Mrejesho: Maneno ya kejeli ya mume wangu

Mrejesho: Maneno ya kejeli ya mume wangu

Duuuhh kazi kweli kweli. Napenda kulaa tabia mbaya na chafu aliyokuonyesha mumeo. Inatia simanzi kama sio kuvunja moyo.

Nakupa hongera kwa hatua uliochukua kwa kuhakikisha unaitafuta haki yako.

Napenda kutoa lawama zangu kwa familia (baba & mama) kwa kashindwa kutoa malezi bora kwa mumeo. Na si mumeo tu bali inasikitisha kuona watu wanakuwa kero au karaha kwa jamii badala ya kuwa furaha. Wazazi watambue/tutambue wajibu wetu wa "kuumba" watu wanyenyekevu wa moyo na wenye kuwa faraja na karaha ktk jamii.

Siku zote nimekuwa nikiwashangaa wabunge wa viti maalum kwa kushindwa kutetea utungaji wa sheria yenye tija kwa wanandoa wenye kuonewa na kunyanyaswa. Sheria iliyopo imejaa urasimu na haitoi haki ktk Muda muafaka.

NB:
 
Pole sana dada Mungu atukufungulia milango ya baraka mara mia. Mali hutafutwa , muhimu tafuta amani ya moyo wako . Mshukuru Mungu kwa yote .
 
Mali inapatikana kila siku, mwachie kila kitu hata hilo gari anza upya. Muda si mrefu ulivyomwachia vitachakaa na hatoweza kujitafutia vingine. Usipoteze muda wako kukimbizana na watu wenye roho mbaya kiasi hiki.

Asante kwa ushauri wako, ilikuwa ngumu mimi kuendelea kukaa pale kwanialikuwa anaitishia hadi nikareport polisi, familia yangu hasa mama yangu akaniambia nakuomba utoke kwenye hiyo nyumba kwani anaweza kukufanyia jambo baya. Pia nisinngeweza kukaa pale nyumbani kwa amani na hii pia ingeathiri kazi yangu ambayo ni muhimu sana kuliko hata hiyo nyumba. Kuhusu gari najua nitaipata kwa vyovyote vile.
 
Gari alinikuta nalo kabla hatujaoana, baadaya kufunga ndoa mimi nikapewa gari ya ofisi nikawa naitumia, kwa kuwa yeye hakuwa na gari nikampa ile ya kwangu ili aitumie, Mwaka jana ikapata yeye alikuwa ndio anaiendesha ikawa total demage na insurance wakalipa nikanunua gari nyingine kwa ile pesa ya insurance. So haikuwa sehemu ya mali ya wanandoa
Dada yangu; Gari hilo litakuwa sehemu ya mgao na nyumba pia itakuwa sehemu ya mgao. lakini kama mna watoto nyumba haitagawanywa kwa mtu yoyote yule. Mahakama itaamua ni nani ataishi na watoto kweny hiyo nyumba. Ila kama hakuna watoto, itagawanya au wafanye estimates halafu huyo jamaa akulipe portion of you contribution. trust me; gari hilo litakuwa sehemu ya division coz lilinunuliwa wakati mko kwenye ndoa regrdless where the cash/proceeds come from. I was in the same situation; Trust me, wakati mahakama watakapo toa samons, najua huyu jamaa hatofika mahakamani. you will come back n tell me. Kwa hiyo jiandae jinsi ya kukabiliana na huyo jamaa endapo kama atakataa/kutotoa ushirikiano kuja mahakamani.
 
Daaaah pole sana mama, hivi wanaume mna nini? Kwenye hizi ndoa wanawake ndio wahanga zaidi.
 
Dada yangu; Gari hilo litakuwa sehemu ya mgao na nyumba pia itakuwa sehemu ya mgao. lakini kama mna watoto nyumba haitagawanywa kwa mtu yoyote yule. Mahakama itaamua ni nani ataishi na watoto kweny hiyo nyumba. Ila kama hakuna watoto, itagawanya au wafanye estimates halafu huyo jamaa akulipe portion of you contribution. trust me; gari hilo litakuwa sehemu ya division coz lilinunuliwa wakati mko kwenye ndoa regrdless where the cash/proceeds come from. I was in the same situation; Trust me, wakati mahakama watakapo toa samons, najua huyu jamaa hatofika mahakamani. you will come back n tell me. Kwa hiyo jiandae jinsi ya kukabiliana na huyo jamaa endapo kama atakataa/kutotoa ushirikiano kuja mahakamani.

Hatukufanikiwa kupata mtoto, ila gari ni replacement ya damage ya gari ambayo ni ya gari yangu ambayo nilinunua wakati hatujafunga ndoa. Anyway hata vikigawanywa pamoja wala sitojali ilimradi haki yangu ipatikani. Chanve ya yeye kuja mahakamani ni ndogo kwa sababu hakuweza kutoa ushirikiano ngazi ya familia na baraza la kata.
 
Hivi huyu dada uselfish wake uko wapi????
Nyumba kamuachia mwanaume kapangisha...bila kukubaliana nae. Kwa lugha nyingine kodi kalamba yeye na hawara yake.

The gari alonunua kwa pesa yake pia kachukua anatumia na hawara yake....

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni






Kwa hiyo huyu dada its okey kuondoka na begi lake la nguo tu???
haki ni lazima itendeke mahakamani.
 
''kapangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu''.........
Nahisi uongo hapa.... Haiwezekani yote haya yatokee.....Wanawake wengi wanatabia ya kusema uongo hasa linapokuja swala la talaka na kuachana na waume zao.
 
Nacherewa

Tafuta mishumaa miwili myekundu
Tumtengeneze fastaaa.
 
Last edited by a moderator:
Kweli wanaume wa kiafrika tumelaaniwa japo sio wote hatupo romantic kuanzia kwa wapenzi wetu hadi wake zetu, na inakuaje unashindwa kuigiza hata kama unachepuka kiaina ili asijejua na uhakikishe unamlindia heshima mkeo mbele ya jamii?
 
Pole sana dada kwa yote yalokukuta,usijali ila itafute hiyo haki yako na mungu atajaalia utaipata tu,mwache huyo takataka anza maisha yako mapya na mungu atakusimamia,maisha haya ni mapito tu,hakuna atakayeishi milele lkn pia mtangulize na mwombe mungu sana akusimamie ktk hili
 
Gari alinikuta nalo kabla hatujaoana, baadaya kufunga ndoa mimi nikapewa gari ya ofisi nikawa naitumia, kwa kuwa yeye hakuwa na gari nikampa ile ya kwangu ili aitumie, Mwaka jana ikapata yeye alikuwa ndio anaiendesha ikawa total demage na insurance wakalipa nikanunua gari nyingine kwa ile pesa ya insurance. So haikuwa sehemu ya mali ya wanandoa

Naomba kueleweshwa hapa. Kisheria, mali ambayo mwanandoa amekukuta nayo say kiwanja/ shamba haihesabiki kama sehemu ya mali ya wanandoa? Kuna ahadi fulani husemwa kanisani (baadhi ya dini za kikristo) kuwa " nakushirikisha kwa mwili wangu na Mali zangu za duniani" hii huwa ni Mali zipi kama sio ulizonazo kabla ya ya ahadi?. Tafadhali naomba ufafanuzi kwa wajuzi.
 
Songa mbele katka kudai haki yako
NB. Life is a game of individuality
 
''kapangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu''.........
Nahisi uongo hapa.... Haiwezekani yote haya yatokee.....Wanawake wengi wanatabia ya kusema uongo hasa linapokuja swala la talaka na kuachana na waume zao.

Sasa ndio yametokea yote hayo, ndugu zake wanajua, serikali ya mtaa wanajua na kata wanajua so mimi sidanganyi na haya yametokea. Wazazi wake na ndugu zake upande wa baba wamemsusia wamesema niende mahakamani nikadai haki yangu na wako pamoja na mimi kwa sababu wananifahamu vizuri na jinsi nilivyohangaika na mtoto wao.

Hii ni messege aliyonitumia baba yake mzazi nanukuu ''Mama nakupenda sana hujanikosea hata siku moja hata kama mtaachana mimi usinitupe, kuhusu suala ya kusimamia huyo mwanangu mimi siwezi nimeshindwa, nenda serikali ya mtaa, polisi au mahakamani upate haki yako'' mwisho wa kunukuu. Hii messege ninayo mpaka sasa hadi nimeiprint kabisa
 
Toka ameanza kuhangaika alishawahi pata hata mimba yakusingiziwa ?
 
gari alinikuta nalo kabla hatujaoana, baadaya kufunga ndoa mimi nikapewa gari ya ofisi nikawa naitumia, kwa kuwa yeye hakuwa na gari nikampa ile ya kwangu ili aitumie, mwaka jana ikapata yeye alikuwa ndio anaiendesha ikawa total demage na insurance wakalipa nikanunua gari nyingine kwa ile pesa ya insurance. So haikuwa sehemu ya mali ya wanandoa
wewe ndio utakuwa una tatizo sio mleta mada
 
Back
Top Bottom