Mpaka leo sijaijua thamani ya 'X'

Utoto huu .
Hakuna hesabu hata moja isokuwa na matumizi .au faida
Usinidanganye wala usijidanganye kuwa hesabu zote ulizojifunza umeshazi-apply ktk maisha.

Ninachofahamu, asilimia 90 ya ulichojifunza kilikuwa kwaajili ya kujibia mtihani, tena ujibu kulingana na marking scheme not otherwise.

Utoto uko wapi.... kuhoji relevance ya mitaala yetu au kuendelea kufurahia uozo?
 
Wewe unadai elimu haisadii ila umetolea mfano kutafuta thamani ya X ambayo ni topic moja ya hesabu basic maths ya Algebra!!!!??
Mbona hukuizungumzia elimu yoote unazungumzia topic moja ya hesabu!!

Ila Algebra mbona ina application nyingi tu mkuu labda nikupe mfano simple tu, umekopa hela benki ukafanyie biashara inayokadiriwa kukupa mapato flani kwa mwaka ni lazima ujue riba itakuwa kiasi gani, rate ya marejesho kiasi gani na uncertainty ya business yako , haya yote ni algebra itakusaidia,

pia production za simple kama kukadiria labda mahindi kiasi fulani zitazalisha mifuko mingapi ya unga, kwa kutumia unit ngapi za umeme na kwa muda gani, na faida gani, algebra pia,
kujua nitalima heka ngapi za shamba ili trekta nililokodisha lisinipe hasara utatumia algerbra pia,

kujua mtaji wangu wa kufugia kuku niutumie kiasi gani kwenye kununua vifaranga na kiasi gani kwenye kujenga banda na kuzilisha ili usijikute umeanza na kuku wengi kuliko mtaji pia utatumia algebra,
Kujua mtaji wangu wa milioni 50 nikikopesha watu kwa miaka 5 nitavuna ngapi kwa muda huo pia ni hesabu

Hii ni mifano simple nimekupa kwa mtu ambaye labda hajaajiriwa na hajui atafaidikaje na elimu yake ( tena topic ya Algebra tu) kama akijiajiri

Ila hesabu ina application nyingi ambazo ni complex na zinarahisisha mambo mengi sana kwenye hii dunia

elimu hasa Sayansi nadhani lengo lake primarily sio kumfanya mtu atajirike, bali kumuwezesha mwanadamu kuishi comfortable zaidi kwa kuya master mazingira yake na kutajirika ni matokeo yake ya pili kwa watakao tumia elimu hiyo kutoa service ambazo watu watazilipia
Well, nipo na vijana wengi sana mtaani... wana degrees za I.T, banking, law n.k lakini wameshindwa kutumia hata hiyo algebra.Kifupi maisha yamewagonga.. algebra waliyojifunza iliwaandaa kuajiriwa.. hawajaweza kumaster maisha.

Hiyo inanipa sababu ya kuhoji mfumo wetu wa elimu.Je, unatuandaa kuwa watu wa namna gani?

Inawezekana kabisa hata wewe umeajiriwa, hujajiajiri.
 
4db0da18a019f59247986075650ffa21.jpg
 
kila topic ya mathematics ina matumiz yake alafu iyo X ni assuming variable tu kwa kwa kukusaidia nenda ka Google application ya kila topic ya math ndio utafahamu sio vichaa kuwekwa ivo bt sema wanakaza sana kwenye pepa za kibongo
 
kwa engineers maana ya hesabu inakuja kidogo. ila computer zimepunguza matumizi ya hizo hesabu direct
 
Unaipata mara nyingi tu sema shida yako ni kutoitambua. Ukijua purpose/ goal ya wewe kufundishwa hiyo equation na equations nyingine nyingi utaona zinavyokusaidia kwenye maisha.
Tatizo la hii nchi wengi hatuwez practice tunapanga sana ila hatufanyi mipango ndio maana izo equations tunaona si kitu
 
Kwanini nisome kitu ambacho sitakuja kukitumia maishani?

Mimi nadhani elimu inapaswa kunisaidia kuishi... haina maana nikiwa nina masters halafu siwezi hata ku-afford kujenga nyumba ya kuishi!!!

Niambie tafsiri yako ya mafanikio ni ipi.
Mkuu, unaliangalia suala hili kwa ufinyu mno. Jaribu kupanua wigo wako wa kufikiri na uliangalie jukumu la elimu kwa upana wake kidhahnia na hata kifalsafa.

Kama tukikuweka wewe hapo ambaye umesoma na kutafuta hiyo x ambayo unadai haijakusaidia na mtu ambaye hajasoma kabisa hii elimu ya darasani; na bila kujali uwezo wenu wa kiuchumi, tunakutegemea wewe uwe na welewa mpana wa mambo mbalimbali kimalimwengu. Kama huyo mwenzio anaamini kuwa radi inatokana na jogoo kubwa lenye hasira linapogonganisha mabawa yake, wewe tunakutegemea ujue kuwa radi ni matokeo ya msuguano wa chaji hasi na chanya huko mawinguni zinapogongana katika mazingira maalumu; na tunakutegemea ukijenga nyumba uweke kinga zitakazofanya nyumba yako isipigwe na radi. Hiyo ndiyo elimu. Ni mambo yote yanayokutofautisha wewe na mwenzako ambaye hakuipata - hata kama ni milionea!

Na kwa maoni yangu hakuna kitu ambacho umesoma shuleni ambacho hakijakusaidia maishani. Tatizo lako unaangalia mambo kijuujuu tu huku umekazia macho kwenye utajiri.

Narudia tena; kama lengo lako ni kutajirika hakuna hata haja ya kwenda shule na kupoteza muda wako bure. Hata watoto wako kama umewapeleka shule kwa lengo la kutajirika unawapotezea muda bure tu. Watoe huko shuleni na uwanunulie hata bodaboda waanze ujasiriamali kungali asubuhi na mapema.

The way you see the problem IS the problem!!!
 
Haya maisha chenye thamani ni "K" tu hiyo "X" hata waliokutuma hawajaipata na hawataipata kwasababu wanatafuta kitu ambacho hakipo.

"A mathematician is a blind man in a dark room looking for a black cat which is not there"
Charles Darwin
 
Well, nipo na vijana wengi sana mtaani... wana degrees za I.T, banking, law n.k lakini wameshindwa kutumia hata hiyo algebra.Kifupi maisha yamewagonga.. algebra waliyojifunza iliwaandaa kuajiriwa.. hawajaweza kumaster maisha.

Hiyo inanipa sababu ya kuhoji mfumo wetu wa elimu.Je, unatuandaa kuwa watu wa namna gani?

Inawezekana kabisa hata wewe umeajiriwa, hujajiajiri.
Wapo wengi walioajiriwa pia na kutajirika lakini hizo elimu zao hazijawasaidia in real sense

wanafanya mambo kama routine tu na wala sio kubadilisha yanavyofanywa ili kuwe na ubora na ufanisi zaidi,

hii ndio inayofanyw hata bara letu limedumaa licha ya kuzalisha wasomi wengi na wengi pia wamesoma nje ya nchi ambako kuna hiyo mitaala/mifumo ya elimu unayoona ni bora kuliko ya Tanzania...

lakini wanakuja na mentality kama za kutumia elimu kujipatia kipato badala ya kuleta mabadiliko katika kukabiliana na changamoto ili kurahisisha maisha ya mwanadamu kiujumla.

hilo ni tatizo lao, sio tatizo la mfumo wa elimu
Elimu hii hii, sayansi hihii, uchumi huhuu ndio imezalisha ma engineer, wachumi, madaktari bingwa, wagunduzi, huko ulaya, uchina India na very kwingineko tangia miaka , tofauti kama ipo ni kidogo sana
Tofauti ya matokeo ya elimu kwao na kwetu ni sababu ya attitude za kivivu na tamaa

Hili ni tatizo kubwa sana
 
Mkuu, unaliangalia suala hili kwa ufinyu mno. Jaribu kupanua wigo wako wa kufikiri na uliangalie jukumu la elimu kwa upana wake kidhahnia na hata kifalsafa.

Kama tukikuweka wewe hapo ambaye umesoma na kutafuta hiyo x ambayo unadai haijakusaidia na mtu ambaye hajasoma kabisa hii elimu ya darasani; na bila kujali uwezo wenu wa kiuchumi, tunakutegemea wewe uwe na welewa mpana wa mambo mbalimbali kimalimwengu. Kama huyo mwenzio anaamini kuwa radi inatokana na jogoo kubwa lenye hasira linapogonganisha mabawa yake, wewe tunakutegemea ujue kuwa radi ni matokeo ya msuguano wa chaji hasi na chanya huko mawinguni zinapogongana katika mazingira maalumu; na tunakutegemea ukijenga nyumba uweke kinga zitakazofanya nyumba yako isipigwe na radi. Hiyo ndiyo elimu. Ni mambo yote yanayokutofautisha wewe na mwenzako ambaye hakuipata - hata kama ni milionea!

Na kwa maoni yangu hakuna kitu ambacho umesoma shuleni ambacho hakijakusaidia maishani. Tatizo lako unaangalia mambo kijuujuu tu huku umekazia macho kwenye utajiri.

Narudia tena; kama lengo lako ni kutajirika hakuna hata haja ya kwenda shule na kupoteza muda wako bure. Hata watoto wako kama umewapeleka shule kwa lengo la kutajirika unawapotezea muda bure tu. Watoe huko shuleni na uwanunulie hata bodaboda waanze ujasiriamali kungali asubuhi na mapema.

The way you see the problem IS the problem!!!
Hujajibu swali mkuu...

Mafanikio maana yake nini?
 
Haya maisha chenye thamani ni "K" tu hiyo "X" hata waliokutuma hawajaipata na hawataipata kwasababu wanatafuta kitu ambacho hakipo.

"A mathematician is a blind man in a dark room looking for a black cat which is not there"
Charles Darwin
...looking for whatttt???. Teh teh teh tiiih
 
Wapo wengi walioajiriwa pia na kutajirika lakini hizo elimu zao hazijawasaidia in real sense

wanafanya mambo kama routine tu na wala sio kubadilisha yanavyofanywa ili kuwe na ubora na ufanisi zaidi,

hii ndio inayofanyw hata bara letu limedumaa licha ya kuzalisha wasomi wengi na wengi pia wamesoma nje ya nchi ambako kuna hiyo mitaala/mifumo ya elimu unayoona ni bora kuliko ya Tanzania...

lakini wanakuja na mentality kama za kutumia elimu kujipatia kipato badala ya kuleta mabadiliko katika kukabiliana na changamoto ili kurahisisha maisha ya mwanadamu kiujumla.

hilo ni tatizo lao, sio tatizo la mfumo wa elimu
Elimu hii hii, sayansi hihii, uchumi huhuu ndio imezalisha ma engineer, wachumi, madaktari bingwa, wagunduzi, huko ulaya, uchina India na very kwingineko tangia miaka , tofauti kama ipo ni kidogo sana
Tofauti ya matokeo ya elimu kwao na kwetu ni sababu ya attitude za kivivu na tamaa

Hili ni tatizo kubwa sana
You are a smart woman indeed! Bila kubadili fikra zetu Waafrika hatutakaa tuendelee. Hata elimu, ambayo ndiyo inapaswa kuwa mkakati mama katika ukombozi wetu, tumeivisha jukumu ambalo silo lake, jukumu la kibinafsi na ambalo mara nyingi halina faida kwa jamii kuu. Kama jukumu la elimu ni kumtajirisha aipataye, ni nani atakayeiokoa jamii na kuipigania? Tunashangaa kwa nini sisi hatugundui cho chote. Utagundua nini cha maana kama lengo lako ni kutajirika? Watu wanajitoa mhanga usiku na mchana ili waache legacy katika uwanja wao wa kitaaluma, sisi tumekazana kutajirika kama lengo letu la jumla la wasomi wetu. Halafu tunalalamika wasomi wetu wanapokimbilia siasa. Eti wasomi wetu hawana faida kwa taifa letu. Watakuwaje na faida kama jamii yenyewe inawategemea kuwa matajiri kama zao la moja kwa moja la elimu yao? Na wakitajirika then what?

Bila kubadili mtazamo na mkondo wetu wa fikra haki ya nani tutaendelea kuzalisha wasomi wabinafsi na wasiokuwa na faida yo yote katika ukombozi wa Jamii yetu. Umenifurahisha sana mkuu. Napenda sana watu smart na ambao wanaweza kufikiri nje ya boksi!!!
 
Yaaani Heading umeiweka vizuri sana,Hongera.! ila nlipochoka ni pale nlipoona maswala ya hesabu oohh oouuhh ouhh ma file ya kichwa yameingia virus vya "trojanhorse"
 
Back
Top Bottom