hiyo,
Jamaa hata kama utamuita mshamba haisaidii kama unaijua vizuri nguvu ya technolojia nadhani utaiona aibu anayoikwepa mbeleni,
Mwisho kutoa msaada kwa wenye uhitaji ni jambo jema lakini haihitaji mtelezo
Fanya kazi katika sehem ya matumizi yako wakumbuke usisubiri mpaka upate fedha usiyoifanyia kazi ndio ukatoe msaada.
 
Na kama isingejulikana? Kwa hiyo umerudisha kwa sababu unaogopa itajulikana? hivi kwanini watu huwa wanafikiria negatively kabla ya kujaribu jambo
Kwenye uzi wangu wa mwanzo niliweka wazi dhamira yangu kua asipojitokeza muhusika wa hizo pesa nitazitoa sadaka, mimi nisingeweza kuzitumia maana haikua haki yangu

Suala la kujulikana ni ushauri na maoni ya watu waliotoa kwenye uzi ule, sasa nimepiga ndege wawili kwa jiwe moja mkuu. Nia yangu ya kumpata muhusika itaenda kutimia na atarudishiwa pesa zake, lakini pia nimetunza heshima na uaminifu na bankers wangu
 
Ushamba saa zingine unaokoa ndugu yangu, hata kama ningetumia hizo pesa ingejulikana wangekata kwenye akaunti yangu kiulaiiini kabisa mkuu
Sio kweli huyo Meneja wa Bank alikuwa anakupa tu mifano isiyokuwa na maana wanashindwa kukata hela wanazozilocate kwenye acc ya mtu bahati mbaya ije kuwa pesa ambayo mtu mwingine ametoa we umeokota tu? We ni mwoga tu au una pesa mingi sana .....lkn hiyo ilikuwa bahati yako wala hakuna ambae angafuatilia
 
Mkuu, mwenye pesa hapangiwi matumizi,
Hata kama ni wewe umetafuta pesa kwa bidii ni vema ukazitumia kwa namna yoyote unayoona inafaa ilimradi huvunji sheria,
Hata kama jamaa ni mlevi lakini haiondoi hiyo kama ni haki take, btw hujui ilikuwaje mpaka akanywa pombe cku hiyo,
Jamaa hata kama utamuita mshamba haisaidii kama unaijua vizuri nguvu ya technolojia nadhani utaiona aibu anayoikwepa mbeleni,
Mwisho kutoa msaada kwa wenye uhitaji ni jambo jema lakini haihitaji mtelezo
Fanya kazi katika sehem ya matumizi yako wakumbuke usisubiri mpaka upate fedha usiyoifanyia kazi ndio ukatoe msaada.
Hakuna kitu kama hicho,kwanza watu wa bank hawana muda wa kufuatilia video kama hizo hizo hela jamaa kaenda kumpa zawadi tu meneja atakaa muda hata mwezi mmoja atazitoa hizo hela na atazitumia yeye
 
Mkuu, mwenye pesa hapangiwi matumizi,
Hata kama ni wewe umetafuta pesa kwa bidii ni vema ukazitumia kwa namna yoyote unayoona inafaa ilimradi huvunji sheria,
Hata kama jamaa ni mlevi lakini haiondoi hiyo kama ni haki take, btw hujui ilikuwaje mpaka akanywa pombe cku hiyo,
Jamaa hata kama utamuita mshamba haisaidii kama unaijua vizuri nguvu ya technolojia nadhani utaiona aibu anayoikwepa mbeleni,
Mwisho kutoa msaada kwa wenye uhitaji ni jambo jema lakini haihitaji mtelezo
Fanya kazi katika sehem ya matumizi yako wakumbuke usisubiri mpaka upate fedha usiyoifanyia kazi ndio ukatoe msaada.
Asante sana mkuu kwa maneno yenye busara ya hali ya juu sanaa
 
Sio kweli huyo Meneja wa Bank alikuwa anakupa tu mifano isiyokuwa na maana wanashindwa kukata hela wanazozilocate kwenye acc ya mtu bahati mbaya ije kuwa pesa ambayo mtu mwingine ametoa we umeokota tu? We ni mwoga tu au una pesa mingi sana .....lkn hiyo ilikuwa bahati yako wala hakuna ambae angafuatilia
Naomba nitofautiane na wewe hapo mkuu. Bank washindwe kukakata pesa ambazo zimekua wrong posted kwenye account yako? Tena na wao wenye ndio wame miss post!!!? Hakuna bank ya namna hiyo
 
Back
Top Bottom