kamati yamaamuzi magumuu
JF-Expert Member
- Nov 14, 2019
- 227
- 262
umegusa mzizi mkubwa saana wa ndoa tulizonazo kwasasa nanyingi zinasua sua saana!! Vijana tujichekeche saana , Ndoa zinakuwa ngumu kutokana na sababu kuu Kama hizi zilizopelekea kufunga Ndoa!!!!Hata walio oa/kuolewa hawana majibu ya kuridhisha kwanini wameoa
1. Wapo waliooa kwasababu ya shinikizo la wazazi, wapo wazazi wamekua wakiwalalamikia watoto zao kuwa umri unaenda wanataka wajukuu
2. Lipo kundi ambalo wameoa/kuolewa kwasababu wamekua wakiona watu wa rika zao wote wameoa hivyo wana inferior kuwa jamii inawaona kwa jicho baya
3. Wapo walio oa kwasababu ya mkumbo wamekuta jamii ikiishi katika utamaduni huo kua umri fulani ni lazima mtu awe ameoa/kuolewa
4. Na saizi wapo wanao oa kwasababu kesho ni mfungo, kundi hili la watu wamejiwekea udhaifu kwamba ni ngumu kuishi katika hicho kipindi bila kufanya ngono, na kufanya ngono ya bila ndoa katika kipindi hicho ni dhambi hivyo inamlazimu aoe ili kuhalalisha ngono
5. Wapo walio oa kwasababu ya uvivu wa kazi ndogo ndogo za nyumbani, hili ni kundi lenye watu wengi sana mpaka sasa. Hii inamaana kwamba watu hawa hawakuingia kwa nia madhubuti ya kifamilia/kindoa changamoto za kufua, kuisha vyombo, usafi kiujumla zimepelekea kufunga ndoa. Hapo utaona nafasi ya mke ni kama beki tatu
6. Lipo kundi la watu walioingia kwenye ndoa kutokana na "HOFU". Hili ni kundi ambalo ukiwauliza kwanini umeoa watakuambia "maisha bila mke ni risk sana kwasababu unaweza ukaumwa usiku ukakosa nguvu hata kushika simu ukashindwa hivyo bila mke waweza kufa"
7. Hawa ni wale walio oa baada ya kukutwa na hatia ya kuzini eidha alimpa mimba mwanamke kwa bahati mbaya hivyo ikamlazimu amuoe. Wapo pia wanawake watukutu waliogomea kwenye mageto ya masela kwa kuforce kuolewa
Siku ambayo watu watajua sababu ya msingi kwanini wanaoa kuna uwezekano tukadhibiti kwa kiasi fulani hii migogoro ya ndoa na idadi ya talaka
#Umetoa points hizi kama ulikua kwenye brain yangu