Monica wa Maganzo

Monica wa Maganzo

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Hii ni stori ya Monica wa Maganzo Shinyanga namna gani alijiingiza katika biashara ile.

Alizaliwa katika hospital ya Kolandoto mnamo mwaka 1983. Wazazi wake walikuwa ni wakulima. Baba yake mzee Magina alikuwa na wake wawili, Mama yake Monica akiwa mke wa pili.

Mzee Magina hakuwa na shida kihivyo maana pamoja kuwa mkulima alikuwa na biashara ndogo ndogo za kuuza vitu ndani ya mgodi wa mwadui. Kwahiyo Monica hakuwa na shida sana katika maisha yake tofauti na watu wengine kijijini pale.

Hakika ukimuna Monica huwezi amini kama kweli anaweza kujihusisha na biashara ile. Mtoto ameumbika mithili ya Sara wa kibinda, macho yake ya huwa, shingo imechongoka kama upanga wa mkata fito za kinyemberi. Sauti yake na mwendo wake hakika hutawenza kuamini. Sauti ya Monica ni ya vituo haina papara, kwa mara ya kwanza ukimuona utaridhia hakika mtoto huyu anafaa kuolewa.

Mnamo mwaka 1998 ndipo Monica alipojiunga na Sekondari ya Maswa Girls Sec School.
Huko ndiko sasa alipo anza kujifunza tabia tofauti tofauti.

Mwaka huo akiwa kidato cha kwanza alipata rafiki yake Mage mkazi wa sumbawanga. Walikuwa pamoja kila mmoja akielezea jinsi wanavyoishi nyumbani kwao.

Mage alimuomba Monica awaombe wazazi ili wakifunga shule waende Sumbawanga. Monica alikubali. Monica aliwaambia wazazi wake.

Fuatilia hii stori ya kusismua
Je Monica alipowaambia wazazi wake walisema na ilikuwaje usiikose kaa hapo hapo

Africa.jpg

 
Hii ni stori ya Monica wa Maganzo Shinyanga namna gani alijiingiza katika biashara ile.

View attachment 105197Alizaliwa katika hospital ya Kolandoto mnamo mwaka 1983. Wazazi wake walikuwa ni wakulima. Baba yake mzee Magina alikuwa na wake wawili, Mama yake Monica akiwa mke wa pili.

Mzee Magina hakuwa na shida kihivyo maana pamoja kuwa mkulima alikuwa na biashara ndogo ndogo za kuuza vitu ndani ya mgodi wa mwadui. Kwahiyo Monica hakuwa na shida sana katika maisha yake tofauti na watu wengine kijijini pale.

Hakika ukimuna Monica huwezi amini kama kweli anaweza kujihusisha na biashara ile. Mtoto ameumbika mithili ya Sara wa kibinda, macho yake ya huwa, shingo imechongoka kama upanga wa mkata fito za kinyemberi. Sauti yake na mwendo wake hakika hutawenza kuamini. Sauti ya Monica ni ya vituo haina papara, kwa mara ya kwanza ukimuona utaridhia hakika mtoto huyu anafaa kuolewa.

Mnamo mwaka 1998 ndipo Monica alipojiunga na Sekondari ya Maswa Girls Sec School.
Huko ndiko sasa alipo anza kujifunza tabia tofauti tofauti.

Mwaka huo akiwa kidato cha kwanza alipata rafiki yake Mage mkazi wa sumbawanga. Walikuwa pamoja kila mmoja akielezea jinsi wanavyoishi nyumbani kwao.

Mage alimuomba Monica awaombe wazazi ili wakifunga shule waende Sumbawanga. Monica alikubali. Monica aliwaambia wazazi wake.

Fuatilia hii stori ya kusismua
Je Monica alipowaambia wazazi wake walisema na ilikuwaje usiikose kaa hapo hapo

Annael na wewe umekuwa kama shigongo? au MziziMkavu na riwaya endelevu?
sawa bhana.
 
Last edited by a moderator:
^^
Umenikumbusha Maganzo,Mwadui,,tena ulipogusa Maswa girls,,nikakumbuka maeneo ya Binza day,
Miaka ile ya 90 lol
Time is really passing
Ngoja nisubiri part 2
^^
 
Mbona unatoa fupi fupi sana, vipi niendelee kuvizia au wiki ijayo tena?
 
Ilipoishia
Mage alimuomba Monica awaombe wazazi ili wakifunga shule waende Sumbawanga. Monica alikubali. Monica aliwaambia wazazi wake.

PART II
Usiku wa Kuhangaika


Mzee Magina alikataa kata kata sababu tu kwamba Monica ni mtoto pekee wa kike lakini mama yake Monica alimbembeleza na kumsihi njinsi Monica alivyokuwa akielezea kuhusu wazazi wake Mage.

Mke wa pili wa Mzee Magina alijulikana kwa jina Kagole lakini jina lake halisi alikuwa akiitwa Nyandalo Ni mwanamke aliyejaliwa kiwa na ushawishi wa hali ya juu. Mzee Magina alikuwa anapenda sana kumwita Kogole. Yaani alikuwa anatamka kwa Lugha ya kisukuma Kagole wane
Ikiwa na maana ya Kagole wangu.

Mzee Magina alikubali na kuhakikisha kuwa anampatia vitu vyote vya muhimu ikiwamo vitu vya kimila.

Siku ya kufunga shule ikafika Monica alisema anakumbuka kabisa siku hiyo ilikuwa siku ya ijumaa. Mimi na Mage tulifungasha mizigo yetu na kwenda kuwaaga wazazi wangu Maganzo.

Siku ya jumamosi Mzee Magina aliwasindikiza stend ya mabasi yanayotoka Mwanza kuelekea Tabora.

Walipo panda basi tu, ndipo Mage alianza kumweleza vitu vilivyomfanya Mage ashangae na kutamani wafike haraka aweze kujionea kwa macho yake. Stori zilizidi kupamba moto huku Mage akiwa ndiye kinara wa kutoa stori.

Ilipofika mida ya saa 10 za jioni tayari walikuwa wameshapita Tabora. Na msitu mnene ukawa unawaita, msitu ule ulikuwa namiti mikubwa mikubwa na kufanya jua lisionekane.

Nyimbo za ndege na sauti za wanyama mbali mbali zilitanda kwenye msitu huo, na istoshe mda huo njio ndio inaingia. Ghafla kulisikika mlio mkumbwa na kishindo wa "Pwaaaaaauuuu!!!" na basi walilokuwa wakisafilia "Roho ya paka" likayumba kulia kushoto kulia kushoto baada ya hapo likaacha njia.

Kila mmoja ndani ya basi alikuwa akimuomba Mungu wake. Basi lilipoteza mwelekeo na kujita linaparamia miti, likagonga mti mmoja na kumbiringika.

Monica: Niliona watu wenye nguo nyeupe wakitokea pande nne za dunia na mmoja wao akasema "muacheni kwanza huyu ngoja wengine wote tuwachukue" Nilijaribu kuongea kuwa uliza nyie ni nani lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sikuweza hata kuongea, akilini ninawaza cha kusema lakini siwezi.

Baada ya hapo kitu gani kilitoke endelea kufuatilia





 
napenda hapo kitu gani kilitokea,endelea kufatilia........

imenikumbusha enzi zile nafatiiaga hadithi za Shigongo
 
Ilipo ishia.
Monica: Niliona watu wenye nguo nyeupe wakitokea pande nne za dunia na mmoja wao akasema "muacheni kwanza huyu ngoja wengine wote tuwachukue" Nilijaribu kuongea kuwa uliza nyie ni nani lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sikuweza hata kuongea, akilini ninawaza cha kusema lakini siwezi.

Part II inaendelea....
Monica: Nikasikia sauti mmoja akiita "Gabriel, Gabriel" mmoja wa hao watu akageuka, hakika nilishindwa kuiona vizuri sura yake, maana uso wake ulikuwa unag'aa mithili ya miale ya jua.
Yule aliyeitwa kwajina hilo alijibu akisema "Yuhiel mshike mkono mlete hapa"

Ndipo Monica alipo poteza fahamu na hakuelewa tena kitu gani kinaendelea.

Sauti za ndege akiimba zilisikika kwa mbali, wengine ni kama miluzi ya watu wanaofukuza mbwa mwizi, zingine kama kuku akitafuta sehemu ya kutagia. Kila aina ya sauti zilisikika.

Pale ndipo nilipo pata fahamu na kuona moshi mnene ukitokea upande wa kulia kwangu. Sikuelewa huo moshi ni kwaajili ya nini Monica alisema.

Hakuna mtu hata mmoja aliye baki isipokuwa Monica pekee yake maana basi liliteketea lote kwa moto. Hakuna mabaki yoyote yaliyobaki.

Ndipo Monica akaanza kulia kwa sauti ya huzuni akiita Mage, Mage, Mage uko wapi. Kila akiita mwangi ulisikika ukirundia maneno yake. Hakuna hata chembe ya kitu kilibaki pale.

Ilikuwa ni kama saa 12 alfajiri ndipo alipogundua kumbe amebaki peke yake. Majeraha madogo madogo kwenye mguu wake wa kushoto na mgongoni aliyapata. Kusema kweli Monica hakuumia.
Hakuelewa ni kitu gani kilichomfanya achomoke ndani ya gari pasipo yeye kuumia.

Ilikuwa kama umbali wa mita 20 kutoka barabarani, akiendelea kulia hakuna mtu yeyote aliye pita barabarani. Macho yake yalivimba na kuwa mekundu mithili ya mtu aliyepakwa pilipili kwenye macho. Mdomo wake ulikauka na pua yake kujaa makamasi kama mama aliyepotelewa na mwanae mpenzi.

Mda huo Monica alijipa matumaini huenda Mage yupo sehemu na kuendelea kuita kwa sauti. Mpaka pale sauti yake ilipokauka na kushindwa kabisa kuongea.

Njaa nayo ilianza kunyemelea tumbo lake, kichwa chake kilikuwa kizito kana kwamba kabeba mzinga wa maboksi ya chaki. Alikuwa akisikia sauti ndani ya kicha ikitwanga "kiko! kiko! kiko! kiko!" Mpigo yake ya moyo yakipiga haraka haraka.

Japo kuwa Monica alikuwa kwenye majonzi sura yake zuri ya kiafrika haikupotea. kadri alivyozidi kufumba macho na kufunga mdomo mashimo yalijitokeza kwenye mashavu yake mithili ya visima juu ya mawe ya engaruka.

Monica alichoka, hakuwa na wakumsaidia wala kuongea naye tu. Monica alizoa kusikia sauti za watu leo hii hakuna hata mmoja wa kuongea naye. Monica aliishiwa nguvu, ndipo usingizi mzito ukampitia

Je usingizi huo ulikuwaje endelea kufuatilia



 
Niendelee nisiendelee!!?
 
....

...HII inanikumbusha Shybush pale bweni la chui ..........dadadek watoto wa mgodini ilikuwa chakula yetu....wapi Marieta......

......Mkubwa Masala uko wapi?
 
Ilipoishia..
Monica: Niliona watu wenye nguo nyeupe wakitokea pande nne za dunia na mmoja wao akasema "muacheni kwanza huyu ngoja wengine wote tuwachukue" Nilijaribu kuongea kuwa uliza nyie ni nani lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sikuweza hata kuongea, akilini ninawaza cha kusema lakini siwezi.

Part III Maisha mapya na mzee Kihamba
Ilikuwa yapata saa saba za mchana siku ya jumapili, Ndipo Monica aliposhituka kutoka usingizi.
Alipo fumbua macho aliona kundi la mbwa likiwa limemzunguka. Kila mbwa alikuwa ametoa ulimi nje na kutoa mpumzi "hahihahihahihahi". Alipotazama pembeni aliona mtu wa makamo akiwa amebeba mkuki.

Hakika alikuwa ni pande la mtu, alionekana ni mtu mwenye nguvu kwa haraharaka alionekana kama mtu mwenye umri wa miaka 50-60 hivi. Ndipo yule mzee alipiga mluzi mbwa wate wakamfuata. Akapiga mluzi tena kwa sauti tofauti mbwa wote wakalala.

Ndipo yule mzee akamsogelea Monica na kuongea kwa lugha ambayo Monica hakuielewa.
Monica alikaa na ndipo huyo mzee akamsogelea, naye akakaa chini karibu na monica.

Kusema kweli mzee alitoa harufu mbaya na isitoshe alikaa upande wa upepo unakotokea. Ndipo yule mzee akaongea kwa kiswahili kilicho nyooka.
Mzee: Unaitwa nani biti mrembo.
Monica: Naitwa Monica.
Mzee: Eehe imekuwaje ukohapa pekee yako na kuna mabaki ya vitu pale "alionesha kwa kidole"
Monika alieleza kila kitu kilichoteokea.
Ndipo mzee Kihamba akampa pole na kusema itabidi tuende kwangu
Monica hakuwa na uchanguzi mwingine alikubaliana na mzee kihamba.
Safari ilianza kwa miguu na ilikuwa mbali kiasi fulani. Baada ya kama saa moja Monica alichoka hakuweza tena kutembea. Ndipo mzee kihamba akamwambia Monica hebu tutafute kivuli tukae, maana naona umechoka sana.
Walipata kivuli na kukaa. Nipo mzee Kihamba akaanza kuelezea kisa chake.
Mimi ni mwenyeji wa Tanga kisa changu kufika hapa ni baada ya kusingiziwa kuwa nime muua mama yangu mzazi.
Kulikuwa na ugonvi baina ya mama yangu na mjomba yangu Uledi. Walikuwa ni wawili tu kwa babu yangu.
Kisa ilikuwa kugombania mali za urithi. Mjomba alikuwa anataka auze shamba la mikonge ambalo babu aliliacha. Lakini mama yangu alikua akikataa. Alikua akidai sivyema kuuza mali za urithi maana itakuwa thawabu kwa watoto wetu miaka ya mbeleni.
Ilikuwa siku moja mimi na mama yangu tuko shambani tunalima. Mjomba alikuja shambani akiwa na panga mkononi. Alikuja ghafla na akaisimika panga kichwani kwa mama yangu. Nilishikwa na butwaa sikuweza hata kusogea. Mama yangu alianguka chini.
Ndipo mjomba Uledi alichomoa panga kichwani kwa mama yangu na kuiweka miguuni kwangu. Hapa fahamu zangu zilikimbia.
Ndipo mjomba alikimbia akipiga kelele "Kihamba Kihamba umemuua dada yangu"
Sikuwa na kitu cha kuongea. Baada ya muda kidogo niliona kwa mbali kundi la watu wakiwa na mjomba wamebeba mapanga na silaha mbali mbali. Ndipo hapo fahamu zilipo nijia nilitoka mbia nikakimbia nikakimbia. Sijui nguvu zile nilipata wapi.
Endelea kuisoma hii stori ya kusisimua JF bana....
 
Ilipoishia.
Sikuwa na kitu cha kuongea. Baada ya muda kidogo niliona kwa mbali kundi la watu wakiwa na mjomba wamebeba mapanga na silaha mbali mbali. Ndipo hapo fahamu zilipo nijia nilitoka mbia nikakimbia nikakimbia. Sijui nguvu zile nilipata wapi.



Part III inaendelea…
Watu walinifukuza wakipiga kelele mkamateni mkamateni amerukwa na akili. Nilijaribu kujinasua na hao watu lakini bahati mbaya nilishindwa.
Walinikamata na kunifunga kuwa eti nimerukwa na akili. Walinichukua na kunifungia kwenye chumba chenye giza.
Kwa kweli sitaweza kumsahau Sabina, ni msichana aliyekuwa ananipenda kwa dhati. Alikuwa ni msichana mwenye adabu, heshima na hekima. Kila wakati alikuwa akinieleza "This is the word of bitches". Alipokuwa akisema hayo sikuelewa maana yake kabisa. Baada ya kunikuta haya ndipo nilipoelewa maana yake.
Aliposikia kuwa mimi nimerukwa na akili alitumia kila njia ili japo aje anione. Baba yake Sabina alikuwa na mwenyekiti wa kijiji chetu. Alimuomba sana sana ili aje anione. Baada ya kuomba muda mrefu ndio baba yake alipo ridhia kuwa aje. Walihakikisha kuwa wameweka ulizi ili nisije nikamdhuru.
Basi Sabina alikuja. Kusema kweli Sabina alikua ananifahamu sana tabia yangu. Aliwaomba walizi watuache pekee yetu. Walihakikisha wamenifunga vizuri.
Mzee Kihamba alipumua kidogo na kutikisa kichwa. Huku Monica akiwa anamsikiliza kwa makini.
Kisha akaendelea….
Nilipo muona Sabina Hakika nilitoa Machozi.
Sabina alitaka nijue kitu gani kilitokea.
Nilisimulia kila kitu na kumueleza kitu gani.
Mzee Kihamba akamwambia Monica basi ngoja tuendelee na safari nitakuelezea kila kitu. Basi safari ilianza tena huku mbwa wa mzee kihamba wakikimbia huku na kule. Walitembea tena umbali wa kutembea nusu saa ndipo kwa mbali Monica aliona vibanda vitatu vya nyumba za nyasi kuanzia chini mpaka juu.
Chakula kikuu cha mzee Kihamba kilikua Nyama za kuchoma. Kweli Mzee huyo alikuwa anaishi maisha ya ujima maana hata moto tu ulikuwa unatokana na kupekecha vijiti.
Ilikuwa yapata kama saa kumi na mbili jioni tayari mzee kihamba alikua amechoma nyama akamkaribisha Monica. Monica hakuwa na uchaguzi aliziparamia nyama hizo na kula.
Wale mbwa alikuwa wakija na kumnusa nusa Monica. Mzee Kihamba alimtoa wasi wasi.
Baada ya wiki tatu hivi Monica alikua ameanza kuzoea maisha ya porini. Na mzee Kihamba alikuwa namfundisha vitu tofauti tofauti.
Ilikuwa Jioni baada ya kutoka kuwinda Monica alimuomba mzee Kihamba aendelee kumueleza habari ya kuhusu Kusingiziwa kuua.
Endeelea kusoma hii hadithi ya kusisimua…..

 
Tusimulie basi maana hapa macho yamenitoka


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Hii ni stori ya Monica wa Maganzo Shinyanga namna gani alijiingiza katika biashara ile.

View attachment 105197Alizaliwa katika hospital ya Kolandoto mnamo mwaka 1983. Wazazi wake walikuwa ni wakulima. Baba yake mzee Magina alikuwa na wake wawili, Mama yake Monica akiwa mke wa pili.

Mzee Magina hakuwa na shida kihivyo maana pamoja kuwa mkulima alikuwa na biashara ndogo ndogo za kuuza vitu ndani ya mgodi wa mwadui. Kwahiyo Monica hakuwa na shida sana katika maisha yake tofauti na watu wengine kijijini pale.

Hakika ukimuna Monica huwezi amini kama kweli anaweza kujihusisha na biashara ile. Mtoto ameumbika mithili ya Sara wa kibinda, macho yake ya huwa, shingo imechongoka kama upanga wa mkata fito za kinyemberi. Sauti yake na mwendo wake hakika hutawenza kuamini. Sauti ya Monica ni ya vituo haina papara, kwa mara ya kwanza ukimuona utaridhia hakika mtoto huyu anafaa kuolewa.

Mnamo mwaka 1998 ndipo Monica alipojiunga na Sekondari ya Maswa Girls Sec School.
Huko ndiko sasa alipo anza kujifunza tabia tofauti tofauti.

Mwaka huo akiwa kidato cha kwanza alipata rafiki yake Mage mkazi wa sumbawanga. Walikuwa pamoja kila mmoja akielezea jinsi wanavyoishi nyumbani kwao.

Mage alimuomba Monica awaombe wazazi ili wakifunga shule waende Sumbawanga. Monica alikubali. Monica aliwaambia wazazi wake.

Fuatilia hii stori ya kusismua
Je Monica alipowaambia wazazi wake walisema na ilikuwaje usiikose kaa hapo hapo

MMMh leo ni shinyanga tuuu,
Kolandoto,Maganzo,Maswa Girls,bado nasubiria Mwandoya,Lalago,Sakasaka,Mwabusalu tupate story zao.....
 
Back
Top Bottom