Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,440
- 1,029
Siku moja NYANI na MJUSI walikuwa juu ya mti wanavuta banghi.Mara MJUSI akajisikia kiu,akaamua kwenda kunywa maji kwenye mto wa karibu.Alipofika huko mtoni,MJUSI aliuawa na MAMBA.Yule MAMBA alifuatilia nyayo za MJUSI zinakotokea mpaka akaufikia ule mti alipo NYANI. NYANI alipomwona MAMBA, akashangaa huku akisema;"mwanangu MJUSI utakuwa umekausha maji ya mto wote,yaani umekunywa maji mpaka umevimba namna hiyo,anyway karibu tuendelee kupata dawa".