Mradi wa Viwanja vipya - Kinyerezi

kweli ngumu, nimeongea na mtu mmoja pale manispaa ya Ilala ananiambia hata yeye kama mtumishi ameshindwa na gharama na masharti. sqm moja 10,000 halafu ndani ya siku 14 uwe umeshalipia hela zote za kiwanja. Na hii hali wanadhani kila mtu kajilimbikizia kama wao!!! nadhani itakuwa kama ile ya Arusha tu, mtu 1 anajitwalia viwanja kadhaa, kweli mwenye nazo huongezewa. kama unajua ndani ya siku 14 huwezi maliza lipia kiwanja hela yote dnt waste your time and money (20,000 ya form = lunch 20 mtaani kwetu)
 
  • Thanks
Reactions: Aza
nenda pale mbezi unanunua viwanja vinne kwa iyo bei na unapata na hela ya kuanza ujenzi kila kiwanja cha 30x 30 ni millioni mbili umeme upo kasoro maji


mbezi gani na tumwone nani address please.
ivi vya kinyerezi izo forms zitapatikana wapi hasa?
 
Tarehe 16/05/2011 nilisoma Tangazo kwamba serikali imepima viwanja Kinyerezi inaviuza kwa bei ya mita moja ya mraba shiringi 10,000, 15,000, 20,000, 5,000 na 8,000 kwa Viwanja vya makazi, makazi na biashara, huduma za jamii na ibada respectively, bei ambazo Watanzania wachache (hasa humu JF)wenye uelewa walilalamikia, mimi nikiwa mmoja wao, Pamoja na hayo jana nikaamua kwenda kujipinda kulipia form, leo nimeenda mahala husika(viwanja vya anautogro) na pay in slip ili kuchukua form za maombi, sijaamini nilichokiona kwasababu nimekuta kuna foleni ya watu wasiopungua miatano(500) na baadhi yao wana form zaidi ya moja mkononi na mbaya zaidi watu wanazidi kumiminika kulipia forms. Binafsi nilijua tutakuwa wachache sana tulioamua kujilipua kwa hizo bei, ndipo nikajua kumbe Watanzania wana pesa nyingi sana haiwezekani bei kubwa namna ile kukawa kuna ushindani mkubwa kiasi hicho. baada ya kudodosa dodosa nikaambiwa viwanja tunavyogombea vipo jumla 150 tu ambavyo kimsingi watapata watu 150 tu. Kwasababu mimi naamini haki itatendeka hivyo mtu wa kwanza kuviomba mpaka wa miamoja hamsini(150) ndiyo watakaopata, sisi wengine imekula kwetu sikutaka niendelee kupoteza mda wangu nikaamua kujiondokea na kuiachia serikali 20,000 ya form.

Nikiwa naondoka nilijaribu kuingizia habari za bei za viwanja kwa watu niliokuwa karibu nao wengi walionyesha hawajui bei yake na mbaya zaidi hawajui hata unaposema Mita moja ya mraba unamaanisha nini, na chakustaajabisha zaidi wengi wa watu wa namna hiyo wamelipia form za maombi ya viwanja zaidi ya kimoja.

Mtu mwingine nilipo muuliza alinijibu kwamba yeye anataka kiwanja kimoja tu cha mita 40 kwa 30 ili jumla iwe mita 70 maana ana 700,000 kwenye akaunti yake ambayo alikuwa anatafuta sana eneo la kujenga kibanda cha kujihifadhi.

Kutokana na niliyoyaona leo serikali inatakiwa inapotoa tangazo itoe kwa makusudi elimu ya ziada kwa umma maana siyo wote wanaelewa nini maana ya mita moja ya mraba, wangetoa mfano kwa kiswahili kwamba kiwanja cha 40 kwa 30 ni Milioni12 kusingekuwa na msongamano wa watu wengi kiasi kile, vinginevyo itaishia kuzikusanya elfu ishiriniishirini za Watanzania wengi ambao wana elimu duni.


daaah kweli bongo vituko! wapo wengi sana wa namna hii.
 
aisee kwa habari za chini ya carpet ni kuwa vwanja vilishaanza kuuzwa na mkurugenzi wa manispaa,unaongea nae vizuri unapata plot..sasa sisi walalahoi itakuwaje jamani..
 
kwa walio chukua form nadhani watakaa pending kwani manispaa iliandaa mpango wa kuwadhulum wananchi waliokuwa wanamiliki maeneo hayo. Fidia haijafanywa na wao wanatangaza kuuza viwanja na cha ajabu eti na mmiliki ambaye alikuwa anasubiri fidia anaambiwa eti na yeye achukue form. kwa waandishi wa habari saa7 mchana kuna kikao cha wananchi wakiwa na diwani wao kuhusu sakata hilo. wamiliki hawakubali kudhulumika kienyeji. Nadhani ni wiki imepita chanel ten walipoibua sakata la waathilika wa gongolamboto siku moja baadae kaimu mkuu wa mkoa aliongea kuwa waathilika wa gongolamboto nyumba zao watajengewa kinyerezi na akaongea kuwa tatizo ni kwamba viwanja vya kinyerezi vinahitaji kufidiwa kwanza kisha ndo process zingine ziendelee, sasa jiulize ndani ya wiki moja baada ya kaimu mkuu wa mkoa kuongea wamesha fidia wananchi wa pale waliokuwa wanamiliki yale maeneo? saa 7 leo maeneo ya Kifulu patakuwa hapatoshi, wananchi wamekasirika sana sana na mpango huo wa manispaa kutaka kudhurumu haki za wanyonge
 
mimi nina kiwanja pale kinyerezi mwisho wa lami nilipigwa stop kuendelea na ujenzi eti mpaka kipimwe lakini naona jirani zangu wanaendelea na ujenzi
 
Kama sio julius kambarage nyerere sisi wakinayahe hata hapo mbagara tusingejenga........... Hiii sasa tunatakiwa kwa umoja wetu kukataa hali hii kwa pamoja. Nchi ikiisha kuwa corrupt masikini haba chake.....j k nyerere
 
mimi nina kiwanja pale kinyerezi mwisho wa lami nilipigwa stop kuendelea na ujenzi eti mpaka kipimwe lakini naona jirani zangu wanaendelea na ujenzi

kaka siyo wewe tu wapo wengi walikuwa wamesha anza ujenzi walipigwa stop toka walipopima. wananchi wamekaa na makaratasi ya fidia yanayoonesha mazao yaliyokuwepo katika maeneo yao,eti leo mtu anaibuka na kuanza kuuza else if hapakuwa na mmliki.
 
kaka siyo wewe tu wapo wengi walikuwa wamesha anza ujenzi walipigwa stop toka walipopima. wananchi wamekaa na makaratasi ya fidia yanayoonesha mazao yaliyokuwepo katika maeneo yao,eti leo mtu anaibuka na kuanza kuuza else if hapakuwa na mmliki.

hata mimi nina makaratasi eti yanaonyesha nina miti kiasi gani kwenye uwanja wangu,hii srikali ovyo sana bwana,badala ya kusaidia wananchi ili wajenge inakuwa kama wanazuia maendeleo yetu,mungu angewaua wote ningefurahi sana
 
kaka siyo wewe tu wapo wengi walikuwa wamesha anza ujenzi walipigwa stop toka walipopima. wananchi wamekaa na makaratasi ya fidia yanayoonesha mazao yaliyokuwepo katika maeneo yao,eti leo mtu anaibuka na kuanza kuuza else if hapakuwa na mmliki.

mkuu naomba sana niwekee no yako kuna kitu nataka kukuuliza manake mimi nipo mbali
 
Tanzania imekuwa nchi ya JUNGLE LAW! ngoja niende pale bustani ya mnazi mmoja nikachimbe Msingi KHAAAAAAA!!!
 
sasa izo form apo ofisi yao,yani uswahili mtupu
wanaboa kishenzi
 
wakuu naombeni kama kuna mtu anatoka tabata kinyerezi anisaidie kwenye hili,mwaka juzi walitusimamisha kuendelea na ujenzi wakidai viwanja vipimwe kwanza,naomba nielewe kwa kuwa ni muda mrefu sijui nini kinaendelea
 
Wakuu nina kiwanja pale kinyerezi karibu na mwisho wa lami. Naombeni mnipe taarifa lakini walitupiga picha na kuchukua taarifa zetu.

Nini hatma yetu kwenye viwanja vyetu?
 
Na viwanja vya Kisarawe navyo ni utapeli tu au? Kuna jamaa alishaniambia kuwa viwanja vinapatikana kwa not more than 1,500,000 (bei ya Serikali) kwa MEDIUM DENSITY. Je ni kweli?
 
Kaka mimi nimesoma gazeti la Mtanzania jana sikuamini. Nikapiga simu mahala nikaambiwa habari ndiyo hiyo. Yaani ukitaka kiwanja cha 25mx22m = 550m2 (high density) unatakiwa utoe Tshs. 5,500,000.00 tena within 2 weeks. Jamani nani anaweza kupata hizo pesa na kulipa. Mfanyakazi gani atapata kiwanja cha bei hizi? Serikali naona sasa inachezea maisha ya watu. Kama hali ni hiyo kwa nini watu wasijenge mabondeni na kwenye hifadhi za barabara?


Wanasema unatakiwa urudishe gharama za miundombinu wakati hakuna miundombinu ni vichaka vitupu kule kinyerezi - Kifuru. Jamani jamani serikali hii naona imetuchoka sasa.

Ndio Tanzania yetu yenye AMANI!???,tuendelee kujivunia amani na utulivu wetu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom