Mrejesho: Maneno ya kejeli ya mume wangu

Mrejesho: Maneno ya kejeli ya mume wangu

Nacherewa

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2015
Posts
285
Reaction score
457
Habari za asubuhi wana JF

Mwezi wa saba nilipost mkasa kuhusu matatizo na mume wangu https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/876139-maneno-ya-kejeli-ya-mume-wangu-10.html

Baada ya kupata ushauri kutoka kwa wana JF, ndugu zangu na upande wa mume niliamua kuongea naye kuhusu tabia zake, lakini hakuweza kubadilika. Siku moja aliondoka kwenda Msata kama alivyodai mwezi mzima bila kuaga wala kujua naishije pale nyumbani. Siku zote hizo hakuwa anapiga simu mpaka mimi ndio nimpigie.

Nilichukua uamuzi wa kumuomba baba yake amuite ili tuweze kuyaongea kama familia zote mbili. Baba aliitisha kikao cha kukutana na familia za pande zote lakini alikataa kuja na kusema mimi niondoke pale nyumbani na asinikute maana ataniumiza.

Nikaamuakupeleka shauri baraza la kata kwasababu imeshindikana kwa ngazi ya familia. Kata nako aliitwa mara tatu lakini hakufika. Kumbe siku zote hizo yuko hapahapa Dar anaishi na yule mwanamke ambaye alimtambulisha polisi kama mke wake na pia alishawahi kumleta pale myumbani.

Mimi nikachukua uamuzi wa kuondoka pale nyumbani chini ya mjumbe na mjomba wake nikaenda kwa dada yangu. Siku hiyo naondoka nilikutana naye njiani anarudi nyumbani akiwa na yule mwanamke, kumbe alimuambia mjomba wake akiondoka tu mke wangu uniambie mimi niko karibu nitakuja.

Alipofika pale nyumbani siku ileile aliondoka na vitu vyote pale nyumbani na akaweka mpangaji baada ya siku mbili yeye akaondoka akarudi kwa yule mwanamke. Jana baraza la kata limenipa barua ya kwenda mahakamani kudai talaka na madai mengine baada ya huyu mwanaume kushindwa kutoa ushirikano baraza la kata.

Nimeshafungua kesi mahakama ya mwanzo na leo ndio taandikiwa wito wa kumuita mahakamani. Pamoja na kupangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu.

Nawashukuru sana wana JF kwa michango yenu, pia na member mmoja ambaye amekuwa msaada mkubwa kwangu mpaka nafikia hatua hii. Michango yenu ni muhimu sana hasa kipindi hiki cha kudai haki yangu.

Asanteni sana

Mungu awabariki sana
 
nampongeza memba aliyekushika bega mpaka umefikia hapo.... pole sana mama muhimu ni talaka hapo huna mume hapo
 
Very very good. Maisha yanaendelea hata bila yeye, songa mbele.
 
Pole dada.

Kwa vile umeshafika kote huko basi tusubir uamuzi wa cort
 
Wanaume aliyeturoga kafa na huyo mwanamke wake anaona sawa kuvunja ndoa ya mwanamke mwenzake.
 
Pole dada..ila usikatw tamaa wapo wanaume wa kweli..usifunge mlango wa mapenzi...ila nakuambia huyo kapewe libwata..likiisha atakutafuta..yaani aiku hizi wadada wamujini kazi waganga na madawa kuharibu nyumba za wenzao..muombe mungu atakaekuja awe mcha mungu maana hii ndio dawa kwa sasa
 
daah i feel so sad kwa yanayokukuta.....mimi sina msaada sana zaidi ya kukutakia maisha mapya mema jipe muda wa kutafakari upya maisha yako lakini usisahau kitu kimoja....maisha lazima yaendelee.....ila haki yako lazima ipatikane kwa vyovyote vile ata nyumba ikibidi iuzwe mgawane..ila gari arudishe haraka sana uyo kiazi mbatata....mwisho kabisa ukishamaliza huo mpango wa talaka na kugawana mali tulia kidogo then endelea na maisha ya mapenzi usithubutu kukaa chini ukalia sababu ya huyo kiazi asiejitambua....narudia tena usithubutu...kila la heri dada
 
Kama hiyo gari ulinunua wewe nakushauri uifate na ukaichukue mara moja kabla haijaharibika ili ikusaidie.
 
pole sana,alipoanza kukusumbua hiyo gari ungemnyanganya,halafu kwann ulitoka ktk Nyumba mliojenga wote?ungemwacha aendelee kukaa KWA kimada wake we ungebaki na NYUMBA!nakutakia mafanikio ktk kufuatilia haki zako
 
pole sana,alipoanza kukusumbua hiyo gari ungemnyanganya,halafu kwann ulitoka ktk Nyumba mliojenga wote?ungemwacha aendelee kukaa KWA kimada wake we ungebaki na NYUMBA!nakutakia mafanikio ktk kufuatilia haki zako

Asante kwa ushauri wako, ilikuwa ngumu mimi kuendelea kukaa pale kwanialikuwa anaitishia hadi nikareport polisi, familia yangu hasa mama yangu akaniambia nakuomba utoke kwenye hiyo nyumba kwani anaweza kukufanyia jambo baya. Pia nisinngeweza kukaa pale nyumbani kwa amani na hii pia ingeathiri kazi yangu ambayo ni muhimu sana kuliko hata hiyo nyumba. Kuhusu gari najua nitaipata kwa vyovyote vile.
 
Nacherewa

Dada yangu pole kwa yaliyokukuta; nakukumbusha kitu hapo kwenye uzi wako,........''kupangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu'', Nyumba mlijenga wote, Je Gari alikukuta nalo? Kama jibu ni hapana; then you are too selfish...., any way, wanawake ndio mlivyo, kama jibu ni ndio; basi inabidi uprove mahakamani kuwa ulinunua kabla hamjaoana. Ila nahisi kuna dosari pia upande wako ambazo hujazika wazi. Ila nahisi wewe uko too SELFISH.....,
 
Last edited by a moderator:
Dada yangu pole kwa yaliyokukuta; nakukumbusha kitu hapo kwenye uzi wako,........''kupangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu'', Nyumba mlijenga wote, Je Gari alikukuta nalo? Kama jibu ni hapana; then you are too selfish...., any way, wanawake ndio mlivyo, kama jibu ni ndio; basi inabidi uprove mahakamani kuwa ulinunua kabla hamjaoana. Ila nahisi kuna dosari pia upande wako ambazo hujazika wazi. Ila nahisi wewe uko too SELFISH.....,

Gari alinikuta nalo kabla hatujaoana, baadaya kufunga ndoa mimi nikapewa gari ya ofisi nikawa naitumia, kwa kuwa yeye hakuwa na gari nikampa ile ya kwangu ili aitumie, Mwaka jana ikapata yeye alikuwa ndio anaiendesha ikawa total demage na insurance wakalipa nikanunua gari nyingine kwa ile pesa ya insurance. So haikuwa sehemu ya mali ya wanandoa
 
Hivi huyu dada uselfish wake uko wapi????
Nyumba kamuachia mwanaume kapangisha...bila kukubaliana nae. Kwa lugha nyingine kodi kalamba yeye na hawara yake.

The gari alonunua kwa pesa yake pia kachukua anatumia na hawara yake....

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni



Dada yangu pole kwa yaliyokukuta; nakukumbusha kitu hapo kwenye uzi wako,........''kupangisha nyumba ambayo tumejenga wote bila ridhaa yangu pia aliondoka na gari yangu'', Nyumba mlijenga wote, Je Gari alikukuta nalo? Kama jibu ni hapana; then you are too selfish...., any way, wanawake ndio mlivyo, kama jibu ni ndio; basi inabidi uprove mahakamani kuwa ulinunua kabla hamjaoana. Ila nahisi kuna dosari pia upande wako ambazo hujazika wazi. Ila nahisi wewe uko too SELFISH.....,


Kwa hiyo huyu dada its okey kuondoka na begi lake la nguo tu???
 
Back
Top Bottom