Mnyika tafadhali soma hii


Asante mkuu
 
Jambo la ajabu mtu anakuja na allegation zake then yeye anategemea wana jamvi wampatie ukweli hii inawezekana vipi?
La msingi njoo na concrete evidence then issue itakuwa na mashiko
 
Kwa kweli ningejisikia fahari kama JJ angekuja mwenyewe kama Zitto anavyofanyaga na HKigwangala alivyofanya hawa ndio mashujaa na wanaonekana wanachokisema tunaangalia kupembua zipi pumba na yapi.......... PEOPLE??????????????
 
Asante, ndiyo nimeisoma; kwa wale wageni ambao hatukuwa pamoja toka BCS/TEF/JF nk muelewe tu kwamba nina kawaida ya kujibu masuala mbalimbali yanayonihusu, kukihusu chama au kulihusu taifa katika mtandao huu ambao mimi ni mwanachama tangu kuanzishwa kwake. Hata hivyo, kwa sasa nipo nje ya nchi, na nilipo sina fursa ya kuwa kwenye mtandao.

Naomba nijibu kwa ujumla masuala yaliyojitokeza katika majadiliano haya kama ifuatavyo:

Mosi; Sihusiki na vibali vya utupaji taka ngumu pale mabwawa saba Mabibo; hata hivyo wiki chache zilizopita nilipata taarifa kuwa kuna watu walianza kumwaga uchafu. Nilifuatilia kwa niaba ya wananchi na kuzuia. Kama hali hiyo imejirudia tena nitafurahi kujulishwa; pamoja na kuwa si wajibu wangu kutoa vibali wala kuzuia ni jukumu langu kuwawakilisha wananchi kama ilivyo kwa mwenyekiti wa mtaa na diwani wa eneo husika. Sakata la mabwawa saba ni la miaka mingi na kuna wakati lilikuwa likishughulikiwa na wanasheria wa mazingira.

Pili; sijawahi kupewa rushwa; hata ya shilingi moja na yoyote katika jambo lolote. Kwa wanaonifahamu vizuri wanaweza kuzungumza kuhusu maadili yangu katika masuala kukataa ufisadi kabla sijawa mbunge na hata sasa.

Tatu; sina akaunti yoyote yenye milioni 280 kama ilivyodaiwa; toka nizaliwe sijawahi kukopa mkopo binafsi hata wa senti moja katika benki yoyote kwa ajili ya chochote. Pamoja na kuwa nina fursa ya kukopa mamilioni kama mbunge natathmini sana kiwango cha mkopo Vs Utumishi wangu kama mbunge kwa kuwa collateral ya mbunge katika mkopo wake ni utumishi wake na makato yake ni katika mshahara wake na posho zake. Maamuzi yoyote nitayoyafanya katika jambo kama hili lazima yazingatie kuhakikisha kwamba naendelea kutimiza wajibu wangu kwa ufanisi katika utumishi wa umma. Kwa sasa mkazo katika kazi zangu ni kuweka msingi wa utendaji jimboni na bungeni; masuala mengine yana wakati wake. Naelewa ni jambo la kawaida kukopa na ni ishara ya kuwa tayari kuchukua risk na kusonga mbele kwa haraka-lakini napenda kutenganisha kati ya utumishi wangu wa kila siku katika nafasi zangu mbalimbali na biashara.

Kwa yoyote mwenye ushahidi wa kupingana na majibu yangu hayo matatu namkaribisha kuutoa. Nawatakia heri; nitakuwa nje ya mtandao wa internet mpaka baada ya siku kadhaa.

JJ
 
MIMI NI CDM,SIPINGI ILA NAOMBA UTHIBITISHO KUWA ALITETEMEKA SIKU ALIYOPEWA CHEQ NA KUWEKEA MIL280 BENK,NAJUA NAO NI BINADAM:frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty::frusty:
 

Amechukua hela toka kwa magari ya maji taka ili....then yeye peke yake kaamua zoezi la kumwaga liendelee!!!!!
Tumieni akili bwana, hizo propaganda zenu siku hizi hata watoto wanazishitukia!! nimeona hata clouds tv leo ikiendelea kumipiga propaganda mnyioka kuhusu hilo.....
Badilikeni , hiyo mbinu mbona haiwa saidii watu wa CCM na ndiyo kwanza mnazidi kuchukiwa?
 
Kama kuna mtu anafahamu kilichosemwa kwa ukamilifu wake kwenye kipindi cha Daladala kilichotajwa pamoja na Clouds TV tafadhali naomba anijulishe kupitia johnmnyika@gmail.com au aandike hapa ili nikirejea Tanzania niweze kuchukua hatua. Siku njema

JJ
 
Kipindi cha daladala hakirushwi na ITV bali ni TBC1.Kwa hiyo hata habari yako ni ya uongo kuanzia taarifa ya tv ..husika
 
Nadhani waliotaka kusikia maneno ya mbunge kutoka kwenye vidole yake vilivoandika ujumbe sasa wana amani. Kama kuna tuhuma zaidi mbunge kasema aelezwe hapa jamvini au mtafute kwa email yake. Hawa ndo wabunge wa kuigwa,ukiongeza H.Kigwangala,DrSlaa,regia ,zitto na wengineo wanaotupa majibu moja kwa moja. Asante kwa kuelewa jamvi mbunge wangu!
 

mh.mbunge,kipindi cha daladala kipo Tbc1 si cloudsTv. Wahusika ni kijo na bibi kiroboti. Nasema ili uweke kumbukumbu vizuri.
 
@Ng'wenekele weka wazi ni nini kimeongelewa zaidi ili mhe.JJ afanye mambo,kipindi hiki ni kigumu sana kisiasa lkn viongozi safi wapo tayari kujibu propaganda na JJ ni moja ya viongozi safi wa sasa na baadaye huyu bwana na Julius mtatiro ni hazina,wanajua nini wanafanya tofauti na umri wao...PROPAGANDA aitotupeleka popote tuache viongozi wetu wafanye mema wanyanyue nchi yetu ya Tz...vijana ndio wajenga nchi ...viongozi vijana ndio njia tuwape support jama tuache itikadi
 
Kuna mtu alishasema ukiwa kada wa CCM hata ukiwa na degree mbili ni sawa na darasa la saba kumbe ni kweli! Mwenye akili timamu yeyote hawezi kuamini na kuandika tena TETESI kuwa mbunge anafanya kazi ya kugawia watu madampo wamwage taka isipokuwa kwa mwanaCCM waweza kuwa na Masters. Kwa upeo wa chama chako umejitahidi sana, HONGERA JF WAMEKUJUA
Sasa mbona umekuja juu? tulia watu waandike uone jinsi kijana wenu alivyo nae fisadi, niliisha wahi kusema humu ndani hakuna mtu msafi CDM hata mmoja, yataanza kujionyesha kwa mmoja baada ya mwingine, haya ya mnyika hayo sasa
 
Asante Mbunge.
Nilikuwa napata shida kadri ninavyosoma maoni ya baadhi ya member.Tuhuma ni tuhuma na lazima ipate majibu na ni hatua nzuri kwa kutoa majibu.

Ushauri tu!Usiishie hapo kama kweli habari husika imetokana na Chombo cha habari (TBC1)au Clouds FM kwa mujibu wa mtoa habari ni vizuri kufuatilia pale uatakapo pata nafasi ili tabia inayotaka kujengeka ya watangazaji kuwa mashabiki wa Udaku na Udakuzu wa habari za mtaani zisizofanyiwa kazi ipate kurekebika mapema.
Nawasilisha.
 
Yaani Jamii forum wazima mnadiscuss kipindi cha daladala!!!!
 
Kijana ameingia kwa kasi sana kukamata mshiko, nasikia siku alipopewa ile cheki ya Tshs 90m alichanganyikiwa akaanza kutetemeka , kwani hakuamini kabisa kama angeweza kupata hela kama hizo

MARA MIL 90, MARA 280, SASA TUWAELEWE VIPI AU MNA NIA YA KUMCHAFUA JINA MBUNGE, KAMA SIYO KWANINI MSIANDIKE KITU KINACHOELEWEKA
 
Ungeielezea vizuri hiyo ishu ina ukweli? Au ndo kuchafua majina ya watu. Jamani msigeuze jf kuwa sehemu ya udaku.
 
As a General Rule, Hearsay evidence is not admissible............yaani unaleta mambo ya kusikia kwenye jukwaa kama hili? Atetemekena kuchanganyikiwa kwa m90? kwani za kununulia magari walipewa ngapi?......
 
Kwa msiyo na taarifa sahihi kipindi cha daladala kwa sasa kinarushwa na ITV...........(UKITAKA KUJUA UNDANI ZAIDI TUWASILIANE)
 
As a General Rule, Hearsay evidence is not admissible............yaani unaleta mambo ya kusikia kwenye jukwaa kama hili? Atetemekena kuchanganyikiwa kwa m90? kwani za kununulia magari walipewa ngapi?......
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…