Mpango wa waziri Makamba wa kupunguza bei ya petroli kwa 75% na Tanzania kuwa petrol hub umeishia wapi?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Ni zaidi ya mwaka mmoja sasa tangia waziri wa nishati, Mh. January Makamba, atangaze mpango wa serikali utakaoiwezesha nchi yetu kuwa petrol hub itakayokuwa inasambaza mafuta haya kwa nchi nyingi za SADEC na Afrika Mashariki.

Mpango ulikuwa kwa kushirikiana na nchi rafiki za OPEC+ kujengwa kwa kituo kikubwa kabisa jijini Dar es Salaam cha kupokea na kuhifadhi mafuta haya (yaani petrol hub) kwa soko la ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Katikq mpango huo serikali ya Tanzania ingalikuwa inayanunua mafuta hayo moja kwa moja mafuta hayo kutoka nchi hizo rafiki za OPEC+ kwa bei ya asilimia 25% tu ya bei inayoyanunua kwa sasa kutoka kwa watu wa katikati. Serikali ilitembelea hizo nchi rafiki za OPEC+ na kukubaliana na mpango huu. Mwezi Septemba 2021 majaribio ya ununuzi yalifanyika ambapo serikali iliweza kununua mafuta hayo kwa USD 20 kwa pipa badala ya USD 86 kwa pipa iliyokuwa inayanunua kupitia watu wa katikakati.

Ni zaidi ya mwaka mmoja sasa umepita tangia mpango huo ukubaliwe kati ya serikali yetu na hizo nchi rafiki lakini wizara ya nishati imekuwa kimya kueleza maendeleo wa huo mpango. Jee umetupwa kapuni?

 
Mbona umeme ameweza, haukatiki tena tangia Christmas na bwawa la Nyerere kalijaza maji. Hata hili atakuja kutufanyia suprise ya performance yake nzuri.
Umeme haujawah kuwa na shida tangu kipind cha jiwe , watu wote waliona lilikuwa ni tatizo la kutengenezwa , hapa juzi makelele yamekuwa mengi mpk bungeni mpak wafanyabiashara wakubwa tuu wanaanza kumnanga , ikabd aachie , Bwawa la Nyerere hakuwa na Nia nalo , ni watu wa karbu na Raisi tuu walimwambia Raisi itakuwa ni upumbavu wa kiwango cha standard gauge kutelekeza mradi mzito namna hyo , kila mmoja duniani ataona nchi inaongozwa na wehu ,alaf uje kutegemea miradi ya gas ambayo kimsingi nchi itakuwa inauziwa na kulazimika kwenda kukopa ili kulipa ....

Jamaa ana haters wengi tuu mpak huko juu , ni vile tuu wale wazee watatu ndo wanampa kiburi ,
 
Umekaa kabisa unasubiri.
Ndiyo. Wengi tunasubiri kwa hamu kubwa kuiona nchi yetu by 2025 kuwa petrol hub ya nchi za Afrika Mashariki na Kati. Wewe hupendi kuona hilo likitokea?
Umeme haujawah kuwa na shida tangu kipind cha jiwe , watu wote waliona lilikuwa ni tatizo la kutengenezwa , hapa juzi makelele yamekuwa mengi mpk bungeni mpak wafanyabiashara wakubwa tuu wanaanza kumnanga , ikabd aachie , Bwawa la Nyerere hakuwa na Nia nalo , ni watu wa karbu na Raisi tuu walimwambia Raisi itakuwa ni upumbavu wa kiwango cha standard gauge kutelekeza mradi mzito namna hyo , kila mmoja duniani ataona nchi inaongozwa na wehu ,alaf uje kutegemea miradi ya gas ambayo kimsingi nchi itakuwa inauziwa na kulazimika kwenda kukopa ili kulipa ....

Jamaa ana haters wengi tuu mpak huko juu , ni vile tuu wale wazee watatu ndo wanampa kiburi ,
Kwa hiyo na hili petrol hub anasubiri makelele yawe mengi ndiyo aachie?
 
Utakuwaje Petrol hub wakati hauna mafuta?
Mafuta yatatiririka kwa bomba au nyenzo nyingine kutoka nchi rafiki za OPEC+ hadi bandari salaama yetu kama vile ile gesi na mafuta yanavyotiririkaga kutoka Urusi hadi ulaya magharibi.
 
Unahangaika na wapigaji?

Yaani Makamba na Nape wao ni kushukulika na ma bwenyenye ili wapate hela. Hasa za Kampuni.
 
Umeme haujawah kuwa na shida tangu kipind cha jiwe , watu wote waliona lilikuwa ni tatizo la kutengenezwa , hapa juzi makelele yamekuwa mengi mpk bungeni mpak wafanyabiashara wakubwa tuu wanaanza kumnanga , ikabd aachie , Bwawa la Nyerere hakuwa na Nia nalo , ni watu wa karbu na Raisi tuu walimwambia Raisi itakuwa ni upumbavu wa kiwango cha standard gauge kutelekeza mradi mzito namna hyo , kila mmoja duniani ataona nchi inaongozwa na wehu ,alaf uje kutegemea miradi ya gas ambayo kimsingi nchi itakuwa inauziwa na kulazimika kwenda kukopa ili kulipa ....

Jamaa ana haters wengi tuu mpak huko juu , ni vile tuu wale wazee watatu ndo wanampa kiburi ,
Majenereta yanafanya kazi . Dili tayari
 
Mbona umeme ameweza, haukatiki tena tangia Christmas na bwawa la Nyerere kalijaza maji. Hata hili atakuja kutufanyia suprise ya performance yake nzuri.
Unaandika points au unaandika mahaba?
Maisja ya mahaba ni ghali sana, note hilo.
 
Ni zaidi ya mwaka mmoja sasa tangia waziri wa nishati, Mh. January Makamba, atangaze mpango wa serikali utakaoiwezesha nchi yetu kuwa petrol hub itakayokuwa inasambaza mafuta haya kwa nchi nyingi za SADEC na Afrika Mashariki.

Mpango ulikuwa kwa kushirikiana na nchi rafiki za OPEC+ kujengwa kwa kituo kikubwa kabisa jijini Dar es Salaam cha kupokea na kuhifadhi mafuta haya (yaani petrol hub) kwa soko la ukanda wa Afrika Mashariki na Kati. Katikq mpango huo serikali ya Tanzania ingalikuwa inayanunua mafuta hayo moja kwa moja mafuta hayo kutoka nchi hizo rafiki za OPEC+ kwa bei ya asilimia 25% tu ya bei inayoyanunua kwa sasa kutoka kwa watu wa katikati. Serikali ilitembelea hizo nchi rafiki za OPEC+ na kukubaliana na mpango huu. Mwezi Septemba 2021 majaribio ya ununuzi yalifanyika ambapo serikali iliweza kununua mafuta hayo kwa USD 20 kwa pipa badala ya USD 86 kwa pipa iliyokuwa inayanunua kupitia watu wa katikakati.

Ni zaidi ya mwaka mmoja sasa umepita tangia mpango huo ukubaliwe kati ya serikali yetu na hizo nchi rafiki lakini wizara ya nishati imekuwa kimya kueleza maendeleo wa huo mpango. Jee umetupwa kapuni?

Uliamini maneno ya huyu tapeli?
 
Kwa uwezo mkubwa wa akili ya January makamba inawezekana.
Huu ni mpango wa serikali, hata raisi wetu alishatembelea mara kadhaa hizo nchi rafiki za OPEC. Katika ziara hizo tunaamini mojawapo ya majadiliano na makubaliano yalihusu mpango huu wa petrol hub. Mara nyingi katika ziara hizo tulimuona waziri Makamba akiwemo. Tatizo hadi sasa Makamba amekuwa mute kuhusiana na mpango huu muhimu. Watu wa katikati wameendelea kutuuzia mafuta haya kwa bei ya mara nne ya bei ambayo tungaliweza kuyanunua moja kwa moja wenyewe kwa kutumia shirika letu la TPDC. Makamba wala hasemi tena pipa moja hao watu wa katikati wanatuuzia kwa dola ngapi? Kwa nini amekuwa hivyo?
 
Back
Top Bottom