tukiacha teknolojia hata wao tu hawapo serious...kuna vitu vingine vinahitaji akili tu na kujiongeza..kwa mfano kuna movie ya kibongo nikaona eti jini linaagiza redbull bar na wakati wa kuvuka barabara jini linaangalia kulia na kushoto...sasa hapo si hata mtoto mdogo ataona they are not serious!!!
Tukubali tukatae utandawazi pia unachangia sana tuone vyetu havifai. Na hii inatokana na ukweli kwamba tunajifananisha na wenzetu walio tutangulia hatua 1000 mbele yetu. Ulinganishaji huu haupo fair hata kidogo. Nakumbuka Enzi hizo kuna Maigizo ya mambo hayo jahazi ya kaole ya kina bishanga waridi sekioni kusema ukweli ilikuwa inavutia wengi sana kutokana na ukweli kwamba ni wachache sana miongoni mwa wana jamii walikiwa na Access ya kuangalia movie za nje. If am wrong katikati ya miaka ya 2000 hadi 2005 movie za ki Nigeria tulikuwa tuna zi appreciate sana kina Ramsey Noah Geneviev ila ni Wangapi leo wanazikubali hizi movie? Hata za kina bishanga leo hazina mvuto wakati enzi hizo zilikuwa ndo zenyewe. Nilikuwa nawaona wasanii hawafanyi vizuri lakini kusema ukweli tunapojilinganisha na wa nje ni sawa sawa na Timu ya taifa stars Vs Germany au Diamond Vs jay z huu ni uonevu wa hali ya juu. Imagine bongo movie 10 years ago ilikuwaje na imagine itakuwa vipi miaka 10 kutoka sasa.
tusihukumu sana zipo nzuri nyingi tu.
Hivi watanzania nani kawaroga mpaka vya kwenu hata kama si vizuri mpaka mnavikataa? Hivi ni kweli kwamba hata vichwa vyenu tayari navyo vimebinafisishwa? Acheni ushamba wa kudharau kwenu na kutamani vya nje. Cha ajabu huko Ulaya au America hawashobokei za kwenu kama mnavyofanya nyinyi/ninyi. Mjilaumu wenyewe na mje na suluhu nini kifanyike kuboresha movie za ndani
Hakuna. Hazijawahi kuwepo. Na hazita kuwepo
Tukubali tukatae utandawazi pia unachangia sana tuone vyetu havifai. Na hii inatokana na ukweli kwamba tunajifananisha na wenzetu walio tutangulia hatua 1000 mbele yetu. Ulinganishaji huu haupo fair hata kidogo. Nakumbuka Enzi hizo kuna Maigizo ya mambo hayo jahazi ya kaole ya kina bishanga waridi sekioni kusema ukweli ilikuwa inavutia wengi sana kutokana na ukweli kwamba ni wachache sana miongoni mwa wana jamii walikiwa na Access ya kuangalia movie za nje. If am wrong katikati ya miaka ya 2000 hadi 2005 movie za ki Nigeria tulikuwa tuna zi appreciate sana kina Ramsey Noah Geneviev ila ni Wangapi leo wanazikubali hizi movie? Hata za kina bishanga leo hazina mvuto wakati enzi hizo zilikuwa ndo zenyewe. Nilikuwa nawaona wasanii hawafanyi vizuri lakini kusema ukweli tunapojilinganisha na wa nje ni sawa sawa na Timu ya taifa stars Vs Germany au Diamond Vs jay z huu ni uonevu wa hali ya juu. Imagine bongo movie 10 years ago ilikuwaje na imagine itakuwa vipi miaka 10 kutoka sasa.
Jambazi anavua viatu????
Hakuna uhalisia hata kidogo
Kama mimi vile yaani zangu ni NOLLYWOOD kwa sababu zinamafunzo ndani yake. Simjui mwigizaji yeyote wa Bongo movie kwa jina
Dah! Mie hizo za wanaigeria siku hizi ndiyo sisiwezi kabisa yani bora bongo movie,maana story zao wanaigeria ndiyo zilezile toka miaka ile, hasa hasa utaona wanafanya uchawi mwishoni kanisani.
Bongo muvi ni hovyo kabisa tangu afe The Great Kanumba.
Unakuta muvi ina part 1 na 2 ila sasa angalia hyo part tu mbna utakoma na roho yako mfano ni hii muvi inaitwa Bado nipo hai ilioneshwa EATV siku ya jumamosi aisee mule ndani ni hovyo hawajui hata jinsi ya kumaliza muvi. Waigizaji hawajielewi full makelele tu kamera inatikisika hovyohovyo mara sauti ipande na kushuka yaani halafu wanasema wanaibiwa kazi zao mi kwa kazi ipi hadi niibe ujinga huo.
Bora kanumba angekuwa hai ningekuwa naangalia filamu zake maana alikuwa anajua nn anafanya.
Kitu
Expendable
Blacksheep
No Retreat No Surrender
Iris
Krishna
Godfather
Airplane
Neria
Sarafina
Catch A Fire
The Graduate
Seven Samurai
Hotel In Rwanda
Sometimes In April
Themba
Good Dees
Rise And Fall Of Charles Tylor
Bongo Movie Huwezi Kukaa Unaangalia Na Mama Mkwe Wako.
mimi natofautiana na wewe! waigizaji wa sasa hawana ubunifu na sidhani hata kama wana muda wa kujielimisha zaidi kuhusu uigizaji! kila mmoja utamsikia akijisifia kuwa uigizaji uko damuni mwake tangu utoto kitu ambacho siyo kweli! akina bishanga walianza vizuri na hata leo ukiziangalia picha zao bado zina make sense! walitakiwa kujiendeleza kutokea pale ikibidi waende shule za sanaa (drama schools) ikibidi hata nchi za nje kama south africa ambako wako vizuri sana kwa kuigiza!
tatizo la wabong wanawaza kupiga pesa na siyo kuwekeza ili wapige pesa nyingi mbeleni! utawasikia wanalalamika kuwa watanzania hawapendi vitu vya kwa wanasahu hiyo ni kazi na biashara! mtu anataka kitu/bidhaa inayoendana na thamani ya pesa yake!
Nigeria wanajitahidi kuigza uhalisia
Niko poa Kadoda, umesharudi bongo?
Tatizo sidhani kama hawa watayarishaji wa hizi tunazoita muvi wana muda wa kutembelea majukwaa kama haya ili kupata feedback ya kazi zao but its about time we changed jamani. Tusilazimishane tu kupenda visivyopendeka. Hiyo ishu ya sumu ya panya imeniacha hoi mkuu hahaha, umeua. Tutafutane kaka.
Muvi za kibongo ni lazma kuwe na sini watu wawili mwanamke na mwanaume wanafanya shopping katika duka la nguo au wapo bichi.
Hata hizo za Nollywood hazijatofautiana sana na za Wabongo wote mle mle, walau filamu za Wasouth Africa na Wazimbabwe ziko safi