Mpango wa Rwanda kupokea wahamiaji kutoka Marekani (kwa Trump) si tishio kwa usalama wa Afrika Mashariki?

Mpango wa Rwanda kupokea wahamiaji kutoka Marekani (kwa Trump) si tishio kwa usalama wa Afrika Mashariki?

Mende mdudu

Senior Member
Joined
Feb 13, 2023
Posts
197
Reaction score
405
Serikali ya Rwanda imetangaza kwamba iko katika mazungumzo ya awali na serikali ya Rais Donald Trump kuhusu kuwapeleka nchini Rwanda wahalifu waliokamilisha adhabu zao magerezani nchini Marekani. Kauli hii imezua maoni mseto nchini Rwanda na hata kwa africa mashariki watu wenye historia ya uhalifu.

Rwanda inafahamika ina kilometer chache za mraba, vipi kiusalama kwa nchi zenye maeneo makubwa yaliopakana na rwanda kama Congo na Tanzania?

Ni kama Kagame anajua kuchanga karata zake vizuri ?

Soma Rwanda kupokea wahamiaji haramu kutoka marekani
 
Kila nchi ilinde mipaka yake

Hata hapa Tz kuna vibaka kibao, wanateka na kunyang'anya uhai wa watu na hao vibaka hawatoki Rwanda wala nini,

Wengine wanasema, vibaka hao wanatoka ccm
 
Hakuna tatizo ila Kagame ni snitch tu, ana kiherehere sana.

Hata Wakimbizi wa Uingereza walitaka kuwadampo Rwanda huyo mpumbavu kashapewa pesa lakini serikali mpya ya Uingereza imeufuta mpango huo ni kinyume cha haki za binadamu na UNHCR.
 
Hakuna tatizo ila Kagame ni snitch tu, ana kiherehere sana.

Hata Wakimbizi wa Uingereza walitaka kuwadampo Rwanda huyo mpumbavu kashapewa pesa lakini serikali mpya ya Uingereza imeufuta mpango huo ni kinyume cha haki za binadamu na UNHCR.
Aise Sijawahi ona mpumbavu kama wewe, Rais muelevu kiasi hiki anajua kuitafutia nchi yake business sehumu mbalimbali, ila wewe sababu ya wivu basi ni kumtukana. wewe unapaswa uishi bondeni, uishi na mifugo pekee, kwa sababu upumbuvu na ujinga wako wa hari ya juu
 
Nchi ya Rwanda ni Sawa na mkoa wa tanga kilomete za mraba ,

Populations ya Rwanda ni kubwa kuliko arthi ya Rwanda mpka wanyarwanda kukosaaaa hifadhi,

Sasa hao wamilioni ya wakimbizi atawapeleka wapi unadhani
 
Kiuhalisia hapendwi mtu hapa, kwamba wahalifu ndio wameonewa huruma na kupewa hifadhi. Kuna msukumo mwingine.

... tusidanganyane🔥😌

Msukumo mkubwa hapa ni Dollar na mahusiano mazuri na Marekani-tambua pia, Mzee ni wa kupozwa😁

Tariffs 10 -10

Hatahivyo sidhani kama kutakuwa na tishio lelote lile zaidi na kwa Ukubwa na makubaliano ya DRC na Marekani kama nimeelewa sahihi

Hata na sisi Watanzania tuna makubaliano nao tarrifs 10-10
 
Back
Top Bottom