Morogoro: Mji wa watu goigoi

Morogoro: Mji wa watu goigoi

Sigara Kali

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2017
Posts
3,708
Reaction score
8,746
Nipo hapa Morogoro kwa wiki kama mbili hivi sasa, nimetokea mkoani huko Kanda ya ziwa. Kwa siku chache nilizokaa hapa nimegundua mijitu ya hapa ni mivivu sana mabishoo mno halafu wengi njaa hawana kazi za kufanya, wanaume wengi wa Moro ni wavivu sana.

Wadada wengi masistaduu ila wanaishi kwa kudanga, baadhi ya wadada wanaojielewa wanafanya kazi viwandani huko mazafa, polyester na kwingineko.

Watu wa Morogoro mjini inaonekana wengi wavivu kupika mida ya jioni kila uchochoro wa mji unafuka Moshi wa chipsi mayai na mishikaki na kuku broiler watu kibao wake kwa waume utakuta wamejazana kula chips.

Migahawa mingi ya Moro hupati vyakula vyenye afya kama ugali wa dona na udaga, wao ni mwendo wa kula sembe.

Supu ya pweza inagombaniwa hapa mjini, kuna jamaa anauza supu ya pweza mitaa karibu na masika pale unakutana na masela kibao wanaigombania, hawa jamaa hawana tofauti na wanaume wa Dar.

N.B: Watu wa Morogoro tembeleeni mikoani msiishie Dar tu mnaharibikiwa mjue naona tabia za watu wa Dar zishahamia Moro
 
Kuhusu vyakula mleta mada hujakosea. Ni mkoa uliojaliwa kila aina ya chakula, lakini nenda kwenye migahawa na hoteli zao hutatofautisha na mamantilie.
 
Sigara Kali
Wakumbuka maamdamano ya Sudan kisa unga wa ngano umepanda bei?
Umewahi kukaa/kuishi mitaa ya wapemba/wahindi?
Umewahi kuishi maisha ya wamaasai huko longido?
Natumai utakua umepata picha ya tamaduni za watu
 
Mji kasoro, aisee nimeishi sana huo mji for more than 10 years. Maendeleo yake na mabadiliko ni kwa speed ya kinyonga sana. Hapajabadilika kabisa licha ya kuondoka huko miaka 10 iliopita!
 
Kwa hiyo ukila udaga na dona wewe ndio kidume... Musoma na Mara kuna chips na makuku ya kisasa kama kawa ukisogea Mwanza makaka poa wapo lundo wanaliwa kama kawa mnatumia nguvu kutudanganya utadhani hatujawahi kufika uko maporini kwenu,jambo umelikuta Moro unatushambulia wanaume wa Dar hakika mkoani kuna dumaza akili.
 
Hujakaa morogoro wewe ila umekaa morogoro ambayo ni part ya dar.

Morogoro ni mji ambao una sehemu zake (vimji)vinavyojitegemea kama.

morogoro mjini.
Kilosa.
Kilombero.
Mikumi
Ifakara
Gairo
Mahenge .
Mvomero.
Malinyi

Zote ni sehemu zinazojitegemea na mtu akitoka kati ya sehemu mojawapo akitaka kwenda moro mjini anasema na anapanga safari kwamba anaenda morogoro kama nyie mnavyotoka mkoani na kuja moro yaani huwa hawajiesabii kwamba wako morogoro.

Unaweza kumuuliza mtoto au kijana wa ifakara kwamba ulishawahi kufika moro kama bado atakwambia bado sijafika morogoro na wakati huo huo yuko ndani ya mkoa wa morogoro.

Huko nilikotaja ukiachana na morogoro mjini ndio utakutana na wanamoro halisi wachapa kazi.

Mfano ukienda kilombero utakutana na mashamba ya miwa hekta kibao unafikiri wanalima wakina nani kama sio wanamoro wangekuwa wavivu ungeona ile miwa na kununua sukari yao KILOMBERO SUGAR.


Ukienda ifakara,lupiro mpaka malinyi huko kuna bonde la mpunga hekta kibao unafikiri wanalima wakina nani kama siyo wanamoro wangekuwa wavivu ungeona mpunga unalimwa .

Acha kuisema moro wewe umefika hapo tu mjini ambapo Asilimia kubwa ya vijana wanafanya changes na vijana wa dar

Vijana wa moro wanatoka jioni wanaenda kula bata dar hivyo hivyo vijana wa dar wanatoka wanakuja kula bata moro mjini.


Siku inayofuata kila mtu anarudi kwenye mji wake.


Wewe haujakaa moro ila umekaa part ya moro kwa hiyo usiipakazie moro nzima .

Tafuta mtu akutembeze moro yote huone maajabu yake na nikwambie tu itakuwa ni tour ya kuanzia mwezi mzima ili huweze kuimaliza yote.
 
Hujakaa morogoro wewe ila umekaa morogoro ambayo ni part ya dar.

Morogoro ni mji ambao una sehemu zake (vimji)vinavyojitegemea kama.

morogoro mjini.
Kilosa.
Kilombero.
Mikumi
Ifakara
Gairo
Mahenge .
Mvomero.
Malinyi

Zote ni sehemu zinazojitegemea na mtu akitoka kati ya sehemu mojawapo akitaka kwenda moro mjini anasema na anapanga safari kwamba anaenda morogoro kama nyie mnavyotoka mkoani na kuja moro yaani huwa hawajiesabii kwamba wako morogoro.

Unaweza kumuuliza mtoto au kijana wa ifakara kwamba ulishawahi kufika moro kama bado atakwambia bado sijafika morogoro na wakati huo huo yuko ndani ya mkoa wa morogoro.

Huko nilikotaja ukiachana na morogoro mjini ndio utakutana na wanamoro halisi wachapa kazi.

Mfano ukienda kilombero utakutana na mashamba ya miwa hekta kibao unafikiri wanalima wakina nani kama sio wanamoro wangekuwa wavivu ungeona ile miwa na kununua sukari yao KILOMBERO SUGAR.


Ukienda ifakara,lupiro mpaka malinyi huko kuna bonde la mpunga hekta kibao unafikiri wanalima wakina nani kama siyo wanamoro wangekuwa wavivu ungeona mpunga unalimwa .

Acha kuisema moro wewe umefika hapo tu mjini ambapo Asilimia kubwa ya vijana wanafanya changes na vijana wa dar

Vijana wa moro wanatoka jioni wanaenda kula bata dar hivyo hivyo vijana wa dar wanatoka wanakuja kula bata moro mjini.


Siku inayofuata kila mtu anarudi kwenye mji wake.


Wewe haujakaa moro ila umekaa part ya moro kwa hiyo usiipakazie moro nzima .

Tafuta mtu akutembeze moro yote huone maajabu yake na nikwambie tu itakuwa ni tour ya kuanzia mwezi mzima ili huweze kuimaliza yote.

Unatakiwa uelewe kilchozngumziwa ni mji wa morogoro sio mkoa wa morogoro
 
Ok na Kwa Arusha je Sehemu hipi ni mji na hipi ni mkoa ?
 
Back
Top Bottom