Mrejesho ajali ya coaster Tanga

Mrejesho ajali ya coaster Tanga

Mwendo kasi.kuna dogo wa bodaBoda.anaona magari yanakwenda polepole akaona anachelewa.aka overtake kushoto.kumbe mbele kuna lori limeharibika limepaki kushoto.na yeye yupo nduki.akajibamiza mwenyewe nyuma la lori.na safari yake ikaishi hapo hapo.ilikuwa saa moja usiku.
 
pole sana. hiyo coaster niliiona pongwe zikiwa zimeongozana mbili...yenu ilikuwa nyuma mida ya saa 1 jioni, usiku niliposikia ajali na kuona rangi ya gari nilihamaki sana. Ugua na uguza pole mwaya.
 
Pole sana. Mungu ni mwema. Inasikitisha sana hospitali teule kukosa umeme. Serikali iangalie vipaumbele muhimu.
 
pole sana. hiyo coaster niliiona pongwe zikiwa zimeongozana mbili...yenu ilikuwa nyuma mida ya saa 1 jioni, usiku niliposikia ajali na kuona rangi ya gari nilihamaki sana. Ugua na uguza pole mwaya.
Ilipita Pongwe kugombea abiria,shukrani
 
Huduma za kijamii (afya, elimu, maji, miundo mbinu kama mifereji kwenye makazi ya watu na mengineyo) sio muhimu sana, kipaumbele chetu ni flyovers, bombardier, reli, nk.
 
Daah pole sana bro.Mungi awatie nguvu na mtoto.Ila nimejifunza jambo ..hospital hizi..Unaweza kufa kama huna hela kwa wakati husika.Maana si wao wa kulaumiwa.Ni aina ya budget zetu za wizara husika.
 
Kadri siku zinavyokwenda utu wa mtu mweusi unazidi kuporomoka kwa kasi ya ajabu sana, Imagine watu wamepata ajali mijitu mingine inakuja badala ya kutoa msaada..inafikiria kuiba mali za wahanga wa ajali, tatizo ni umasikini au roho mbaya sijui..hii sio poa kabisa! By the way pole sana kwa yaliyokukuta katika ajali!
 
Acha Mungu aitwe Mungu, Mungu aliekuokoeni ndie atakae kuponyeni. Nashindwa kuelezea huzini yangu ila Poleni sana sana
 
View attachment 506991 Tarehe 7/ May nilikuwa miongoni mwa abiria,nikiwa na mtoto wangu 3yrs old tukitoka kumsalimia Babu yake Tanga mjini.
Ajali ilipotokea ni umbali wa dakika 3 mpaka kituo tulichokuwa tushuke. Dereva akiwa speed kwenye kujaribu kuovertake,akaona mbele gari inakuja kasi na pembeni kuna koronga na Scania lilipark,tukasikia break kali na mayowe yakatamaaki.

Dalili ya ajali ilijia,nikamkumbatia mwanangu mapajani huku kalala,dereva akachomeka upande kwenye roli,mshindo mkubwa,mtoto akaanguka chini,nikarushwa mbele kidogo. Mtoto akaanza kulia,nimebanwa na siti kwenye mguu,ikavuta na watu,mtoto akaokotwa,hali ya kuchanganyikiwa ikanijaa,nikajikaza nabubuj8ka damu kichwa kizima,nikatoka na dirishani nikipiga yowe namtaka mwanangu!

Nilijibiwa kashapelekwa hospital,watu wakizidi kujaa kushangaa bila ya wengi kutoa msaada,vijana wakijazana kwenye basi huku nikiugulia chini baada ya nguvu za kysimama kuniisha huku nikipaza sauti "naomba mnipeleke hospital"

Dada mmoja akaja akanifunga na kanga yake kichwani kwani damu zilizidi,akaenda ndani ya bus,hatimae msamaria mwema mmoja akanibeba na mwenzie kwenye pikipiki na kuniwahisha hospital. Nikampa simu yangu awap8gie wazazi na ndugu,simu nyingine ziliibwa,hata saa ya mkononi dikumbuki nilivuliwa saa nggapi japo sikuzimia,Mungu mkubwa!

Nikamkuta mwanangu akishonwa huku akimlilia baba,nikalazwa pembeni yake,akaniona,akapunguza kulia,akapelekwa ward ya watoto.

Nikashonwa kichwani kwa zaidi ya masaa mawili na kibatari pia umeme ulipikatika,bila ganzi,wakahamia na mkononi ila baadhi nikagoma waniache,maumivu ya nyama za mkono yalizidi,hiyo ni hospital ya teule.

Kesho hadi saa 8 mchana sijafanyiwa dressing ya vidonda,kisa umeme hamna na vyombo havijachemshwa,tukapambana nikahamia hospital ya mkoa baada ya wazazi na ndugu kuja juu.

Nashukuru Mungu,naimarika,nafarijika.

Well,wanasema watoto ni malaika,I reserve my comment ila wakati tunapanda mtoto alichagua siti ya mwisho kabisa,nikamwambia njoo huku,akasema hapa,huku,hapa,hatimae akanitii akaja,akakaa dirishani. Nilimchagulia siti karibu na mbinuko wa tyre ili aweze kukanyaga vizuri pia watu wawili,he is 3yrs old.

Siti aliyochagua hakuna aliyekufa,siti yetu tumejeruhiwa,wa mbele yetu wanne walifariki palepale. Mungu awarehemu.

Naendelea kyjiuguza,Ahsanteni,mbarikiwe!
Pole sana Mkuu, Allah akufanyie wepesi katika kupona InshaAllah.
 
Hospital zetu hapa nchini zinakatisha tamaa sana! Imagine mtu anashonwa zaidi ya masaa mawili bila ganzi + umeme hakuna. Pole sana mkuu
Hizo ndizo gharama za CCM ambazo huwezi kuziona mpaka ufikwe na majanga mkuu. Ndipo unapopaswa kujiuliza vipaumbele vyetu ni vipi tofauti na zamani tukiambiwa tuna maadui watatu wakuu: 1. Ujinga. 2. Umasikini na 3.Maradhi.
Laiti tungeliondoa ujinga, umasikini ungeondoka na afya zingeimarika!! Lakini kwa kuwa watawala wana vipaumbele vyao hayo mambo matatu yataendelea kuwa mwiba mpaka tutakapobadilika kwa kutambua nani anatusababishia hao maadui waendelee kuwepo.
Ikiwa nilipata ajali mwaka 1998 nikashonwa mguu bila ganzi mpaka leo ugonjwa ni uleule bado tunaimbiwa nyimbo umeme na afya vimeimarika napata shida kidogo kuelewa!!
 
Back
Top Bottom