Mpangaji wangu kashindwa kunilipa kodi

Mpangaji wangu kashindwa kunilipa kodi

Hapo Inatakiwa akili pia, kwanza nikupongeze kwa moyo mzuri wa uvumilivu.
Pili hao ukisema uwafukuze haita pendeza pia wakiondoka kulipa deni dahau.
Cha kufanya nafikir kaa nao wakulipe nusu ya deni kwa mkupuo then kaeni andikishaneni awe analipa miezi 3 kabla. Huo utakua mkataba mpya.
Ila mmh najiuliza tu kweli hajawahi pitia hako ka binti au,
Any way utani tu hapo!!
 
Huyu mpangaji wangu nimemvumilia sana, ni mwaka wa pili sasa anasema mambo yake hayako vizuri, nikienda kumdai kodi yeye na mkewe wanalia sana kwamba nizidi kuwavumilia.

Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.

Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.

Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.

Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.
Kila mwezi wanaokaa unapoteza 300,000/-. Hata huyo jamaa akipata kazi kukulipa 7m+ sio rahisi. Watafutie vyumba viwili vya 30,000/- ambavyo kodi kwa mwezi itakuwa jumla 60,000/- halafu walipie miezi mitatu wakaanze upya.

Kwa kufanya hivyo wewe utaweza kuweka mpangaji mwingine atakaekupa at least kodi ya miezi 6 ambayo ni 1.8m
 
Kila mwezi wanaokaa unapoteza 300,000/-. Hata huyo jamaa akipata kazi kukulipa 7m+ sio rahisi. Watafutie vyumba viwili vya 30,000/- ambavyo kodi kwa mwezi itakuwa jumla 60,000/- halafu walipie miezi mitatu wakaanze upya.

Kwa kufanya hivyo wewe utaweza kuweka mpangaji mwingine atakaekupa at least kodi ya miezi 6 ambayo ni 1.8m
Wapi huko dsm chumba elfu 30000..?
 
Bwana FUSO wape notice ya miez mitatu wasipolipa watafukuzwa.ikibidi husisha na mwenyekiti wa mtaa husika.Mjini huruma pia ina kipimo chake.
 
Nakushauri ongea nao wote baba,mama na mtoto wao kwa upole ili wakueleze tatizo kubwa hasa linalowakabili ni lipi,ili uligawante hilo deni kwa awamu ambapo wawe wanakulipa kila mwezi na mtiliane saini hati ya makubaliano juu ya makubaliano hayo,sasa wakishindwa hili waondoe kwa kuzingatia sheria za nchi
 
Nyumba ya Laki 3 hujalipwa Kodi ya Miaka miwili???? Alafu unakuja kuuliza kama uwafukuzee mkuu itakuwa unapesaa za kutosha sanaaa endelea kuwasaidia tuu mkuu mpaka pale watakapoipata hiyo hela maana ungekuwa serious na shida na hiyo kodi mwaka mmoja ulitoshaa sanaaa kuwatimuaa wakaishi maisha ya standard yaoo...!!
hawatoweza kujakulipa kwamwe, mana deni lina accumulate
 
kaka pango ni Sh 300,000 kwa mwezi, kwa mwaka ni Tsh 3,600,000 kwa miaka miwili ni 7.2m. ni hela nyingi sana wakuu.
Miaka miwili Ni mingi Sana, Walifaa wawe wamejipanga hata Kama Ni kutafuta Nyumba watakayoimudu.
Umeonesha ubinadamu wa kutosha kuvumilia huo muda wote hata Mungu anaona.
Kama Maisha yakiwashinda warudi kijijini, ukiendelea kujifanya mother Theresa Wewe ndo utaumia sababu hiyo Nyumba ni biashara inafaa ikulipe.
Waambie wajipange unataka Nyumba yako.
 
M
Huyu mpangaji wangu nimemvumilia sana, ni mwaka wa pili sasa anasema mambo yake hayako vizuri, nikienda kumdai kodi yeye na mkewe wanalia sana kwamba nizidi kuwavumilia.

Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.

Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.

Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.

Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.
waandikie notice
 
Miaka miwili Ni mingi Sana, Walifaa wawe wamejipanga hata Kama Ni kutafuta Nyumba watakayoimudu.
Umeonesha ubinadamu wa kutosha kuvumilia huo muda wote hata Mungu anaona.
Kama Maisha yakiwashinda warudi kijijini, ukiendelea kujifanya mother Theresa Wewe ndo utaumia sababu hiyo Nyumba ni biashara inafaa ikulipe.
Waambie wajipange unataka Nyumba yako.
ni kweli kabisa, kwa hili lazima waniewe tu - masuala ya mjini kila mtu alifika na sanduku lake !! Sema kuna wakati imani inanijaa moyoni hasa nikiwacheki watoto wao.

Lakini safari hii wanaondoka tu - shaamua.
 
FUSO kwa heshima kubwa nakuomba uwe na roho ya kibinadamu, wavumilie ila wapige mkwara kuwa wasipitishe mwaka huu bila kulipa kodi. Na kubali wawe wanalipa hata mwezi mmoja mmoja. Asante
 
FUSO kwa heshima kubwa nakuomba uwe na roho ya kibinadamu, wavumilie ila wapige mkwara kuwa wasipitishe mwaka huu bila kulipa kodi. Na kubali wawe wanalipa hata mwezi mmoja mmoja. Asante
kaka nishapiga mikwara saana, cha msingi tupishane na wakishindwa kitakachofuata ni kupiga vitu mnada - Notice tayari nishawapa inaisha 30th Nov Siku ya timbwili.. Maana ni kwenda mahakanani kuikazia notice na kuomba tupige mnada vitu kufidia kodi.

Ushauri tu kwa wasomaji wangu - Maisha yakibadilika na wewe badilika; ishi kutokana na kipato chako cha wakati huo.. kutoka kwenye nyumba ya vyumba vitatu Sinza na kwenda Magomeni chumba kimoja watoto kulala sebureni si dhambi.

Sasa jamaa wengi wanataka ku-maintain status wakati mambo yameshavurugika..sasa haya ndiyo matatizo yake.
 
Huyu mpangaji wangu nimemvumilia sana, ni mwaka wa pili sasa anasema mambo yake hayako vizuri, nikienda kumdai kodi yeye na mkewe wanalia sana kwamba nizidi kuwavumilia.

Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.

Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.

Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.

Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.
Mkuu usifanye hivyo tafadhali wacha mwaka huu uishe. Kisha amua jambo tena kiungwana.
 
kaka pango ni Sh 300,000 kwa mwezi, kwa mwaka ni Tsh 3,600,000 kwa miaka miwili ni 7.2m. ni hela nyingi sana wakuu.
Mkuu tukijitolea kuwachangia kiasi kwa niaba yao,itafaa?
 
Mkuu tukijitolea kuwachangia kiasi kwa niaba yao,itafaa?
Kaka hakuna haja, hujawaleta town na wala hawakukushirikisha wakati wanaongeza famiia....cha msingi walipe tu na kama hawawezi basi wachomoke fasta kabla ya 30th Nov, bado siku 15 tu toka leo..siku za kuwa mstraabu zishaisha.
 
Huyu mpangaji wangu nimemvumilia sana, ni mwaka wa pili sasa anasema mambo yake hayako vizuri, nikienda kumdai kodi yeye na mkewe wanalia sana kwamba nizidi kuwavumilia.

Kuna binti yao yupo form four huyo naye anajiunga nao kunililia anasema baba tusaidie tu babaa tutakulipa huku kanipigia magoti kushika viatu vyangu na suruali.

Imefikia hatua mke wa jamaa ananiandikia sms kuniomba niendelee niwavumilia, hata binti naye anaandikia sms kunipa shikamoo na kuniambia baba naomba tuvumilie tu maana baba yangu hana hela kabisa hata mimi nasoma kwa shida sana babangu.

Anapofanyia kazi huyo jamaa napajua na anapofanyia kazi huyo mkewe napajua ila siwezi kuwaambia sababu ya kulinda maudhui ya hapa JF.

Nipeni ushauri ila mimi naona ni kuwatimua tu tarehe 30th November hii, kifupi kila mtu atabeba sanduku lake mwenyewe na hapa mjini kila mtu kaja kivyake.
. Mkuu endelea kuwahurumia tu ipo siku wata kulipa fadhila zako usijali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom