Mpangaji wangu kashindwa kunilipa kodi

Mpangaji wangu kashindwa kunilipa kodi

Subiri kwanza huyo binti wa form 4 amalize mitihani alafu nitakuambia cha kufanya.
Mkuu hicho ndicho kimesababisha nilete hii mada hapa, yule binti pamoja na mitihani huwa anani sms kuniomba nisiwatimue wazazi wake... huwa nampa moyo kwamba binti endelea na mitihani yako tu usijali siwezi kufanya hivyo - yaani haya maisha jamani laaah
 
kaka pango ni Sh 300,000 kwa mwezi, kwa mwaka ni Tsh 3,600,000 kwa miaka miwili ni 7.2m. ni hela nyingi sana wakuu.
kweli ni hela nyingi ila kama ni watu wazuri wanaweza kukulipa hata nusu ya 7.2m, ongea nao tu ikishindikana basi waondoke, Una moyo wa kipekee mkuu my landlord akizidisha muda ni miezi 3 tu. for real they're very lucky to got a house like your’s and got a landlord like you, I wish I'll be your tenant.
 
Mtu kukosa ni ujinga?
Umeninukuu vibaya ujinga ninaomaanisha unapewa nafasi lakin huitumii unaambiwa soma utaki unaambiwa fanya kazi kwa bidii ufanyi onaona maisha yamebadilika kwann usiame ukatafuta sehemu au nyumba ya bei rahisi
 
Unasema ajanichapa hivi unanijua kweli. ha Ha Ha Ha Ha . Utaniambia kipi katika maisha ya raha na shida hasa hapa bongo na hata nje ya mipaka ya bongo
na bado una ujasiri wa kuandika hivyo.
 
Kama una vacancy muajiri huyo mama/baba au hata huyo binti anaemaliza mitihani wiki hii
 
Maisha Haya?? Duuh hatar tupu
Kaka kwenye majumba yetu humo kuna siri nzito sana...najua watakuwa wanasoma uzi wangu ila kwa kuwa sijawataja na sehemu wanafanyia kazi fresh tu - watakavyofikiria mi sijali.
 
Kimbiza kila mtu ana hali ngumu kama ungekuwa ww wasingekuacha na kama mm zamani nimeshakimbiza mm ukipitiliza mwezi mmoja bila taharifa ujiandae
Kipindi hiki ukifukuza jiandae kufugia kuku chumba.Mkuu siku hizi kupata mpangaji ni ngumu kuliko kudai kodi kwa mpangaji aliyopo.
 
Kama una vacancy muajiri huyo mama/baba au hata huyo binti anaemaliza mitihani wiki hii
kaka wale wameajiliwa.....sasa sijui kuna nini kimetokea kwenye hii familia kwa kweli sijui kabisa....Binti anamaliza shule ndiyo nasubiri akimaliza tu niwashe moto maana huwa anani text kuniomba nisiwatimue wazazi wake na wadogo zake...yaani ni kama binti anajivika majukumu ya kifamilia akiwa bado mdogo....inatia huruma sana... ila wataondoka tu.
 
Kipindi hiki ukifukuza jiandae kufugia kuku chumba.Mkuu siku hizi kupata mpangaji ni ngumu kuliko kudai kodi kwa mpangaji aliyopo.
kaka ni nyumba ya vyumba 3, ipo vizuri sana siwezi kosa mtu wa kukaa kwa hiyo hela.
 
kaka ni nyumba ya vyumba 3, ipo vizuri sana siwezi kosa mtu wa kukaa kwa hiyo hela.
Mkuu fukuza utakuja kunipa mrejesho.Kuna muda mpaka unahisi mpangaji aliyeondoka kairoga nyumba yako.
 
Yah kwa sababu najiamini na mpaka leo na chezea keypad za simu na kuandikia na wewe mkuu usiwachukulie watu poa Poa maisha turiyopitia ndio yanatupa ujasiri
Kama yalishakukuta unasemaje amtimue mkuu.
 
Ndio maana sijakuona kijiweni kwenye moja baridi kumbe ni vile hujalipwa kodi!!
 
ngongoti2000,
Kaka ingekuwa watu wasio na hofu na Muumba, yangekuwa mengine kabisa!! Mungu aniongoze kwenye hili.
 
kaka wale wameajiliwa.....sasa sijui kuna nini kimetokea kwenye hii familia kwa kweli sijui kabisa....Binti anamaliza shule ndiyo nasubiri akimaliza tu niwashe moto maana huwa anani text kuniomba nisiwatimue wazazi wake na wadogo zake...yaani ni kama binti anajivika majukumu ya kifamilia akiwa bado mdogo....inatia huruma sana... ila wataondoka tu.
Hamna mkuu wameshampanga pia achana nae huyo binti wanaweza kukutengezea kesi kama amefanya hivyo atashindwa vipi kutengezea kesi ya mimba au kubaka au kuwagombanisha na shemeji. Mjomba mipango hiyo yote mama ake ndie anamtengeneza huyo binti
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom