Ilipoishia
Mage alimuomba Monica awaombe wazazi ili wakifunga shule waende Sumbawanga. Monica alikubali. Monica aliwaambia wazazi wake.
PART II
Usiku wa Kuhangaika
Mzee Magina alikataa kata kata sababu tu kwamba Monica ni mtoto pekee wa kike lakini mama yake Monica alimbembeleza na kumsihi njinsi Monica alivyokuwa akielezea kuhusu wazazi wake Mage.
Mke wa pili wa Mzee Magina alijulikana kwa jina Kagole lakini jina lake halisi alikuwa akiitwa Nyandalo Ni mwanamke aliyejaliwa kiwa na ushawishi wa hali ya juu. Mzee Magina alikuwa anapenda sana kumwita Kogole. Yaani alikuwa anatamka kwa Lugha ya kisukuma Kagole wane
Ikiwa na maana ya Kagole wangu.
Mzee Magina alikubali na kuhakikisha kuwa anampatia vitu vyote vya muhimu ikiwamo vitu vya kimila.
Siku ya kufunga shule ikafika Monica alisema anakumbuka kabisa siku hiyo ilikuwa siku ya ijumaa. Mimi na Mage tulifungasha mizigo yetu na kwenda kuwaaga wazazi wangu Maganzo.
Siku ya jumamosi Mzee Magina aliwasindikiza stend ya mabasi yanayotoka Mwanza kuelekea Tabora.
Walipo panda basi tu, ndipo Mage alianza kumweleza vitu vilivyomfanya Mage ashangae na kutamani wafike haraka aweze kujionea kwa macho yake. Stori zilizidi kupamba moto huku Mage akiwa ndiye kinara wa kutoa stori.
Ilipofika mida ya saa 10 za jioni tayari walikuwa wameshapita Tabora. Na msitu mnene ukawa unawaita, msitu ule ulikuwa namiti mikubwa mikubwa na kufanya jua lisionekane.
Nyimbo za ndege na sauti za wanyama mbali mbali zilitanda kwenye msitu huo, na istoshe mda huo njio ndio inaingia. Ghafla kulisikika mlio mkumbwa na kishindo wa "Pwaaaaaauuuu!!!" na basi walilokuwa wakisafilia "Roho ya paka" likayumba kulia kushoto kulia kushoto baada ya hapo likaacha njia.
Kila mmoja ndani ya basi alikuwa akimuomba Mungu wake. Basi lilipoteza mwelekeo na kujita linaparamia miti, likagonga mti mmoja na kumbiringika.
Monica: Niliona watu wenye nguo nyeupe wakitokea pande nne za dunia na mmoja wao akasema "muacheni kwanza huyu ngoja wengine wote tuwachukue" Nilijaribu kuongea kuwa uliza nyie ni nani lakini mdomo wangu ulikuwa mzito sikuweza hata kuongea, akilini ninawaza cha kusema lakini siwezi.
Baada ya hapo kitu gani kilitoke endelea kufuatilia