Mo endelea kuiga iga bidhaa za watu

Mo endelea kuiga iga bidhaa za watu

Niliwai ongelea ili swala la uyu jamaa mfano wa Azam ukwaju na Mo ukwaju sasa uncle bakhresa hajaamua fanya ivyo maana akisema aingie kwenye hii vita basi Mo atalambwa pesa mingi


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kuna mo ukwaju?
 
Wabongo ndo tabia zao. Kuna mahari nilifungua kiduka cha m.pasa maeneo ya tegeta A. Biashara ikawa inaenda fresh tu. Baada ya mda nilipopanga frem nikapewa notis nikapata. Frem nyumba ya pili. Cha kushangaza zikaibuka m.pesa kama 4 na Mimi wa 5.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahah wabongo wengi si wathubutu. Wanangojeaga mtu afanye kitu kikiwa successful wanaamua kushindana nae kwa kumuiga typically.
 
Hivi hili jambo linawahusu hawa jamaa tu au hadi kwenye taasisi nyingine.

Mfano.. kwenye benk

Kampuni za simu

Kampuni za bima.

Kampuni za uzalishaji nondo,bati,misumali n.k
Mifano ni mingi.

You own the formula not the product..

Jaribu kulinganisha bidhaa na huduma zao, kama case ni kuigana basi hawa jamaa kesi zingekuwa nyingi.

Si dhani kama Bakharesa angekaa kimya kama kungekuwa na hizo shida sisi walaji tunaotaka kuzianzisha.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hakuna sheria inayobana kuhusu kuiga product. Watu hawajaelewa

Kesi hizi mara nyingi zinahusu trademark/ tradename

Mfano hiyo cleensoft na kleesoft

METL walishashtakiwa kukopi logo ya maji MASAFI


Mihan gas alishtakiwa na O gas kuhusu rangi ya njano ya mitungi ya gesi na alishindwa.

Bakhresa mwenyewe(Azam) alishafanya uhuni Burundi/Rwanda aliwahi kwenda kusajili jina la Azania kama lake ili kumzuia Mikoani Traders(Azania) asilitumie katika hizo nchi au aingie kwa jina jipya( kwakua yeye SSB kalisajili ila halitumii) na kesi bado iko mahakamani

Ila ukiachana na hayo Bakhresa ana bonge la timu la ubunifu. Bongo nzima tukasome
 
Mo anajina so chochote atakachoona unauza akiweka jina na mo mwanzoni watu watanunua tu kwasababu tayari ana reputation nzuri kwenye biashara! Aachane na hiyo cleansoft aite hata Mo usafi
 
Hivi hili jambo linawahusu hawa jamaa tu au hadi kwenye taasisi nyingine.

Mfano.. kwenye benk

Kampuni za simu

Kampuni za bima.

Kampuni za uzalishaji nondo,bati,misumali n.k
Mifano ni mingi.

You own the formula not the product..

Jaribu kulinganisha bidhaa na huduma zao, kama case ni kuigana basi hawa jamaa kesi zingekuwa nyingi.

Si dhani kama Bakharesa angekaa kimya kama kungekuwa na hizo shida sisi walaji tunaotaka kuzianzisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ndio unayechanganya mambo! Kuna kuiga huduma kama kwenye sekta ya bima, mawasiliano, na ma bank! Hiyo haina shida kwenye biashara kwani huibi haki ya mtu, kwani mpesa, ni tofauti na tigo pesa, huwezi lalamika, sasa huyu mo yeye anaenda mbalii zaidi hadi kwenye majina, na kuweka utofauti mdogo sana, na kufananisha hata vifungashio!! Mfano hiyo sabuni ya kleesoft yeye akaleta yake cleansoft!! Huo si uhuni? Ndio maana ameamliwa hiyo bidhaa iharibiwe!! Kwenye matangazo mfano ya radio mteja ataweza kutofautisha kati ya kleesoft na cleansoft? Huko kwingine mfano azam energy, naye mo energy, haina shida kwani ni majina mawili tofauti, na ndio maana hata bakhresa aliwashinda coca cola kipindi kile anaanzisha kinywaji chake cha azam cola kwani walitaka azuiwe kutumia neno COLA!!!
 
Back
Top Bottom