Kuna somo kubwa nimejifunza

Kuna somo kubwa nimejifunza

Mlimani health center

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2021
Posts
600
Reaction score
1,526
Miaka michache iliyopita kulikuwa na dada mmoja ambaye nilikuwa namfahamu kwa mbali. Alikuwa mfanyabiashara.

Kwenye mitandao ya kijamii alikuwa anaonekana kuishi maisha ambayo wengi walikuwa wanayatamani. Mara vacation, hoteli za kifahari, simu za gharama, shopping za kila mara. Ukiangalia picha zake, ungeamini hana tatizo lolote la maisha.

Wengi wetu tulikuwa tunasema, "Huyu maisha yake yamekaa." Kila mtu alikuwa na tafsiri yake kuhusu chanzo cha mafanikio yake.

Lakini siku moja zikaja taarifa za kusikitisha kuwa amefariki akiwa anapatiwa matibabu.

Baada ya msiba ndipo baadhi yetu tulipopata nafasi ya kufika nyumbani kwao. Kilichotukuta kilitufundisha somo ambalo sitalisahau. Nyumba ilikuwa ya kawaida sana, mazingira yalionyesha familia inaishi maisha ya kawaida yenye changamoto nyingi.

Hata maandalizi ya msiba yalikuwa ya uwezo wa kawaida wa familia—tofauti kabisa na picha ya maisha ya kifahari aliyokuwa akiionyesha mitandaoni.

Ndipo nikagundua kuwa mara nyingi tunavutiwa na kile tunachokiona kwenye mitandao, bila kujua uhalisia wa maisha ya mtu.

Somo langu si la kumhukumu marehemu wala familia yake. Ni kutukumbusha sisi tulio hai kwamba tusiishi kwa ajili ya kuonekana. Usiingie kwenye madeni au kujitesa ili watu waseme una maisha mazuri. Mitandao inaonyesha sehemu ndogo tu ya maisha ya mtu, si hadithi yake yote.

Ishi maisha yanayokupa amani, si maisha yanayowavutia watu. Mwonekano unaweza kudanganya, lakini uhalisia hujitokeza siku zote.
 
Kumbe ni nyumbani kwao(kwa wazazi) na sio kwake.

Wabongo mnapenda sana watu wawajibike kwenye mambo
yasiyowahusu.
 
Miaka michache iliyopita kulikuwa na dada mmoja ambaye nilikuwa namfahamu kwa mbali. Alikuwa mfanyabiashara.

Kwenye mitandao ya kijamii alikuwa anaonekana kuishi maisha ambayo wengi walikuwa wanayatamani. Mara vacation, hoteli za kifahari, simu za gharama, shopping za kila mara. Ukiangalia picha zake, ungeamini hana tatizo lolote la maisha.

Wengi wetu tulikuwa tunasema, "Huyu maisha yake yamekaa." Kila mtu alikuwa na tafsiri yake kuhusu chanzo cha mafanikio yake.

Lakini siku moja zikaja taarifa za kusikitisha kuwa amefariki akiwa anapatiwa matibabu.

Baada ya msiba ndipo baadhi yetu tulipopata nafasi ya kufika nyumbani kwao. Kilichotukuta kilitufundisha somo ambalo sitalisahau. Nyumba ilikuwa ya kawaida sana, mazingira yalionyesha familia inaishi maisha ya kawaida yenye changamoto nyingi.

Hata maandalizi ya msiba yalikuwa ya uwezo wa kawaida wa familia—tofauti kabisa na picha ya maisha ya kifahari aliyokuwa akiionyesha mitandaoni.

Ndipo nikagundua kuwa mara nyingi tunavutiwa na kile tunachokiona kwenye mitandao, bila kujua uhalisia wa maisha ya mtu.

Somo langu si la kumhukumu marehemu wala familia yake. Ni kutukumbusha sisi tulio hai kwamba tusiishi kwa ajili ya kuonekana. Usiingie kwenye madeni au kujitesa ili watu waseme una maisha mazuri. Mitandao inaonyesha sehemu ndogo tu ya maisha ya mtu, si hadithi yake yote.

Ishi maisha yanayokupa amani, si maisha yanayowavutia watu. Mwonekano unaweza kudanganya, lakini uhalisia hujitokeza siku zote.
Muhimu kupambana ili kuifikia ndoto hizo,kuliko kufake maisha, Mungu Mwema!
 
Unashindana Kuandaa Msiba....??
Hakunaga Msiba Wa Kifahari Kamwe....
 
Kwahiyo alikuwa anaponda Raha halafu nyumbani Hali mbaya, sasa si Bora angeandika wosia wa kuzikwa baharini Tu, unarudije nyumbani Kwa Hali hiyo?
 
Maisha yangu ya nje ukikutana na Mimi na uhalisia ni vitu tofauti wapo wanaotamn kuwa hv Ila usiige utakufa
 
Afu nyumbani kwa wazazi ni jukumu lenu wote sio la mmoja mwache apumzike kwa amani
 
Miaka michache iliyopita kulikuwa na dada mmoja ambaye nilikuwa namfahamu kwa mbali. Alikuwa mfanyabiashara.

Kwenye mitandao ya kijamii alikuwa anaonekana kuishi maisha ambayo wengi walikuwa wanayatamani. Mara vacation, hoteli za kifahari, simu za gharama, shopping za kila mara. Ukiangalia picha zake, ungeamini hana tatizo lolote la maisha.

Wengi wetu tulikuwa tunasema, "Huyu maisha yake yamekaa." Kila mtu alikuwa na tafsiri yake kuhusu chanzo cha mafanikio yake.

Lakini siku moja zikaja taarifa za kusikitisha kuwa amefariki akiwa anapatiwa matibabu.

Baada ya msiba ndipo baadhi yetu tulipopata nafasi ya kufika nyumbani kwao. Kilichotukuta kilitufundisha somo ambalo sitalisahau. Nyumba ilikuwa ya kawaida sana, mazingira yalionyesha familia inaishi maisha ya kawaida yenye changamoto nyingi.

Hata maandalizi ya msiba yalikuwa ya uwezo wa kawaida wa familia—tofauti kabisa na picha ya maisha ya kifahari aliyokuwa akiionyesha mitandaoni.

Ndipo nikagundua kuwa mara nyingi tunavutiwa na kile tunachokiona kwenye mitandao, bila kujua uhalisia wa maisha ya mtu.

Somo langu si la kumhukumu marehemu wala familia yake. Ni kutukumbusha sisi tulio hai kwamba tusiishi kwa ajili ya kuonekana. Usiingie kwenye madeni au kujitesa ili watu waseme una maisha mazuri. Mitandao inaonyesha sehemu ndogo tu ya maisha ya mtu, si hadithi yake yote.

Ishi maisha yanayokupa amani, si maisha yanayowavutia watu. Mwonekano unaweza kudanganya, lakini uhalisia hujitokeza siku zote.
Kitu gani kimafanya uamini hakuwa na amani katika maisha yake!
 
Back
Top Bottom