Movie: Nobody

Nimetoka kuicheki Jana, me waga nikimuona tu Angelina Jolie sijiulizi mara mbili kuhusu kudownload Ila Kwa movie hii ni tofauti kabisa na Jolie niliemzoea, Kwa tulivomzoea Naweza sema hii ndio movie ya kawaida kutoka kwake

Angelina Jolie kwenye Movie she’s freaking goddess hakoseagi yule mwana mama
 
...Hutch Mansell, kwenye maisha aliyochagua kuishi, vita na walimwengu hakuitaka, ni yeye mmoja, mkewe kipenzi na watoto aliowathamini..
basi ni hivo tu..
...Jumatatu ya leo aliyoamini kamaliza kazi zake za kila siku, giza lilipoingia watu wawili wakaingia nalo,
wakamletea kazi nyingine ukiacha aliyoacha ofisini kwake mchana..nyumba yake ilivamiwa!..
...Walichotaka ni pesa tu, wakazichukua huku wakimwachia jina baya kwa familia yake, mkewe alimuona mume muoga usiku,
asubuhi majirani wakamdhihaki kuwa hawezi hata kuwadhibiti watu wawili!, sasa aliweza nini kingine!..
...Akafadhaika nyumbani, akaikosa salamu ya mtoto wake asubuhi, akanyimwa amani na wafanyakazi ofisini,
wakamvika cheo cha ubaba mzazi tu, wakamvua cha ubaba kazi, hakika aliumia..
...Ni mtoto wake mdogo, mwanae wa mwisho, alipomshtakia kuwa wale wezi waliondoka na kidani cha shingoni cha paka wake,
Hutch akafunga safari hadi nyumbani kwa wale wezi, na alichokifata hakukipata, akapanda kwenye basi kurudi nyumbani..
...Ni humo kwenye gari la abiria ndipo palipombadilishia maisha yake, ni chombo hicho cha usafiri ndicho kilimrudisha kumkumbusha yeye ni nani!...kwanini!
...Walipanda vijana wa kirusi, wakaamrisha basi liwe chini ya himaya yao, wakataka kila mtu mule ndani atii kila wanalosema, hawakujua..ndio hawakujua..
...Alichowafanya vijana wale, kiliandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za dereva, akashuka akarudi nyumbani, huku akiacha kosa kubwa alilofanya barabarani, kosa gani!
..Yulian Kuznetsov, a notorious Russian mob enforcer, muuza madawa mwenye heshima mjini, mtu anaesimamisha magari barabarani na polisi wakiwepo, ili ye apite kwa miguu,
Jeuri ya pesa iliishi kwenye kifua chake, aliutawala mji, akawatawala na watu wake, taarifa zikamfikia kuwa katika vijana waliopigwa kwenye basi, na mdogo wake alikuwepo..
...Akaapa kumtafuta mfanyaji wa hilo tukio, mtu ambae hamuogopi yeye wala jina lake, akatoa amri Hutch aletwe mbele yake kabla ya jua la alfajiri,
na kweli watu wake walikwenda nyumbani kwa Hutch usiku...vitambaa usoni, silaha mkononi..
.....Kwenye chumba kidogo ndani ya nyumba yake, Hutch alimuhifadhi mkewe na watoto wake, mke alipouliza kuna nini, akajibiwa kwa utaratibu tu, kuwa asiwaite polisi!...
...Yess, Hutch Mansell, aliurudia umafia wake wa miaka mingi iliyopita, alitaka kuijenga heshima iliyopotea mtaani,
muda ambao familia yake haimuamini kwa maneno, ye alitaka kuwaonesha kwa vitendo,
kuwa wale wezi wawili wa siku ile ni wachache, ye alihitaji kundi la watu kama wa leo!..
...Mkewe alipotoka ndani na familia yake, walipoona maiti zilizozagaa kwenye nyumba yao, wingi wa watu waliokufa, na muda uliotumika kuwaua,
mkewe aliamua kumkumbatia tu mumewe, hakuwa na namna nyingine..
mtoto wake akatabasamu, wote wakaamini moyoni, kuwa huyu sasa ndo baba,
naam!, baba mzazi, baba mlezi, na baba kazi...
...Taarifa ikamfikia Yulian Kuznetsov, akajulishwa kuwa hakuna mtu wako alienusurika kwenye ile nyumba,
akaamua kuulizia kwani huyo mtu ni nani!...majibu yaliyokuja yalimuacha mdomo wazi!..
An assassin employed by intelligence agencies to kill people, Hutch ni binadamu mbaya, mwenye roho ya kikatili kuwahi kuumbwa kwenye uso wa dunia,
hata mkewe alikuwa hamjui, alichojua yeye ni baba muoga, anaetunza familia tu..
..Ila serikali ya marekani inamtambua kama mtu pekee mwenye uwezo wa ajabu, alieshindikana na mtu yoyote chini ya jua, ni human made for killing,
...Lilipohitajika kwenda jeshi, alienda yeye..
Hutch hajui kuumiza mtu, anachoamini ni kuwa kwenye mkono wake, mwili wa binadamu na roho yake, wanatakiwa wasiishi pamoja..
...Mrusi akachefukwa, akapiga simu kwa kila aliemjua, akaandaa jeshi, akatoa amri kuwa hata kwa yeye kuwa maskini, lakini Hutch aletwe mbele yake akiwa maiti,
...Alichokuwa hakijui ni kuwa huyu former soldier huwa hasubiri kutafutwa, muda yeye anaulizia alipo mwanajeshi yule,
ndo wakati ambao Hutch anaisafirisha familia yake ili akaonane na yeye..
...Yeye anataka kumfuata, mwenzie yupo njiani anamfuata yeye...
....Alikuwa kayavagaa...
...Yulian Kuznetsov hakutaka kushindwa na mtu mmoja, akaamua liwalo na liwe, lakini sasa liwe kwa nani!!...kazi ilianzia hapo..


©Kaisal Ally
Umenikumbusha uandishi wa Ben R. Mtobwa. Kwenye story za tutarudi na rohobzetu? Na malaika wa shetani
 
...Hutch Mansell, kwenye maisha aliyochagua kuishi, vita na walimwengu hakuitaka, ni yeye mmoja, mkewe kipenzi na watoto aliowathamini..
basi ni hivo tu..
...Jumatatu ya leo aliyoamini kamaliza kazi zake za kila siku, giza lilipoingia watu wawili wakaingia nalo,
wakamletea kazi nyingine ukiacha aliyoacha ofisini kwake mchana..nyumba yake ilivamiwa!..
...Walichotaka ni pesa tu, wakazichukua huku wakimwachia jina baya kwa familia yake, mkewe alimuona mume muoga usiku,
asubuhi majirani wakamdhihaki kuwa hawezi hata kuwadhibiti watu wawili!, sasa aliweza nini kingine!..
...Akafadhaika nyumbani, akaikosa salamu ya mtoto wake asubuhi, akanyimwa amani na wafanyakazi ofisini,
wakamvika cheo cha ubaba mzazi tu, wakamvua cha ubaba kazi, hakika aliumia..
...Ni mtoto wake mdogo, mwanae wa mwisho, alipomshtakia kuwa wale wezi waliondoka na kidani cha shingoni cha paka wake,
Hutch akafunga safari hadi nyumbani kwa wale wezi, na alichokifata hakukipata, akapanda kwenye basi kurudi nyumbani..
...Ni humo kwenye gari la abiria ndipo palipombadilishia maisha yake, ni chombo hicho cha usafiri ndicho kilimrudisha kumkumbusha yeye ni nani!...kwanini!
...Walipanda vijana wa kirusi, wakaamrisha basi liwe chini ya himaya yao, wakataka kila mtu mule ndani atii kila wanalosema, hawakujua..ndio hawakujua..
...Alichowafanya vijana wale, kiliandikwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za dereva, akashuka akarudi nyumbani, huku akiacha kosa kubwa alilofanya barabarani, kosa gani!
..Yulian Kuznetsov, a notorious Russian mob enforcer, muuza madawa mwenye heshima mjini, mtu anaesimamisha magari barabarani na polisi wakiwepo, ili ye apite kwa miguu,
Jeuri ya pesa iliishi kwenye kifua chake, aliutawala mji, akawatawala na watu wake, taarifa zikamfikia kuwa katika vijana waliopigwa kwenye basi, na mdogo wake alikuwepo..
...Akaapa kumtafuta mfanyaji wa hilo tukio, mtu ambae hamuogopi yeye wala jina lake, akatoa amri Hutch aletwe mbele yake kabla ya jua la alfajiri,
na kweli watu wake walikwenda nyumbani kwa Hutch usiku...vitambaa usoni, silaha mkononi..
.....Kwenye chumba kidogo ndani ya nyumba yake, Hutch alimuhifadhi mkewe na watoto wake, mke alipouliza kuna nini, akajibiwa kwa utaratibu tu, kuwa asiwaite polisi!...
...Yess, Hutch Mansell, aliurudia umafia wake wa miaka mingi iliyopita, alitaka kuijenga heshima iliyopotea mtaani,
muda ambao familia yake haimuamini kwa maneno, ye alitaka kuwaonesha kwa vitendo,
kuwa wale wezi wawili wa siku ile ni wachache, ye alihitaji kundi la watu kama wa leo!..
...Mkewe alipotoka ndani na familia yake, walipoona maiti zilizozagaa kwenye nyumba yao, wingi wa watu waliokufa, na muda uliotumika kuwaua,
mkewe aliamua kumkumbatia tu mumewe, hakuwa na namna nyingine..
mtoto wake akatabasamu, wote wakaamini moyoni, kuwa huyu sasa ndo baba,
naam!, baba mzazi, baba mlezi, na baba kazi...
...Taarifa ikamfikia Yulian Kuznetsov, akajulishwa kuwa hakuna mtu wako alienusurika kwenye ile nyumba,
akaamua kuulizia kwani huyo mtu ni nani!...majibu yaliyokuja yalimuacha mdomo wazi!..
An assassin employed by intelligence agencies to kill people, Hutch ni binadamu mbaya, mwenye roho ya kikatili kuwahi kuumbwa kwenye uso wa dunia,
hata mkewe alikuwa hamjui, alichojua yeye ni baba muoga, anaetunza familia tu..
..Ila serikali ya marekani inamtambua kama mtu pekee mwenye uwezo wa ajabu, alieshindikana na mtu yoyote chini ya jua, ni human made for killing,
...Lilipohitajika kwenda jeshi, alienda yeye..
Hutch hajui kuumiza mtu, anachoamini ni kuwa kwenye mkono wake, mwili wa binadamu na roho yake, wanatakiwa wasiishi pamoja..
...Mrusi akachefukwa, akapiga simu kwa kila aliemjua, akaandaa jeshi, akatoa amri kuwa hata kwa yeye kuwa maskini, lakini Hutch aletwe mbele yake akiwa maiti,
...Alichokuwa hakijui ni kuwa huyu former soldier huwa hasubiri kutafutwa, muda yeye anaulizia alipo mwanajeshi yule,
ndo wakati ambao Hutch anaisafirisha familia yake ili akaonane na yeye..
...Yeye anataka kumfuata, mwenzie yupo njiani anamfuata yeye...
....Alikuwa kayavagaa...
...Yulian Kuznetsov hakutaka kushindwa na mtu mmoja, akaamua liwalo na liwe, lakini sasa liwe kwa nani!!...kazi ilianzia hapo..


Kaisal Ally
Ndugu yangu kama una group whatsapp naomba uniweke

Wewe ndie mtu pekee utakaenirudisha kwenye ulimwengu wa filamu maana nina miaka saba niliacha kufuatilia izi vitu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom