Mramba anasafishwa?

Mramba anasafishwa?

Kwa hiyo wabunge wote wa CCM walioenda kumpa pole Mramba (na kumkumbatia!) ni ndugu zake? Tueleze basi kama na wewe ni ndugu yake. Hebu basi soma post ya Alpha hapo juu halafu utupe majibu. Naona unataka kupotosha mjadala kwa kutetea vitu ambavyo viko wazi tu!

Post nimeisoma vizuri tu.

Sijui mimi,wewe au na wewe nani hajaielewa. na sijui nani anatafuta sympathy na kama aliomba kukumbatiwa

Any way sinacomment zaidi.
 
Last edited:
Mimi nataka nyie wote mnaopinga.

KAMA ANGEKUWA NI BABA YENU AU REFIKI YAKO WA KARIBU UNGEFANYAJE?

SEMA UKWELI.


Mkuu Kanda2x2

Mbona unakuwa huelewi; angekuwa ni baba yangu ningemwambia; usijali baba angalau tumeshasoma ulaya, nyumba tumejenga dar na kule rombo na bado wewe ni mbunge. Ukifungwa jela tutakuja kukutembelea...

Lazima ukumbuke kuwa familia yake wamekuwa hizo hela pamoja naye hivyo ni muhimu wampe sapoti; hao wabunge badala ya kumuona adui wa yale wanayoyapigania bungeni wao wanampa hug...hawana hata aibu.
 
Mimi nataka nyie wote mnaopinga.

KAMA ANGEKUWA NI BABA YENU AU REFIKI YAKO WA KARIBU UNGEFANYAJE?

SEMA UKWELI.
Kwa wizi na ujambazi wa hawa wakina Mramba, kama angekuwa baba ningemsusia na si ajabu ningemzomea.
Baba mwizi au mama mwizi sina undugu wala urafiki naye.
Tena sikiliza wewe Kandambili, mwizi ni mwizi tu hata akiwa na kesi ambayo haijaamuliwa bado ni mwizi. Na hata wakimu aquit mahakamani bado haitaondoa wizi wake. Kama aliiba atabaki ni mwizi tuuuuuuuuuuuu.
Ebu soma hiyo signature yangu ndugu.
 
Kwa wizi na ujambazi wa hawa wakina Mramba, kama angekuwa baba ningemsusia na si ajabu ningemzomea.
Baba mwizi au mama mwizi sina undugu wala urafiki naye.
Tena sikiliza wewe Kandambili, mwizi ni mwizi tu hata akiwa na kesi ambayo haijaamuliwa bado ni mwizi. Na hata wakimu aquit mahakamani bado haitaondoa wizi wake. Kama aliiba atabaki ni mwizi tuuuuuuuuuuuu.
Ebu soma hiyo signature yangu ndugu.

MKuu, najua wewe ni mpambanaji na mchukia fisadi kweli. Lakini naomba usije ukaingia katika mtego na ukawa kama waziri wetu mkuu Pinda, to be caught up emotionally and throwing law out of the window.
Everybody is assumed innocent until proven guilty, au siyo? Mpaka sasa hatujaona ushahidi dhidi ya Mramba ni upi na hivyo hatuna budi kusubiri kesi yake iendelee tupate kujua zaidi. Nadhani hata wabunge walioenda kumpa pole walikuwa wanafanya hivyo in collegial gesture. Na si kitu kibaya.
Kupambana na ufisadi kunahitaji hekima, cool minds and even temper, ili siku watakapokamatwa waweze pia kushtakiwa na hatimaye kufungwa. Na si kushabikia tu.
 
Friends,
I have just three observations;
1. Was it proper kwa Wabunge ku-express public sympathy kwa Mh. Mramba? My opinion is no- They were neither to express sympathy nor to ignore. In my opinion wangem-treat with the business as usual attitude kama ambavyo wamekuwa wakifanya kabla ya hili zahama, wasubiri outcome then wa-respond kufuatana na outcome! By and large walichokifanya kinaleta tafsiri nyingi, na nyingi si nzuri, unafiki ikiwa inaongoza, ama kuamini kuwa yanayomtokea yote ni chuki binafisi, etc.
2. The notion of innocent till proven guilty- what do I think? My opinion ni kwamba bado hatujui mahakama itafikia conclusion gani na kwa sababu zipi? ili nataka kuhoji kuwa hata akiwa declared innocent na mahakama, ni wangapi tunaamini kuwa haki itakuwa imetendeka na kuwa kweli Mh. Mramba ni innocent kwenye charge hizo na nyingine zinazofanana na hizo ambazo hajashitakiwa nazo? Kama kweli tupo ambao conclusion ya mahakama ikiwa ni mu-declare innocent tutakubali kuwa kumbe yote haya yalikuwa uongo tu na defamation ya mtu safi, basi Mungu aibariki Tanzania!
3. Kama angekuwa mtu wako wa karibu ungefanyaje? My answer to that, is under such circumstances personal attributes zibaki kuwa personal, watu wake wa karibu ambao ni wafaidika wa kwanza na waathirika wa kwanza kwa mambo yanamhusu ndio wajue wana-deal vipi na hili! Wengine tuli-jadili kwa national interest because hatuna personal interests kwenye affairs zake!
 
Kwa wizi na ujambazi wa hawa wakina Mramba, kama angekuwa baba ningemsusia na si ajabu ningemzomea.
Baba mwizi au mama mwizi sina undugu wala urafiki naye.
Tena sikiliza wewe Kandambili, mwizi ni mwizi tu hata akiwa na kesi ambayo haijaamuliwa bado ni mwizi. Na hata wakimu aquit mahakamani bado haitaondoa wizi wake. Kama aliiba atabaki ni mwizi tuuuuuuuuuuuu.
Ebu soma hiyo signature yangu ndugu.

Je na baba yako au mama yako huyo huyo akikuambia kuwa mwanangu mi nimeanza wizi toka kabla hujazaliwa na fedha zote zilizokufikisha hapa kuanzia posa ya mama yako hadi malezi yako yote mpaka leo hii vyote vya wizi utafanyaje hapo?.
 
Je na baba yako au mama yako huyo huyo akikuambia kuwa mwanangu mi nimeanza wizi toka kabla hujazaliwa na fedha zote zilizokufikisha hapa kuanzia posa ya mama yako hadi malezi yako yote mpaka leo hii vyote vya wizi utafanyaje hapo?.

Kweli nitabaki na msimamo wa kuchukia ufisadi wao na wao sintawapenda maana siku wakiondoka mimi na watoto wangu na wajukuu wangu tutabaki katika kilio. Wizi wao utakuwa umenipa tiba ya muda kama vile wanavyofanya kwa uchaguzi maana hii hii miela wanaonga wapiga kura na wanawarudisha bungeni na wakirudi bungeni wanawabeza tena kuwa wale majani. Sioni faida yao kabisa.
Nina machungu mengi nikisimulia hapa utashangaa. Yote chanzo ufisadi huu huu. Ni hawa hawa walikuwa wakisema kwa majigambo kuwa tule majani tu wakati wao wanakula pesa yetu ndugu. Ndugu zangu wakikosa dawa hospitali. Haloooooooooooooooo.
Kama wanashabikiwa na wana wao, sawa lakini siku si nyiingi vizazi vya wana wao watalia tu. Hatutaruhusu wizi huu uendelee na tukae kimya tu. Iko siku tutawauliza hata wana wao.
 
Mimi nataka nyie wote mnaopinga.

KAMA ANGEKUWA NI BABA YENU AU REFIKI YAKO WA KARIBU UNGEFANYAJE?

SEMA UKWELI.

SASA KAMA NI BABA NINGEKUWA NIMESOMESHWA SHULE ZA ACADEMIA, NIMENUNULIWA GARI NIMEPELEKWA ULAYA NA NYUMBA KUPEWA SIKU YA HARUSI,LAZIMA NINGESIKITIKA...
KAMA NI RAFIKI NINGEKUWA NAHUDHURIA MI DINNER PARTY, NIMESAIDIWA KWENYE MI TENDER YANGU, NA NIMESAIDIWA WATOTO WANGU KWENDA NJE ofcourse ningesikitika, ila mimi ni mtanzania watoto wangu wamerudishwa chuo kikuu kwa sababu sina 40% ya kuwalipia, watoto wanaenda shule miguu mitupu, shule kama za Galanos hazina chakula zimefungwa kwa mwezi mzima looh halafu kuna mtu kwa uzembe anasababisha bilions za pesa zipotee kama kweli hawakugawana kwa kweli siwezi hata kumpa mkono samahani sana...
 
MKuu, najua wewe ni mpambanaji na mchukia fisadi kweli. Lakini naomba usije ukaingia katika mtego na ukawa kama waziri wetu mkuu Pinda, to be caught up emotionally and throwing law out of the window.
Everybody is assumed innocent until proven guilty, au siyo? Mpaka sasa hatujaona ushahidi dhidi ya Mramba ni upi na hivyo hatuna budi kusubiri kesi yake iendelee tupate kujua zaidi. Nadhani hata wabunge walioenda kumpa pole walikuwa wanafanya hivyo in collegial gesture. Na si kitu kibaya.
Kupambana na ufisadi kunahitaji hekima, cool minds and even temper, ili siku watakapokamatwa waweze pia kushtakiwa na hatimaye kufungwa. Na si kushabikia tu.

Nadhani tunahitaji msaada wa wataalamu kuhusu haya mambo ya sheria Vs mtazamo na imani ya jamii (public views and perception) linapokuja suala la kesi. Haya mambo ya mtu kuwa mtuhumiwa mpaka hukumu nadhani ni mambo ya kisheria hasa hasa kwa ajili ya kuwalinda wanyonge wasionewe. Hata Mramba ni mnyonge mbele ya serikali inayomshitaki kwa hiyo analindwa pia. Ila kuna suala la jamii na imani yake kuhusu usafi wa Mramba. Nadhani wananchi wengi wanaamini kuwa ni kweli Mramba ni mwizi na hajaonewa. Hapa naaminisha kuwa hukumu ya jamii dhidi ya Mramba iko wazi. Watu wanamjua toka akiwa mtoto hadi sasa na kwa hiyo kama ana kitu kinachotia shaka wanajua. Na wao hawana haja ya kusubiri hukumu ya mahakama ili waamini kwamba ni mwizi. Kwa hiyo sina shaka hata mimi kwamba ni kweli jamaa ni mwizi. Ndiyo maana ninawashangaa wote wanaojifanya kumwonea huruma.
 
MKuu, najua wewe ni mpambanaji na mchukia fisadi kweli. Lakini naomba usije ukaingia katika mtego na ukawa kama waziri wetu mkuu Pinda, to be caught up emotionally and throwing law out of the window.
Everybody is assumed innocent until proven guilty, au siyo? Mpaka sasa hatujaona ushahidi dhidi ya Mramba ni upi na hivyo hatuna budi kusubiri kesi yake iendelee tupate kujua zaidi. Nadhani hata wabunge walioenda kumpa pole walikuwa wanafanya hivyo in collegial gesture. Na si kitu kibaya.
Kupambana na ufisadi kunahitaji hekima, cool minds and even temper, ili siku watakapokamatwa waweze pia kushtakiwa na hatimaye kufungwa. Na si kushabikia tu.

In the face of law, ndio hivyo lakini kwa mshtaki everybody is guilty until proven innocent. Jamhuri kwa niaba ya WaTZ wote inaamini kuwa Mramba ana hatia ndio maana imempeleka mahakamani.
 
Na Nora Damian

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, imempa ruhusa tena waziri wa zamani wa Fedha ambaye pia ni Mbugne wa Rombo, Basil Mramba kwenda kuhudhuria na kufanya shughuli za bunge, kutokana na kesi yake ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni, kupangwa kuanza kusikilizwa Machi3, mwaka huu.


Kabla ya ruhusa hiyo, mahakama iliambiwa na upande wa mashtaka kuwa upelelezi wa kesi ya kutumia madaraka vibaya inayowakabili mawaziri wa zamani, Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja umekamilika.


Hayo yalielezwa jana katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na wakili wa serikali, Fredrick Manyanda mbele ya Hakimu Mkazi, Hezron Mwankenja ambaye alisema washitakiwa hao watasomewa maelezo ya awali Machi 3, mwaka huu.


Wakili anayemtetea Mramba, Hubert Nyange amewasilisha barua mahakamani hapo kuomba mteja wake aruhusiwe kuhudhuria vikao na shughuli nyingine za ubunge.


Barua hiyo iliwasilishwa mahakamani hapo Januari 30 mwaka huu.


Hakimu Mwankenja alikubali ombi hilo na kumruhusu Mramba kwenda bungeni kuendelea na shughuli nyingine za ubunge, lakini akaagiza awepo mahakamani Machi 3 mwaka huu kesi yao itakapotajwa.


Washitakiwa hao wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya Sh 11 bilioni.


Wanadaiwa wakiwa waajiriwa wa serikali walitumia madaraka yao vibaya na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart ya nchini Uingereza kinyume na ushauri uliotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


Souce: Gazeti la Mwananchi
 
Likizo yangu moja nilienda kutembea vijiji vya sehemu fulani hapa Tanzania. Kufika kule nikakutana na habari ya mwizi mmoja kuchomwa moto na wananchi wenye 'hasira kali'. Siungi mkono jambo hili.
Nilipouliza nikaambiwa waliiba siku Tatu zilizopita hapo kijijini na walionwa ila wakakimbia na walikuwa wamejificha mpaka siku walipoonwa walipojificha
Katika kuongea na wanavijiji wale nilipata kujua kuwa wezi pale hawavumiliki
Na sio rahisi mtu wa maeneo Yale akakua akawa mwizi
Maana ingine ni kuwa hizi tabia zina asili yake - kuanzia katika familia mpaka jamii inayo kuzunguka
Kama Mtoto akiiba tunamwita mjanja, jasiri, mjasiriamali na nk tunategemea nini akishakuwa ofisin? Ni kulizwa tu
 
Na Nora Damian

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es salaam, imempa ruhusa tena waziri wa zamani wa Fedha ambaye pia ni Mbugne wa Rombo, Basil Mramba kwenda kuhudhuria na kufanya shughuli za bunge, kutokana na kesi yake ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Sh 11 bilioni, kupangwa kuanza kusikilizwa Machi3, mwaka huu.


Kabla ya ruhusa hiyo, mahakama iliambiwa na upande wa mashtaka kuwa upelelezi wa kesi ya kutumia madaraka vibaya inayowakabili mawaziri wa zamani, Mramba, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja umekamilika.


Hayo yalielezwa jana katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na wakili wa serikali, Fredrick Manyanda mbele ya Hakimu Mkazi, Hezron Mwankenja ambaye alisema washitakiwa hao watasomewa maelezo ya awali Machi 3, mwaka huu.


Wakili anayemtetea Mramba, Hubert Nyange amewasilisha barua mahakamani hapo kuomba mteja wake aruhusiwe kuhudhuria vikao na shughuli nyingine za ubunge.


Barua hiyo iliwasilishwa mahakamani hapo Januari 30 mwaka huu.


Hakimu Mwankenja alikubali ombi hilo na kumruhusu Mramba kwenda bungeni kuendelea na shughuli nyingine za ubunge, lakini akaagiza awepo mahakamani Machi 3 mwaka huu kesi yao itakapotajwa.


Washitakiwa hao wanadaiwa kutumia madaraka yao vibaya na kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya Sh 11 bilioni.


Wanadaiwa wakiwa waajiriwa wa serikali walitumia madaraka yao vibaya na kutoa msamaha wa kodi kwa kampuni ya M/S Alex Stewart ya nchini Uingereza kinyume na ushauri uliotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


Souce: Gazeti la Mwananchi

CCM vs UKAWA
 
Mramba aandaliwa mapokezi mazito
• Mahakama yamruhusu kutembelea jimbo

na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imetoa ruhusa kwa Mbunge wa Rombo, anayekabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kulisababishia taifa hasara ya mabilioni ya fedha, Basil Mramba, kutoka nje ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa siku 29 kwenda kuwasalimia wananchi jimboni mwake.

Kutokana na ruhusa hiyo, Mramba sasa anatarajia kwenda jimboni kwake kesho ambako inaelezwa kwamba ameandaliwa mapokezi makubwa kutoka kwa wapiga kura wake kwa lengo la kumpa pole kwa matatizo yaliyomfika.

Diwani wa Kata ya Kelamfua Makola, Kata ya Mkuu Rombo, Festo Kilewe, aliiambia Tanzania Daima kuwa Mramba aliyekuwa rumande kwa kesi hiyo na baadaye kuachiwa kwa dhamana, ameandaliwa mapokezi makubwa na atafanya ziara katika kata za jimbo lake kuhamasisha shughuli za maendeleo.

Mipango hiyo imethibitishwa pia na msaidizi wa mbunge huyo, Roman Kilega, ambaye alisema Mramba atakuwa na ziara ya siku nne, ambapo ataanzia Kata ya Tarakea na Useri kuhamasisha ujenzi wa madarasa ya shule pamoja na kuangalia maendeleo ya ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Tarakea hadi Mkuu Rombo na kutoka Mkuu Rombo hadi Marangu.

“Kwa vile mahakama imetoa ruhusu hiyo leo (jana), tunatarajia atawasili hapa kati ya Ijumaa na Jumamosi na wapiga kura wake wamejiandaa kumpokea kwa kishindo ili kumpa pole,” alisema Kilega.

Uamuzi wa kumruhusu Mramba kwenda jimboni mwake, ulitolewa jana na mahakama hiyo kutokana na ombi la Mramba lenye kumbukumbu namba 10RCA/A1/64/2009, lililowasilishwa Ijumaa iliyopita na wakili wake, Hubert Nyange na Peter Swai, kutaka aruhusiwe kwenda jimboni kuwasalimia wapiga kura wake.

Akitoa uamuzi huo jana, Mwankenja alisema, amezingatia ibara ya 13(6)(B), inayotamka kwamba mtu asichukuliwe kuwa ana hatia hadi mahakama itakapomkuta na hatia na ibara ya 17 ya katiba ya nchi, inayosema kila mtu ana haki ya kutembea.

“Kwa kuzingatia ibara hizo za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, mahakama inakubaliana na ombi la Mramba kwa sababu bado hajakutwa na hatia, pia ana haki ya kutembea ili mradi asivunje sheria za nchi, na kwa sababu hiyo kuanzia sasa mshitakiwa anaruhusiwa kutoka nje ya mkoa huu.

“Pia niliipitia kwa kina sheria ya Bunge la Tanzania kabla ya kutoa uamuzi huu, kuona mbunge anayeshitakiwa mahakamani kwa kesi za jinai, anatakiwa atendeweje, nimebaini sheria hiyo haisemi chochote katika hilo, hivyo nimetoa uamuzi wangu kwa kutumia ibara hizo nilizozitaja ambazo zipo kwenye katiba ya nchi,” alisema Mwankenja.

Ijumaa iliyopita Mramba kupitia mawakili wake aliwasilisha ombi mahakamani hapo akitaka aruhusiwe kutoka nje ya Dar es Salaam kuanzia Januari 3 hadi Februari mosi mwaka huu.

Ruhusa hiyo itamwezesha pia mbunge huyo kuhudhuria mkutano wa Bunge unaotarajia kuanza Januari 27, lakini pia huenda akalazimika kuomba muda mwingine kwani kwa ruhusa ya sasa, ana uwezo wa kuhudhuria vikao vya Bunge kwa siku sita kabla ya muda aliopewa wa Februari mosi kumalizika.

Mramba ni mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya jinai namba 1200 ya mwaka jana, ambapo anashitakiwa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja.

Mramba aliyekuwa Waziri wa Fedha wakati wa utawala wa Awamu ya Nne pamoja na Yona na Mgonja, wanakabiliwa na mashitaka ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma.

Ilidaiwa kuwa kwa makusudi au kwa kushindwa kuchukua tahadhari kwa mujibu wa taratibu za kazi, akiwa Katibu Mkuu Hazina na wakiwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu waliruhusu kutolewa kibali cha serikali kilichoisaidia Kampuni ya M/S Alex Stewart (Assayers) Government Bussiness Corporation kutolipa kodi, tofauti na mapendekezo ya Mamlaka ya Mapato (TRA), uamuzi ambao uliisababishia serikali hasara ya sh 11,752,350,148.00.

Wakati huo huo, Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Addy Lyamuya, amesema Januari 16 mwaka huu, atatoa uamuzi wa kukubali au kutokubali mtuhumiwa wa 21 wa wizi wa Fedha katika Akauti ya Madeni ya Nje (EPA), katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Jonathan Munisi, aunganishwe kwenye kesi inayomkabili ya mfanyabiashara Japhet Lema.

Lyamuya aliyasema hayo jana baada ya kusikiliza hoja za upande wa wakili wa serikali Fredrick Manyanda na wakili wa utetezi Evarist Mbuya ambapo upande wa utetezi uliomba mteja wao, aunganishwe kwenye kesi inayomkabili Lema kwa sababu mashitaka yake, yanafanana na yanayomkabili mteja wao.

mfungwa na raia
 

Attachments

  • 1436272749108.jpg
    1436272749108.jpg
    26.3 KB · Views: 299
  • 1436272772939.jpg
    1436272772939.jpg
    29.7 KB · Views: 287
Kwa wizi na ujambazi wa hawa wakina Mramba, kama angekuwa baba ningemsusia na si ajabu ningemzomea.
Baba mwizi au mama mwizi sina undugu wala urafiki naye.
Tena sikiliza wewe Kandambili, mwizi ni mwizi tu hata akiwa na kesi ambayo haijaamuliwa bado ni mwizi. Na hata wakimu aquit mahakamani bado haitaondoa wizi wake. Kama aliiba atabaki ni mwizi tuuuuuuuuuuuu.
Ebu soma hiyo signature yangu ndugu.
safi sana ! umeandika kikakamavu sana !
 
Back
Top Bottom