Monica wa Maganzo

Monica wa Maganzo

Ilipoishia
Katarina ni mwanamke mrefu mwenye shingo ya twiga, pua yake imechongoka kidogo na anaumbo la namba nane. Nimwamke mwenye mazoezi, ukimwangalia tu hakika utatamani japo umkumbatie.


PART V Mafunzo ya Kijeshi


Monica alikuwa akiwaza sana sasa "Hivi kweli ndoto yangu yakusoma ndio imezimika hivyo!!, Na wazazi wangu sijui sasa wanafikiria nini" Monica alipiga moyo konde na kujipa matumaini siku moja ataonana na wazazi wake na kurudia maisha yenye furaha.

Hakuna mtu aliye kuwa anaongea wakati huo, Katarina alikuwa yuko kimya lakini macho yake yalikuwa yakipepesa pepesa.

Baada ya muda wa masaa 14 walikuwa tayari wamekaribia kwenye kambi No3 ya A13.

Walipofika walishuka huku Monica akichechemea. Walipewa chakula pamoja na wenzake.
Kuseakweli chakula kilikuwa kizuri chenye afya.

Baada ya kumaliza kula kilammoja alipewa mavazi. Walipewa Sare, nguo zenye langi ya kijivu aina ya kadeti (Suruali na shati).

Eneo lile nilikua na askari kila mmoja alikuwa na kazi anafanya. Wengine walionekana wakikimbia kimbia huku na kule. Magari ya kivita yalikuwa yamepaki eneo fulani. Vifaru vya aina tofauti tofauti vilionekana pale.

Monica aliona kama ndoto vile. Maana vitu hivyo alikuwa anaviona kwenye video tu. Sasa hapa anaona kwa macho yake.

Walielekezwa sehemu ya kuoga na kuamriwa baada ya kuoga wabadilishe nguo na wavae zile sare. Walifanya hivyo.

Monica alipendeza sana.

Katarina aliwaita nakuanza kuwaeleza:
Kesho mtaandikishwa kwenye daftari majina yenu. Mtakaa siku tatu baada ya hapo mtaondoka eneo hili na kupelekwa sehemu ya mazoezi.

Walielekezwa sehemu ya kulala.

Kusema kweli eneo lile lilikuwa zuri na walihudumiwa vizuri sana.

Katika kundi hilo la akina Monica wakuwemo wasichana 5 aikiwemo na Monica. walielekezwa sehemu ya kulala wanawake. Baada ya kufika kula walitambulishana majina yao.
Monica, Alice, Tekra, Sofia na Vivian.

Monica alieleza yeye anatoka Maganzo. Hawakuelewa Maganzo iko wapi maana wote hao walikuwa sio watanzania. Monica aliwashangaa sana yaani hawajui maganzo!!.

Aliwaeleza maganzo iko wapi na wakaelewa.
Alice alikuwa akiongea kiswahili kibovu kibovu alisema yeye anatokea Somalia
Tekra yeye alisema anatokea Sudani.
Sofia aliongea kiswahili cha kikenya akasema yeye ametokea machakosi
Vivian akasema yeye ametokea Ethiopia.

Walitambulishana na kujuana zaidi.
Baada ya muda kama wa dakika 30 hivi askari akapita na kuwaambia wasiongee walale. walikaa kimya na hawakuongea tena.

Mpendwa msomaji wa JF unaionaje hii stori. Endelea kuisoma na utashangaa namna Monica alivyo jifunza biashara ile.......

 
Ilipoishia
Baada ya muda kama wa dakika 30 hivi askari akapita na kuwaambia wasiongee walale. walikaa kimya na hawakuongea tena.

PART V Mafunzo ya Kijeshi inaendelea....


Sauti zilisikika za watu wakiimba nyimbo mbali mbali. Tayari askari walikuwa wameamka kwenye hiyo kambi walikuwa wakiimba nyimbo huku wakikimbia mchakamchaka.

Ilikuwa yapata saa 11 alfajiri askari mmoja alikuja kuwaamsha akina Monica.

Tayari wale wakiume walikuwa wameamka.

Katarina alikuwa yupo kwenye kibanda amekaa, juu ya meza kulikuwa na bunduki na kitabu cheusi.
Upande mwingine kulikuwa na moto unawaka na kwenye moto kulikuwa na vyuma. Monica na wenzake waliungana na wale wa kiume waliokuwa wanne na kuelekea kwenye kibanda alikokuwa amekaa Katarina.

Katarina: Leo kunazoezi la kuwaandikisha na kuwawekea alama. Alama mtakazopewa ni utabulisho wenu. Mtawekewa alama kwenye mabega. Baada ya kuandikisha jina lako unaelekea kwenye kimbanda kile. alionesha kwa kidole.

Akasema wewe njoo. kijana wa kiume alisogea
Taja jina lako na lababa yako Katarina alisema. Yule kijana akasema: Katongo Nzila
Katarina akaandika jina lake ndani ya kile kitabu cheusi. Akaelekea sehemu ya kuwekewa alama.

Yaani ilikuwa sio mchezo vyuma vilikuwa na namba na vimewekwa kwenye moto vimepata moto na vimekuwa vyekundu. Kilichukuliwa chuma namba 5115 na kikasimikwa kwenye bega la katongo. Katongo alilia sana alimwagiwa dawa flani kwenye bega ili kukausha kidonda.

Huku kikiendelea litendo cha kuandikisha na kuwekewa alama.

Bakari Said aliwekewa namba 5114
Paul Katesha aliwekewa Namba 5115
Deo David aliwekewa 5116
Tekra aliwekewa 5117
Sofia aliwekewa 5118
Alice aliwekewa 5119
Monica aliwekewa 5120
Vivian aliwekewa 5121

Walipata maumivu makali sana. Vidonda viliuma sana.

Katarina akawaita na kuwaeleza mambo mengi kuhusu mafunzo watayopata.

Tutaanza na mafunzo ya ukakamavu na
utii ambayo ni ya msingi kabisa yatachukua mwezi mmoja.

Baada yahapo tutaendelea na mafunzo ya ukakamavu pamoja na kutumia silaha mafunzo haya pia yatachuku mwezi mmoja.

Miezi miwili mtakuwa mnafundishwa saikolojia na kutunza siri .

Miezi miwili mtafundishwa Binu za kupeleleza na Kuteka.


Baada ya miezi hiyo sita tutakuwa tumewajua na kila mmoja atawekwa kwenye kitengo fulani.


Baada ya maelezo hayo waliondoka nakuelekea aliko elekezwa. Nyuso zao zilijaa majonzi baada ya kuwekewa zile alama.


Baada ya siku tatu alichukuliwa na gari na kupelekwa porini. Tayari vidonda vya alama vilikuwa vimekauka. Siku hiyo ilikuwa ngumu sana maana walifanya mazoezi ambayo hawajawahi kuyafanya.

Walinyolewa nywele zao na kubaki na kipara. Japo kuwa walikuwa na kipara sura nzuri ya Monica iliendelea kuonekana.

Walifundishwa mazoezi ya mwili kuwa mwepesi, kareti, kombati-kareti, Kufuu-kareti, mieleka na kila aina ya kujihami bila silaha.

Monica alisahau kabisa maswala ya kusoma tena.
Viviani alikuwa ni msichana mrefu na mwenye mikogo alikuwa mwepesi sana wa kuelewa.
Lakini Tekra alikuwa mgumu kuelewa akili zake hazikuwa zina fanya kazi haraka.
Monica alikuwa mwepesi wa kuruka na mweili wake jinsi ulivyokuwa umekaa aliyamudu mafunzo yale kisawa sawa.

Wengine alikuwa wa kawaida tu. Vivian na Monica alianza kuwa marafiki na isitoshe Vivian ngozi yake ni yeupe kiasi fulani.

Hakika wote wawili walikuwa ni wasichana warembo. Kila baada ya mazoezi walikaa pamoja.

Mwezi wa kwanza ulikatika kama kufumba na kufumbua tu.

Endelea kusoma hii stori nzuri sana....



 
ilipo ishia Mwezi wa kwanza ulikatika kama kufumba na kufumbua tu.

PART V Mafunzo ya Kijeshi inaendelea....


Mafunzo ya kutumi silaha yalianza kwa kasi. Walianza kuzoea na kufahamiana zaidi.
Walifundishwa namna ya kufungua na kufunga bunduki. Walifundishwa aina mbali mbali za bunduki na milio yake.

Walifundishwa jisi ya kutumia silahazingine kama visu, kamba, fimbo na kila aina ya zana.
Mafunzo yalipamba moto na pale sasa Monica na Vivian walikuwa kama vichaa maana waliyapenda mafunzo hayo na kuyamudu kisawa sawa.

Sofia alichukia sana jinsi Viviani na Monica walivyo na urafiki. Hakupenda hata kidogo wawe karibu.
Lakini hakuwa na la kufanya alikaa kimya tu.

Walifundishwa kutega na kutegua mabomu. Vilevile walijifunza namna ya kujificha na kuchimba mahandaki.

Walifundishwa mbinu za kutembea na kuficha silaha ndogo ndogo sehemu yenye ulinzi.
Mafunzo hayo yaliwafanya waive kisawa sawa hukuwaki fundishwa mashariti yote.

Bwana Java ambaye ni mkuu wa A13 alikuja kutembelea mafunzo hayo alifurahishwa sana na jinsi vijana hao wanavyo mudu.

Java ni mwanajeshi mstafu nchini Uholanzi. Kwa sasa anakisimamia kikundi hicho cha A13 baada ya aliyekuwa msimazi kufariki mwaka jana kwenye ajari ya ndege iliyo tokea marekani.
Pia ni msimamizi wa makampuni mbali mbali katika nchi tofauti tofauti.

Baada ya kifo cha aliyekuwa Mmiliki wa A13 (ambaye ni baba yao) yeye na mdogo wake Android wamekuwa na kutofautiana hapa na pale ni kwa sababu ya kampuni yao ya utengenezaji wa Magari nchini Ujerumani.

Android alikuwa akidai wagawane mali na waifunge hiyo kampuni lakini Java alisimamia msisitizo kwamba kampuni hiyo haiwezi kufungwa ni kuiboresha tu na kuipa ufanisi zaidi wa kubuni magari mazuri ya kisasa.

Adroid amekuwa akihofia sana kutokana na magari yao kutonunuliwa maana nchi za asia zimekuwa zikiuza sana magari. Hususani nchi ya china ndio imekuwa ikimkatisha tamaa.

Baada ya mazoezi vijana wote walitabulishwa kwa bwana Java.
Java aliwaeleza kuwa amekuwa akisikia habari zao kuwa wanafanya mazoezi vizuri. Na kikundi cha ni bora kabisa tofauti na vikundi vingine vilivyo wahi kufundishwa hapo.

Kikundi chenu kimekuwa kina elewa haraka mafunzo haya Java alisema. Baada ya mafunzo ya miezi sita baadhi yenu mtachukuliwa na kwenda kufanya mafunzo ya ngazi ya juu zaidi nchini Urusi Java aliongea. Alisisitiza zaidi kuwa na nidhamu na kusikiliza kwa makini kile wanacho fundishwa.

Mafunzo ya kutumia silaha yalifanyika vizuri na mwezi wapili uliisha haraka sana.

Endelea usiache kuisoma hii....



 
Sasa wazazi wa monica walishakaa matanga au wanajua mtot wao yuko wapi Annael
 
Last edited by a moderator:
kwanini unachukua muda mrefu kuiendeleza pale ilipoishia.........?
 
Waimuliaji wa humu nao

Sasa annael umeenda wapi, mbona kimya
 
Monaco usisahau na Mwanhuzi, Mwambegwa, Nkoma, Sapa, Bulyashi, Bukundi, Mwagwira, etc. Hahahahaha
MMMh leo ni shinyanga tuuu,
Kolandoto,Maganzo,Maswa Girls,bado nasubiria Mwandoya,Lalago,Sakasaka,Mwabusalu tupate story zao.....
 
Ilipo ishia.
Monica: Niliona watu wenye nguo nyeupe wakitokea pande nne za dunia na mmoja wao akasema "muacheni kwanza huyu ngoja wengine wote tuwachukue" Nilijaribu kuongea kuwa uliza nyie ni nani lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sikuweza hata kuongea, akilini ninawaza cha kusema lakini siwezi.



Part II inaendelea....
Monica: Nikasikia sauti mmoja akiita "Gabriel, Gabriel" mmoja wa hao watu akageuka, hakika nilishindwa kuiona vizuri sura yake, maana uso wake ulikuwa unag'aa mithili ya miale ya jua.
Yule aliyeitwa kwajina hilo alijibu akisema "Yuhiel mshike mkono mlete hapa"

Ndipo Monica alipo poteza fahamu na hakuelewa tena kitu gani kinaendelea.

Sauti za ndege akiimba zilisikika kwa mbali, wengine ni kama miluzi ya watu wanaofukuza mbwa mwizi, zingine kama kuku akitafuta sehemu ya kutagia. Kila aina ya sauti zilisikika.

Pale ndipo nilipo pata fahamu na kuona moshi mnene ukitokea upande wa kulia kwangu. Sikuelewa huo moshi ni kwaajili ya nini Monica alisema.

Hakuna mtu hata mmoja aliye baki isipokuwa Monica pekee yake maana basi liliteketea lote kwa moto. Hakuna mabaki yoyote yaliyobaki.

Ndipo Monica akaanza kulia kwa sauti ya huzuni akiita Mage, Mage, Mage uko wapi. Kila akiita mwangi ulisikika ukirundia maneno yake. Hakuna hata chembe ya kitu kilibaki pale.

Ilikuwa ni kama saa 12 alfajiri ndipo alipogundua kumbe amebaki peke yake. Majeraha madogo madogo kwenye mguu wake wa kushoto na mgongoni aliyapata. Kusema kweli Monica hakuumia.
Hakuelewa ni kitu gani kilichomfanya achomoke ndani ya gari pasipo yeye kuumia.

Ilikuwa kama umbali wa mita 20 kutoka barabarani, akiendelea kulia hakuna mtu yeyote aliye pita barabarani. Macho yake yalivimba na kuwa mekundu mithili ya mtu aliyepakwa pilipili kwenye macho. Mdomo wake ulikauka na pua yake kujaa makamasi kama mama aliyepotelewa na mwanae mpenzi.

Mda huo Monica alijipa matumaini huenda Mage yupo sehemu na kuendelea kuita kwa sauti. Mpaka pale sauti yake ilipokauka na kushindwa kabisa kuongea.

Njaa nayo ilianza kunyemelea tumbo lake, kichwa chake kilikuwa kizito kana kwamba kabeba mzinga wa maboksi ya chaki. Alikuwa akisikia sauti ndani ya kicha ikitwanga "kiko! kiko! kiko! kiko!" Mpigo yake ya moyo yakipiga haraka haraka.

Japo kuwa Monica alikuwa kwenye majonzi sura yake zuri ya kiafrika haikupotea. kadri alivyozidi kufumba macho na kufunga mdomo mashimo yalijitokeza kwenye mashavu yake mithili ya visima juu ya mawe ya engaruka.

Monica alichoka, hakuwa na wakumsaidia wala kuongea naye tu. Monica alizoa kusikia sauti za watu leo hii hakuna hata mmoja wa kuongea naye. Monica aliishiwa nguvu, ndipo usingizi mzito ukampitia

Je usingizi huo ulikuwaje endelea kufuatilia




kaka, kama umetoa kitabu tafadhali tujulishe tuje tununue, hadithi yako ni nzuri sana, hii subiri subiri ngumu sana hii.
 
Najuutaa kuisoma na mimi nshaingia kwenye iyo waiting list yako...

Sent from my BlackBerry 9810 using JamiiForums
 
tatizo wasomaji hawampi msimuliaji LIKE kama congratulation, tunasomaaaa tu bila pongezi
 
Back
Top Bottom