sijui kama naikumbuka vizur watoto walichukuliwa wakaenda mlima ......aaarrgghh nimesahau tena
Ni simulizi ya mwaka 1300 kwenye mji wa Hamelin huko Ujerumani
Huo mji ulikuwa ni sugu kwa ugonjwa wa tauni unaosababishwa na panya ambao walikuwa wengi kupitiliza kwenye huo mji...wakazi wa hamelin walishajaribu kila namna kuwadhibiti wale panya lakini ilishindikana kabisa
Siku moja alikuja mgeni mwenye mavazi makuukuu akiwa kabeba filimbi na kuwaambia wenyeji wa hamelin kuwa angeweza kuwaondolea baa lile la panya
Kwa muonekano wake wa kifukara hawakuamini kuwa angeweza kufanya hiyo kazi hivyo wakampa sharti la kumlipa baada ya kazi kukamilika
Jamaa hakubisha akaanza kazi mara moja kwa kupuliza filimbi yake ambapo mapanya yote yalitoka kwenye kila tundu kila ficho na kila nyumba na kumfuata
Aliendelea kupuliza filimbi yake huku akielekea upande wa mji kulikokuwa na mto mkubwa huku maelfu ya panya yakimfuata nyuma . ...kufika pale mtoni alisimama na kila panya aliyefika pale alirukia majini na kupotea...baada ya panya wote kupotelea majini alirudi mjini kudai ujira wake
Watu wa hamelin kwa ujuha wao wakamzingua na kugoma kumlipa ujira wa kazi yake, Jamaa akaondoka na kinyongo chake
Siku tatu baadae Jamaa alirejea Hamelin nyakati za jioni hivi na kuanza kupiga filimbi yake huku akielekea upande mwingine wa mji kulikokuwa na mlima mrefu...filimbi ya kipindi hiki haikutoa panya bali watoto wote wa mji wa hamelin
Wazazi walijaribu kuwakataza watoto wao wasimfuate bwana yule lakini haikuwezekana...alipofika pale mlimani, mlima ulifunguka naye akazama na kupotelea huko na wale watoto wote
Aliyesalimika ni mtoto mmoja mlemavu wa miguu ambaye aliachwa nyuma na mpaka anafika pale mlima ulikuwa umeshajifunga
Huyu ndie aliyerudi mjini na kusimulia kilichotokea (left to tell)