Morogoro Enzi Hizo: Hii ndio Morogoro bwana!

Morogoro Enzi Hizo: Hii ndio Morogoro bwana!

Siku hizi waterfalls hatuzioni tena mkuu..waluguru wamesafisha mlima kwa kukata miti na mashindano ya kuchoma moto mlima...ile scenic beauty haipo tena
kweli kabisaaa
morogoro imekuwa na joto Kali mnooo kuna nyakati huwa inatoa ngoma draw na dar
joto haswaaa ..wakulima wameikata kata miti mbaya zaidi watu wanazidi kusogeza makazi yao kule milimani hali hiyo inapelekea kuuwa uosto wa asili direct kwaajili ya shughuli mbali mbali za kibinaadamu ..nadhani sekta ya Mali asili na utalii kwa muda mrefu sasa imeshindwa kulithibiti hilo sijui kwanni ..nawakati wanajua fika kuwa vyanzo vya mito ya moro ndio vinavyo tegemewa kwa mahitaji ya maji hapa jijini dar wat if vyanzo hvyo vikizidi kukauka...!!?
zamani ule mto wa morogoro ulikuwa una jaa maji mnoo achilia mbali mto kikundi ..lakini sasa hvi mto kikundi umekuwa sio MTO tena Bali nikama mtaro tu..
 
Mie nilikuwa hapo chuo cha kilimo mwaka 1996-2000
Mengi mmeseama na kuongea sahihi isipokuwa kwa moro hakuna mango garden bali MANGO PARK
 
Natamani kufunguka lakini nina wasi wasi kama wewe sio mshkaji wangu wa Kitaa MG, classmate MG, basi ndugu weee yangu!
 
Hahaaa nimesoma shule ya msingi Mwere pale ...dah miaka ya 96 jaman moro ilikua tamu balaa ...nimekaaa sana msufini na mzee akajenga bigwa na kihonda kwa hiyo moro ni home japo wazee hawakai hapo ...mzee umeisahau Mango garden

95 nimemaliza hapo,unamkumbuka luzebele na kanda..
 
Soko chafu kuliko yote limejengwa 1953 nimesoma sua hakuna hata mtu wa moro mji umejaa wageni wenjeji wa moro kazi kubeba mabox kwa wahindi
 
Kigurunyembe alikuwa head master Mr magere.waliokuwa wanasoma pale wanajua machungu yake.na mazuri yake na ndio wengine kawafikisha hapo mlipo.
 
Ck hz hata mvua hakuna misitu yote imekatwa.watu wanajenga mahotel kwenye vyanzo vya maji!
 
Dahh habari za Moro bana,acha kabisa kipindi tunanyapianyapia watoto wa kilakaka aka kilei.
 
Naizungumzia zaidi Moro ya kipindi cha nyuma kidogo ya miaka ya 90 hadi 2000 mwanzoni... Hii town ya wajanja , vijana wanaojua kuvaa,wenye exposure, wapenda burudani na utafutaji... Ni mji uliofikia kuitwa jiji kasoro bahari kutokana na upatikanaji wa kila kitu kinachotakiwa... Kulikuwa na shule kubwa mbili Forest Hill na Kigurunyembe ambapo Forest ilikuwa ya watoto wa kishua na Kigurunyembe ilikuwa ya watoto wa kihuni... Mitaa maarufu ilikuwa ya kishua ni Forest, Liti, Sua na Rock garden... Mitaa maarufu ya ushenzini kulikuwa na Mji mpya, Kichangani, Mafiga.

Watu wa Moro ni wapenzi sana wa burudani haswa muziki na soka.... Kulikuwa na timu ya mji maarufu Reli kiboko ya vigogo hii ilikuwa daraja la kwanza alikuwa akija Simba au Yanga atoki.. Hiyo Reli naizugumzia ya kina Duncan Butinini, David Mihambo, Fikiri Magoso, Mohamed Mtono hapo kuna mshangiliaji maarufu sana wa kuitwa Ya mungu ambae ndio shabiki wa kwanza mtanzania kujichora mwilini... Licha ya Reli mtaani kulikuwa na team nyingi sana za mchangani kama chama langu Jamaica, kulikuwa na Black Viba, Small boys, Zaragoza baadae ikawa Moro United, Uruguay, Burkina Fasso, Rhino nk mtaani ilikuwa ni hatari.

Kwenye muziki Moro ina historia ndefu kidogo siwezi kuzungumzia enzi za kina Mbaraka Mwishehe kwa kuwa sikuwepo mimi nilikuwepo enzi za shimoni Morogoro Hotel na Rock Garden na maonyesho ya Forest Hill... Hapa kuna mtu anaitwa Dj Sweet Coffee alikuwa pale mtaa wa Konga ndio alomfundisha Udijei John Dilinga enzi hizo akiitwa John Mkimbizi sababu baba yake alikuwa mkimbizi kambi ya Solomon Mahlangu.. Disco lilikuwa linapigwa shimoni na mara nyingi alikuwa anakuja Dj Joseph Kusaga akimfundisha kazi Dj Peter Moe.

Watu wa Moro najua mpo wengi umu Jf naomba tukumbashane mawili matatu matukio, maujanja na mazuri ya Moro Town.

Moro Town ulikuwa pia mji wa kibabe.. Kulikuwa na watemi wa mji kina Slim mtoto wa sheikh mkuu, Matata, Gamba mcheza judo, vijana wa siafu toka mji mpya nk

Unaikumbuka Miss Morogoro? Unamkumbuka Alex Nictas?

Unawakumbuka mabingwa wa kudansi kitaifa? Kina Askofu, Bob Tigger, Super Ngedere nk

Unakumbuka mashindano ya magari? Unawakumbuka wakimbiza magari maarufu kina Collen, Steve, Pat, Kararambe, Shanto, De Santos nk

Unakumbuka wagiriki na bata zao kwa Mama Perina na Acropol? Unakumbuka masista duu na mabraza meni wa mitaa ya Forest?

Unakumbuka enzi za Mnet inaingia mjini? Moro mji wote ulikuwa na access ya kuona dstv bure.

Unakumbuka heka heka za ligi za mbuzi uwanja wa shujaa, makaburini kilakara na kikundi?

Unakumbuka Fete Fete? Unakumbuka Shan cinema? Unakumbuka swimming pool ya rock garden?

Unamkumbuka Mzee Mkwidu na Patel wakuu wa shule maarufu KG & Forest?

Unamkumbuka Maneno Big G rip? Unamkumbuka Mnambo wauza ngada maarufu?

Unamkumbuka Ndanje jambazi aliyetikisa mji? Unakumbuka ishu yake ya silaha na February Ma rope?

Unamkumbuka toz wa kipindi hicho Puzzo na kundi lake la kurap Watukutu akiwa na Sallam meneja wa Diamond sasa hivi? Unawakumbuka Gangster Family? Unawakumbuka Ze domp?

Unamkumbuka Achimpota? Unaikumbuka bus la Chambo?

Unakumbuka ule upepo uliokuja wa watu kuzamia Sauz na ulaya?

Umeishi mtaa gani Mafisa, Msufini, Kilakara, Ngoto, Kingo, Mlapakoro, Boma road, Sua, Vibandani, Relwe magorofani, Kigurunyembe, Madizini? Au wapi Umeishi?

Kuna watu maarufu wengi sana DSM ambao maujanja yao wamejifunzia Moro Town... Hakika Morogoro ni jiji kasoro bahari.

WATOTO WA MOROGORO MIKONO JUU.
Naikumbuka sana Moro, Aghakan
Nursery then nikaenda Nguzo 1988.Shani cinema nilikua na Mihogo ya kuchoma na pia Lunah palikua na koni na juice tamu sana
 
Naizungumzia zaidi Moro ya kipindi cha nyuma kidogo ya miaka ya 90 hadi 2000 mwanzoni... Hii town ya wajanja , vijana wanaojua kuvaa,wenye exposure, wapenda burudani na utafutaji... Ni mji uliofikia kuitwa jiji kasoro bahari kutokana na upatikanaji wa kila kitu kinachotakiwa... Kulikuwa na shule kubwa mbili Forest Hill na Kigurunyembe ambapo Forest ilikuwa ya watoto wa kishua na Kigurunyembe ilikuwa ya watoto wa kihuni... Mitaa maarufu ilikuwa ya kishua ni Forest, Liti, Sua na Rock garden... Mitaa maarufu ya ushenzini kulikuwa na Mji mpya, Kichangani, Mafiga.

Watu wa Moro ni wapenzi sana wa burudani haswa muziki na soka.... Kulikuwa na timu ya mji maarufu Reli kiboko ya vigogo hii ilikuwa daraja la kwanza alikuwa akija Simba au Yanga atoki.. Hiyo Reli naizugumzia ya kina Duncan Butinini, David Mihambo, Fikiri Magoso, Mohamed Mtono hapo kuna mshangiliaji maarufu sana wa kuitwa Ya mungu ambae ndio shabiki wa kwanza mtanzania kujichora mwilini... Licha ya Reli mtaani kulikuwa na team nyingi sana za mchangani kama chama langu Jamaica, kulikuwa na Black Viba, Small boys, Zaragoza baadae ikawa Moro United, Uruguay, Burkina Fasso, Rhino nk mtaani ilikuwa ni hatari.

Kwenye muziki Moro ina historia ndefu kidogo siwezi kuzungumzia enzi za kina Mbaraka Mwishehe kwa kuwa sikuwepo mimi nilikuwepo enzi za shimoni Morogoro Hotel na Rock Garden na maonyesho ya Forest Hill... Hapa kuna mtu anaitwa Dj Sweet Coffee alikuwa pale mtaa wa Konga ndio alomfundisha Udijei John Dilinga enzi hizo akiitwa John Mkimbizi sababu baba yake alikuwa mkimbizi kambi ya Solomon Mahlangu.. Disco lilikuwa linapigwa shimoni na mara nyingi alikuwa anakuja Dj Joseph Kusaga akimfundisha kazi Dj Peter Moe.

Watu wa Moro najua mpo wengi umu Jf naomba tukumbashane mawili matatu matukio, maujanja na mazuri ya Moro Town.

Moro Town ulikuwa pia mji wa kibabe.. Kulikuwa na watemi wa mji kina Slim mtoto wa sheikh mkuu, Matata, Gamba mcheza judo, vijana wa siafu toka mji mpya nk

Unaikumbuka Miss Morogoro? Unamkumbuka Alex Nictas?

Unawakumbuka mabingwa wa kudansi kitaifa? Kina Askofu, Bob Tigger, Super Ngedere nk

Unakumbuka mashindano ya magari? Unawakumbuka wakimbiza magari maarufu kina Collen, Steve, Pat, Kararambe, Shanto, De Santos nk

Unakumbuka wagiriki na bata zao kwa Mama Perina na Acropol? Unakumbuka masista duu na mabraza meni wa mitaa ya Forest?

Unakumbuka enzi za Mnet inaingia mjini? Moro mji wote ulikuwa na access ya kuona dstv bure.

Unakumbuka heka heka za ligi za mbuzi uwanja wa shujaa, makaburini kilakara na kikundi?

Unakumbuka Fete Fete? Unakumbuka Shan cinema? Unakumbuka swimming pool ya rock garden?

Unamkumbuka Mzee Mkwidu na Patel wakuu wa shule maarufu KG & Forest?

Unamkumbuka Maneno Big G rip? Unamkumbuka Mnambo wauza ngada maarufu?

Unamkumbuka Ndanje jambazi aliyetikisa mji? Unakumbuka ishu yake ya silaha na February Ma rope?

Unamkumbuka toz wa kipindi hicho Puzzo na kundi lake la kurap Watukutu akiwa na Sallam meneja wa Diamond sasa hivi? Unawakumbuka Gangster Family? Unawakumbuka Ze domp?

Unamkumbuka Achimpota? Unaikumbuka bus la Chambo?

Unakumbuka ule upepo uliokuja wa watu kuzamia Sauz na ulaya?

Umeishi mtaa gani Mafisa, Msufini, Kilakara, Ngoto, Kingo, Mlapakoro, Boma road, Sua, Vibandani, Relwe magorofani, Kigurunyembe, Madizini? Au wapi Umeishi?

Kuna watu maarufu wengi sana DSM ambao maujanja yao wamejifunzia Moro Town... Hakika Morogoro ni jiji kasoro bahari.

WATOTO WA MOROGORO MIKONO JUU.
Mzee nilikuwa Modeko pale,badae Sangasanga,mazimbu hatimae Kihonda.
Mitaa ya chamwino kulikuwa na washkaji watukutu balaa akina kobelo na jamaa ake,wale jamaa walikuwa wahuni sana cha kushangaza hawakuwa wanatumia bangi.
 
Nilishawahi kuposti humu kuwa Moro ni mji Mzuri lakini kwangu nakosa AMANI ninapoiangalia hiyo Milima naona kama INATAKA KUNIANGUKIA........................!!!

Sawa sawa na kuna Tangazo humu JF Linanitisha ninapoliona basi tu kwa sababu JF naipenda tu navumilia...................Sijui ni Kipande cha KUKU kimeveshwa TAULO...!!! au sijui ni NDUMBA ya Mshana Jr sijui ebu ona kwenye hii Link Vodacom (Marry Brown)
 
Back
Top Bottom