Monica wa Maganzo

Monica wa Maganzo

Unapotaja MAGAZO unanikumbusha enzi zile za wanafunzi kusafiri kwa Warrant.....kutoka Nanjilinji hadi Shybush na Maganzo ndio Town yetu siku za mnada...... Palikuwa na majambazi wengi sana wakati ule....... mji wa madili.......
 
Ilipo ishia
Ilikuwa Jioni baada ya kutoka kuwinda Monica alimuomba mzee Kihamba aendelee kumueleza habari ya kuhusu Kusingiziwa kuua.

Part III inaendelea

Basi mzee Kihamba alimwambia Monica mwanangu, "Hujafa hujaumbika". Hebu naomba unikumbushe niliishia wapi kweli.

Monica alimkumbusha mzee Kihamba.

Mzee Kihamba aliendelea, Basi baada ya kueleza kila kitu Sabina alitokwa na machozi, baada ya kumtazama nikajikuta na mimi nina tokwa na machozi. Basi Sabina akaniambia atatafuta njia ya kuweza kuninasua na hii hali.

Sabina aliondoka, yaani huwezi amini kuanzia siku hiyo sikumuona tena Sabina hadi leo hii.
Monika aliuliza swali je ilikuwaje sasa hadi leo upo hapa?

Mzee Kihamba: Nakumbuka Mzee mmoja anaitwa mzee Iddi ndiye aliyeninasua kwenye hiyo hali.
Mjomba alipanga njama kubwa sana ili nifungwe maisha. Lakini mzee Idd aligundua kuwa mjomba yangu anania mbaya na mimi.

Alitafuta mbinu kabambe ili niweze kujinasua pale. Alimtuma kijana mmoja kwakweli simkumbuki akaniletea walaka uliokuwa umefungwa ndani. Nilipousoma ulikuwa unahusu mbinu itakayotumika kununasua na mtego huo. ndani yake alikuwa ameweka shilingi kumi ya noti kama nauli nikifanikiwa kujinasua.

Siku ikafika, yaani sitakaa niisahau siku hiyo. Uliitishwa mkutano wa wanakijiji wote. Ndipo mzee Idd akasimama kwenye mkutano akasema "Huyu kijana amefanya jambo la laana katika jamii yetu kwa kweli hatuwezi kumvumilia"

Mzee Idd alitoa maoni kwamba niende nikafungwe porini na huko laana ya kijiji itapotea. Ndipo wanakijiji wakakubaliana na kwamba hatakiwi mtu yeyote kufika nilikofungwa mpaka mda wa mwezi mmoja.

Basi linipelekwa kule nikafungwa huku ndani ya kaptula yangu nimeweka hiyo shilingi mia moja.
Nilifungwa kwenye mti ambao mzee Idd aliuchagua. Kwakua nilikuwa naelewa mbinu hiyo sikuwa na wasi wasi.

Ndani ya walaka wa mzee Idd alikuwa ameeleza kuwa kuna mahali atakuwa ameweka kisu.
Siku ile watu walikuwa kama wanyama, wanaimba nyimbo za kuondoa mikosi kwenye kijiji.
Kusema kweli nilijisikia kuwa hapa duniani sifai kuishi.

Wakati huo Monica alikuwa ameshaanza kupata usingizi, maana alikuwa amechoka sana kutokana na kazi ngumu za porini ambazo hajazizoea. Basi Mzee Kihamba kuona hivyo ilibidi akatishe mazungumzo na kumuacha Monica aweze kulala.

Kitu gani kitatokea kwa Mzee kihamba endelea kusoma hii stori ya kusisimua ....

 
Ilipoishia
Wakati huo Monica alikuwa ameshaanza kupata usingizi, maana alikuwa amechoka sana kutokana na kazi ngumu za porini ambazo hajazizoea. Basi Mzee Kihamba kuona hivyo ilibidi akatishe mazungumzo na kumuacha Monica aweze kulala.

PART III Inaendelea


Basi kila mmoja aliingia kwenye kibanda na kulala.

Siku hiyo ilikuwa ni siku ya jumatano usiku huo ulikuwa wa aina yake.

Mbwa walibweka walibweka sana, Monica alikuwa akijua ni kawaida tu ya mbwa kubweka. Lakini alikua akijiuliza kwanini sasa leo wabweke hivyo? Maana mbwa hao walifululiza kubweka.

Kunambwa mmoja alikuwa anaitwa Shekimambi, huyu alikuwa akiwaongoza mbwa wote alisikika kwa sauti ya ajabu akibweka tofauti na siku zingine. Mzee Kihamba alitoka kwenye kibanda chake na kuangalia kulikuwa na nini? Kuhamaki aliona Simba aliye fura akiwa amezungukwa na hao mbwa. Mzee Kihamba alikuwa na mkuki wenye mpini mfupi laki urefu wake ni kama futi tano na nusu hivi.

Basi mzee kihamba alinyata taratibu kuelekea eneo hilo. Wakati huo Monica alichungulia kwa mbali na kuona kila kitu kilichokuwa kinaendelea maana siku hiyo ilikuwa siku ya mbalamwezi. Mzee kihamba alinyata nyuma ya simba huyo, huku Monica akitetemeka maana hajawahi kumuona simba japo anawiki kadhaa hapo porini.

Taratibu taratibu mzee kihamba alijisogeza akanyanyua mkuki wake na kuudunga karibu na shingo ya huyo simba. Simba aliunguruma kwa sauti ya kutisha. Hapo hapo simba alianguachini, akawa anarusha rusha miguu yake.

Mzee Kihamba akawa anajaribu sasa kuuchomoa mkuku wake ili aweze kumchoma tena, bahati mbaya alitereza na kuangukia kwenye huo mkuki. Mkuki ukamchoma kifuani na ukatokeza upande wa pili. Mzee Kihamba alitulia hapo hapo hakuweza kufurukuta. Mbwa wote walikaa kimya hakuna hata mmoja aliye bweka.

Monica alishikwa na butwaa na kujiona kana kwamba yuko kwenye ndoto. Aliduwaa na kufa ganzi kwa muda kama wa dakika tano. Hakuelewa kabisa kama kweli hicho anacho kiona kinatokea mbele ya macho yake.

Monica hakujua sasa afanye nini hakuelewa hivi alie au akae kimya. Monica alijaribu kilia lakini alishindwa maana hakuna hata mmoja angeweza kumsikiliza. Na hapo walikuwepo mbwa tu.

Mpendwa msomaji endelea kufuatilia hii stori ya kusisimua. Ili ulewe Monica alianzaje hiyo biashara? na mpaka anapokuja kutoa hii stori....
 
Nakushauri, tafuta kazi hapo Global publishers, huwezi kukosa kazi, na utaishi vizuri tu hapa mjini! Mh, sorry, you sound like a Sukuma! Au we ndio Shigongo nini?
 
Ilipoishia
Monica hakujua sasa afanye nini hakuelewa hivi alie au akae kimya. Monica alijaribu kilia lakini alishindwa maana hakuna hata mmoja angeweza kumsikiliza. Na hapo walikuwepo mbwa tu.

PART IV Maisha ya Kishujaa Porini

Monica hakuweza kabisa kuelewa nikitu gani sasa kinafanya maisha yake yawe vile. Hakuamini kabisa macho yake kwa yale aliyokuwa anayaona.

Mbwa wote walikuwa kimya kabisa hakuna hata mmoja aliyeweza kubweka. Monica alibaki kwa mbali akimwangalia Mzee Kihamba akiwa ametulia tuli juu ya mgogo wa simba. Mapigo ya moyo yalikuwa juu.

Baadaye Monica akakumbuka ile ajari iliyo tokea, akafikiria sana ni kitu gani kilichomfanya yeye apone? Akapiga moyo konde na kusema moyoni hakika kile kilicho niponya kule na hapa kitaniponya.

Akaanza kupiga hatua za kunyata kuelekea kule Mzee kihamba alikojilaza. Kweli mda huo Monica hakuwa na uchaguzi. Ghafla zilimjia hisia na kummpa nguvu, kwa kweli hakujua hizo hisia zilitoka wapi, badala ya kunyata alianza kutmbea kwa hatua za kawaida tena kwa kujiamini.

Alipofika pale, aaaah tayari mzee Kihamba alikua amemtoka, maana hakuweza kabisa kuhema na joto la mwili wake lilianza kushuka. Simba alikuwa tayari ameshakufa maana ule mkuki ulimchoma kwenye moyo.

Monica alijaribu kumchomoa mzee Kihamba kwenye mkuki alishinndwa, maana Monica alikuwa ni binti tu mwenye kilo 45 hivi lakini mzee Kihamba lilikuwa ni pende la mtu zaidi ya kilo 75. Alijaribu kila njia kuweza kumtoa lakini alishindwa.

Monica hakuwa mwoga tena maana nguvu ya ajabu ilimjia na kujiona kuwa kama yeye ni shujaa. Hakuweza kuogopa tena kitu chochote.

Baadaye lilimjia wazo kwa nini asiende kuchukua kisu na kumkata kata vipande vipande mzee Kihamba ili aweze kumzika. Monica alifanya hivyo, alimkata kata vipande vipande mzee Kihamba na Kuvibeba vipande vipande vyake na kuviweka ndani ya kibanda alichokuwa analala Monica.

Monica alitapakaa damu, lakini yeye hakujari lolote.

Alivikusanya vipande vipande vya mwili wa mzee Kihamba na kivirundika kwenye kundi moja.
Baada ya hapo alirudi kwenye mzoga wa simba, alipofika pale alipika kelele "aaaaaaaaaaaa!".
Alianza kumrarua rarua yule simba kwa kutumia kisu alichokuwa nacho.

Monica alikuwa kama kichaa sasa, na alipata nguvu za ajabu.

Endelea kuisoma hii sitori uelewe ni kwanini Monica alijihusisha na biashara ile.....

 
Story nzuri ila unachelewa sana

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
daaah mbona bongo movies hawatengenezagi stori za hivi?
 
....me like this story
natamani nijue ni biashara ya namna gani hiyo
 
Story imetulia inanifanya niingia jf kila baada ya dakika kuangakia ka inaendelea
 
khaaa napenda hadithi lakini za hivi zinaniboa sana,niendee nisiendelee?nimalizie nisimalizie?endelea toleo lijalo, nilishaachana nazo tokea miaka ya 2000 mwanzoni nilipokuta meza yangu imejaa magazeti ya global publisher.
 
MMMh leo ni shinyanga tuuu,
Kolandoto,Maganzo,Maswa Girls,bado nasubiria Mwandoya,Lalago,Sakasaka,Mwabusalu tupate story zao.....
...aiseeh!! monaco hii kitu Lalago umenikumbusha nikiwa Shybush aisee lilipigwa debe tukawaalika watoto toka Lalago(lagos) Mkuu sitasahau....

...niendelee ni sisiendelee?
 
Ilipo ishia
Monica alikuwa kama kichaa sasa, na alipata nguvu za ajabu.

PART IV Maisha ya Kishujaa Porini Inaendelea....

Monica alibadilika kabisa na kuonekana kama mnyama. Hakuwa muoga tena maana vitendo alivyovifanya sasa ni vya ajabu mwanadamu wa kawaida hawezi kuvifanya. Sauti yake nyororo ya kirembo ilibadilika na kuwa sauti nzito. Monica hakuwa na akili tena za binadamu wa kawaida.

Baada ya kurarua rarua mzoga wa simba, Monica aliishiwa nguvu na kujikuta anaanguka chini. Macho yake hayakuweza kuona vizuri tena. Japo kuwa kulikuwepo na mwanga wa mwezi giza nene lilitanda kwenye macho yake. Alishindwa kabisa kufanya chochote.

Baada kama dakika tano hivi, aliona viumbe mithili ya mwanadamu vikitokea kwa mbali. Monica alijaribu kunyanyuka hakuweza kabisa maana nguvu zilimwishia. Viumbe wale walizidi kumkaribia. Akili za Monica zilikuwa zinafanya kazi lakini viungo vyake vya mwili havikuweza kabisa kufanya kazi.

Viumbe vile vilikuwa na miguu miwili kama ya mwanadamu, mikono yake ilikuwa mirefu sana, uso wake ulifanana kabisa na punda maana mdomo wake ulichongoka. Cha ajabu viumbe hao walikuwa na manyoya ya rangi tofauti tofauti. Lakini kwenye shingo yao walikuwa na rangi ya kijani. Urefu wao ulikuwa kama futi 12 mpaka 15. Alikuwa wamejipanga mistari miwili kama askari waendao vitani. kadri walivyo karibia aliwaona dhahili kuwa wakotofauti na mwanadamu maana walikuwa na mapembe 6 kwenye vichwa vyao.

Wanyama hao walikuwa wanakuja kwa kasi ya ajabu. Walionekana wenye hasira sana maana nyuso zao zilikunjamana. Alisikia sauti kutoka kwa mmoja wao "Uliokoka wakati ule leo tumejiandaa na hakuna wa kukusaidia" Monica hakuwa na nguvu, hakuweza kabisa kujisogeza, kinywa chake kilikuwa kizito, hakuweza kuongea chochote.


Wanyama wale walifika sehemu alipokuwa Monica, wakamzunguka wote kwa pamoja wakapiga kelele "Wuuuuuuuuuuuuuuuu Woooooooooo tutakuchukua tutakuchukua".

Baada ya hapo walianza kuimba wimbo:-

Kamwana, kamwana tukachukue tukapeleke kwa mtemi x2
kataweza kuwa ka mwali kamwali ka mwana ka mtemi x2
kamwana, kamwana tukachukue tukapeleke kwa mtemi x2


Wakati wanyama hao wakiendelea kuimba wakiwa wamemzunguka Monica na Monica hawezi kufanya kitu chochote ulitokea upepo mkubwa, ngurumo za radi zilisikika, mwezi ulipotelea kwenye mawingu.

Monica alipoteza fahamu na hakuelewa kabisa kitugani kiliendelea baada ya hapo.


Mbwa walisikika wakibweka, ndege wakiimba. Mwanga wajua wa asubuhi ndio ulimuamsha Monica.


Mpenzi msomaji hebu endelea kusoma hii stori ya kusisimua usiondoke hapa JF.......



 
Duh:! Leo katuchinjia baharin.. tunaomba utupe hata siku ambazo utakuwa unaendelea jamn cz huku tunakuwa vichaa wa jf kwa kungojea kwa hamu
 
Kaa sasa mkao wa kusikilza nitaanza nitaanza kuitoa ndefu kias fulani.
Si unajua tena Jpili siku ya kumwabudu Mungu.
 
Ilipoishia
Mbwa walisikika wakibweka, ndege wakiimba. Mwanga wajua wa asubuhi ndio ulimuamsha Monica.

PART IV Maisha ya Kishujaa Porini Inaendelea....

Alipo fungua macho aliona watu watatu wamekaa pembeni wakiwa na bunduki mkononi.
Alipotazama kwa makini akagundua kuwa mmoja wao alikuwa mwanamke. Alipotazama kuliakwake aliona mzoga wa simba ukiwa umeraruriwa raruriwa. Hakuelewa kabisa kitu gani kilitokea, na wale viumbe ilikuwa kitu gani. Je ilikuwa ndoto au ilikuwa njozi?

Kwa mbali aliona gari limepaki na kuna watu wakiwa wanazunguka zunguka kwenye gari hilo.
Yule wa kike akamsogelea akiwa amekunja uso. Akamshika na kumyayua.

Monica wakati huo alikuwa amejiamini sana. Akawauliza nyie ni akina nani? Yule mwanamke akajibu utaelewa tu subiri.

Yule mwanamke akasema:
Sikiliza biti mrembo kwa makini, kuanzia sasa hivi ukochini ya himaya yetu. Mashariti yafuatazo yanatakiwa uyaweke kichwani.

Shariti la kwanza: Hutakiwi kuuliza maswali zaidi ya matatu kwa siku.
Shariti la pili: Unatakiwa kujibu swali unaloulizwa.
Shariti la tatu: Unatakiwa kufanya unachoamriwa kufanya.
Shariti la nne: Ratiba zote utapangiwa.
Shariti la tano: Unatakiwa kumaliza kula ndani ya dakika tano.
Shariti la sita: Unatakiwa uwe mwepesi wa kuelewa.

Hayo ni mashariti ya mwanzo uyaweke kichwani. Ukikiuka shariti lolote adhabu kali utapata.
Sasa elekea kwenye gari ile.
"Huku akionesha kwa kidole"

Monica akasema: mpaka mnieleze nyie ni akina nani? mmetoka wapi? na mnafanya nini hapa?

Yule mwanamke akasema kwa sauti ya ukali: Umekiuka shariti la kwanza, Umekiuka shariti la tatu na umekiuka shariti la sita. Askari

Wale wawili wakaja wakamkamata Monica na kufunga kamba miguuni na mikonono. Wakaanza kumpiga ngumi, mateke. Monica alisikia maumivu makali maana ngumi walizo mpiga zilikuwa za uhakika. Mmoja akamtandika ngumi ya pua, ndipo Monica akaanza kutokwa na damu puani hapo hapo wakaacha kumpika.

Monica alikuwa amepigwa vibaya mwili wake ulitoa nundu kila sehemu. Hebu fikiria jamani: "Yaani wanaume walioshiba wanamchangia kumpiga mtoto mzuri wakike!!"

Walimfungulia na kumuamrisha aelekee kwenye gari. Monica hakuwa na uchaguzi alitemebea kwa kuchechemea kuelekea kwenye gari hilo.

Gari lilikuwa limezibwa hauwezi kuona nje. Lilikuwa na matundu madogo madogo tu ya kupitishia hewa.

Alipoingia ndani ya gari aliwakuta watu wengine wakiwa ndani ya lile gari. Wakiwa wamekaa nguo zao zimechakaa.

Yule mwanamke akingia nyuma ya gari kule walipokuwa akina Monica. Gari lilianza kuondoka.
Yule mwanamke akaanza kusema:
Mimi ninaitwa Katarina kwa wale wasionifahamu ni kiongozi wa kikundi namba tatu cha A13.
Kuhusu A13 mtajulishwa baada ya kufika tunakoelekea. Kwa wale msiofahamu wapi tunaelekea, kwa kifupi kabisa tunaelekea Goma. Kwa faida ya wale wasiofahamu Goma iko wapi, Goma ipo nchini Kongo. Kwa baadhi yenu msiojua Kongo ikowapi ni magharibi ya nchi hii tunayotoka sasa.
Mtakuwa kwenye mafunzo ya kijeshi kwa mda wa miezi sita ili kuipigania A13.


Wakati huo Monica alikuwa ametulia akimsikiliza Katarina.

Katarina ni mwanamke mrefu mwenye shingo ya twiga, pua yake imechongoka kidogo na anaumbo la namba nane. Nimwamke mwenye mazoezi, ukimwangalia tu hakika utatamani japo umkumbatie.

Endelea kusoma hii stori ni nzrui mno......

 
Back
Top Bottom