Zomba, siamini kama umetumwa. Inawezekana umejituma mwenyewe. Hilo tuliache.
Turudi kwenye huo mpasuko. Nadhani twende kwa mifano hai;
1) Kususia Hotuba ya Rais
Hili limetuonyeshaa ni jinsi gani Chadema inavyoendeshwa bila muelekeo, wakati wabunge wao wengi wa-kisusia hotuba ya Rais wengine wengi walisusia shinikizo la Mwenyekiti wao na kuamuwa kuto ingia kabisa bungeni siku hiyo. Na wengine tukawaona, usiku huo kwenye hafla ya Rais ilhali viongozi wa Chadema walishinikiza wabunge wa Chadema wote wasiende huko.
Hapa hoja yako ni kwamba kitendo cha baadhi ya wabunge kutofautiana kimawazo kuhusu kuingia au kutokuingia bungeni ni mpasuko. Kitendo cha Shibuda kwenda kwenye hafla ya Raisi ni mpasuko. Nikitaka kukubaliana na hoja yako najiuliza, je huo ni mpasuko au dalili ya mpasuko? Hivyo ni vitu viwili tofauti. Lakini, najiuliza tena, kuna athari gani viongozi wa chama cha siasa kupingana kimawazo? Ninavyoamini mimi ni kwamba kupingana mawazo ni faida endapo mwisho wa siku muafaka utafikiwa kama ilivyotokea kwa CHADEMA. Suala la kutokuhudhuria bungeni lilijadiliwa na Kamati Kuu na uamuzi kutolewa wa nini kifanyike. Huo ni ukomavu wa kisiasa.
2) Kugombea vyeo na nafasi za upendeleo.
Tumeona sakata la nafasi za upendeleo haswa za ubunge jinsi zilivyoleta mvutano ndani ya Chadema na kufikia wana Chademaa wengine kuwachia ngazi, hii ni dalili tosha kuwa utawala wa ndani wa Chadema una mapungufu makubwa.
Hapa umepotea. Je kuna ubaya gani mtu 'kupendelewa' kutokana na uwezo, elimu na utendaji wake? hakuna dhambi kumpendelea mtu kwa vigezo hivyo ambavyo ndivyo vilivyotumika kupata wabunge wa viti maalum. Ni tofauti pale mtu anapopendelewa kwa sababu ya mzazi wake, fedha zake na mchango wake katika kuliibia taifa. sihitaji kukueleza zaidi. Kuna watu ambao kwa kiasi kikubwa waliamini kwamba CHADEMA itayumba kwa sababu ya Viti Maalumu. Lakini leo hii hali ni tofauti sana!! Angalia kabla ya wao kujitoa na sasa ili uone CHADEMA iko wapi.
Kwa kiongozi kujitoa kwenye chama kisa nafasi ya ubunge ni ishara wazi kwamba mtu huyo ana walakini. Kitendo cha mtu kutaka apewe nafasi kwa sababu tu amekaa muda mrefu kwenye chama hakikubaliki ndani ya CHADEMA. Kuondoka kwa watu wa aina hiyo ni faida kwa chama.
Tukaona pia jinsi Zitto alivyopigwa chini na Mwenyekiti wake katika kuwania nafasi ya uongozi wa upinzani bungeni. Hali kadhalika tukaona Zitto alivyosulubiwa mpaka kulazwa hiospitali na kupigwa marufuku na uongozo wa Chadema kuwa asiongee na vyombo vya habari kuhusu Chadema kwani yeye si msemaji wa Chadema.
Utaratibu uliotumika kuhusu KUB ni utaratibu unaoleweka kwa urahisi sana. Sihitaji kukufundisha kutokana na umri wako ambao umeulinganisha na Prof. Shivji. Nitakuheshimu hivyo nitaliachia hapo. Ni kweli Zitto si msemaji wa chama. Ungependa CHADEMA kila mtu aseme analojisikia kusema kama ilivyo kwa Mwakyembe, Sitta, Vuai, Makamba, Chitanda, Wassira, JK, Membe n.k kuhusu kilichotokea Arusha??? Hayo ndiyo yanayokufurahisha? Je hu ni mpasuko ndani ya CCM na Serikali??
3) Sakata la Arusha:
Tumeona jinsi wengi wa viongozi wa Chadema kutokuhudhuria kwenye maadamano yaliyoshinikizwa na kushadidiwa na viongozi wachache wa Chadema. Na pia tukaona mvutano mkubwa ukitokea katika kutumia maiti kama njia ya kujipatia umaarufu Chadema, ni viongozi wachache wa Chadema walihudhuria "kuaga miili ya marehemu" hao.
Kwa mara nyingine umepotea ila safari hii umenipoteza na mimi. Viongozi wachache ni wangapi? kwenye maandamano hayo walikuwepo wafuatao Mwenyekiti wa taifa, Katibu Mkuu, Mwenyekiti wa Mkoa, Katibu wa Mkoa, Mwenyekiti wa Wilaya, Katibu wa Wilaya. Wenyeviti wa Kata, Wabunge na Madiwani. Hao ni wachache???
Umaarufu?? Umati uliohudhuria mkutano siku hiyo ulienda kuona maiti?? Kulikuwa na maiti uwanjani siku ya tarehe 5?? Ni umaarufu upi CHADEMA imeupata? CHADEMA ni watu, sio chombo. Kuna watu wanashindwa kuliona hilo ndio maana anguko lao liko karibu sana. Unapolaani CHADEMA unalaani watanzania zaidi ya milioni 5 ambao ni wafuasi wa CHADEMA!
Tukaona kuwa hata Fundikira ambae ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Chadema mkoani Arusha kukataa kuhudhuria muago huo, akisingizia kuwa alikuwa na wageni nyumbani kwake. Wageni zaidi ya Mwenyekiti wake wa Taifaa na Katibu Mkuu wake na Kuaga "wahanga"? hilo ni la kujiuliza.
Fundikira alihudhuria vikao vyote. Yeye ndiye aliyempigia Sheikh Mkuu wa Bakwata na viongozi wengine na kuwaambia wasiilazimishe familia ya marehemu kuacha kuaga mwili. mwenyekiti wa taifa alimshirikisha Mzee Fundikira wakati wote kwa kuona umuhimu wake kama Muislamu na kiongozi. Humjui Mzee Fundikira hivyo usipotoshe ukweli. Kusema ukweli ni sababu ya kuheshimika zaidi.
Ukitazama kwa juu juu utaona hayo si kama mambo ya kawaida, na ukiingia ndani kidooogo, utaona kuwa huo ni mpasuko na mtafuruku mkubwa ndani ya Chadema.
Hakuna mpasuko CHADEMA. Tofauti za mawazo au maoni tofauti sio mpasuko. Kwa Chama makini hu o ni mwanzo pia kipimo cha ukomavu. CHADEMA wanathibitisha hilo kila kukicha. Hauwezi kujiandaa kuongoza nchi kama haupitii katika hali hiyo ya utofauti wa mawazo.
"A smooth sea doesnt make a good swimmer"
:Cry: