Mnyika kalisahau jimbo lake la Kibamba

Mnyika kalisahau jimbo lake la Kibamba

Haya mkuu, naomba tu nimalize ligi hii kwa kusema kwamba hayo niliyoandika ndiyo malalamiko yetu sisi wakazi wa Jimbo la Kibamba (kwa sehemu kubwa). Kama kata ya Kibamba amefanya hayo
itakuwa vizuri, ila ajue na sisi tunamhitaji, yeye pia atazihitaji kura zetu.
Tushirikiane.
Hapo sahihisha kidogo kuwa malalamiko yenu "Wakazi wengi wa kata ya Msumi" wala usijumuishe Kibamba nzima..Mnyika ni mtu wa watu hakika atashirikiana na nyinyi katika kuitengeneza Kibamba iwe mfano wa kuigwa.
 
Afanye kazi yake ya kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Awakilishe mawazo yetu.


Bunge limekaa mara ngapi tangu Kikao hiki cha kumi kianze? unatumia criteria gani kusema mnyika hakuwakilishi?

Unataka awawakilishe vipi? Unajua kuwa Mnyika ni Mbunge mwenye michango mingi zaidi Bungeni...au unamaanisha nini?
 
Hapo sahihisha kidogo kuwa malalamiko yenu "Wakazi wengi wa kata ya Msumi" wala usijumuishe Kibamba nzima..Mnyika ni mtu wa watu hakika atashirikiana na nyinyi katika kuitengeneza Kibamba iwe mfano wa kuigwa.

Muda ni sasa, hii atashirikiana ni future mkuu.

Mtu wa watu kama hatekelezi majukumu yake haina maana.
 
Kule Kibamba hatuina shida naye, hata asipokuja...Ila moyoni tuna amani, hatupo chini ya CCM
 
Muda ni sasa, hii atashirikiana ni future mkuu.

Mtu wa watu kama hatekelezi majukumu yake haina maana.
Si ndo kaanza kata ya kibamba,kwembe,atakuja hadi huko Msumi unakokulilia wewe na kata zilizobaki
 
Bunge limekaa mara ngapi tangu Kikao hiki cha kumi kianze? unatumia criteria gani kusema mnyika hakuwakilishi?

Unataka awawakilishe vipi? Unajua kuwa Mnyika ni Mbunge mwenye michango mingi zaidi Bungeni...au unamaanisha nini?

Hapo kwenye red unamaanisha Bunge la kipindi kipi?

Sina ugomvi na alichokifanya Bunge lililopita, na hiyo ilikuwa ni moja ya sababu za mimi kumchagua bila hata kuzisikiliza kampeni zake.

Kama utakumbuka mwaka 2011 Mnyika alisimama bega kwa bega na wananchi wa Kata za Goba, Kimara na maeneo mengine kupaza sauti za maji, na ilikuwa mwanzoni tu baada ya yeye kuchaguliwa.
 
Mteteeni, mfikishieni ujumbe.

Nia na lengo la huu uzi ni jamaa afikishiwe ujumbe, aijue tathmini yetu juu yake, abadilike na tuwe wamoja.

Asante mkuu kwa taarifa, hizo ndo taarifa tunazitaka na.

Sidhani kama ni kutetea, lakini Kuna Tofauti gani ya sasa na kipindi kilichopita? Tangu achaguliwe umeshapita muda gani?, hata mwaka haujapita watu wameshaanza malalamiko,
Kaka jimbo ni kubwa na lina changamoto nyingi sana, Eneo la jimbo la Kimamba ni eneo ambalo lilikuwa ni mashamba na sehemu kubwa ni milima na mabonde, na Serikali haikuwai kutengeneza miundo mbinu ya aina yoyote katika jimbo hilo, Hakuna Barabara za maana, hakuna network ya maji, umeme watu wamejivutia wenyewe, nyumba zimejengwa kiholelaholela tu,
kwa mfano mbunge akiamua kushughulikia tatizo la maji inaweza kumchukua miaka yake yote mitano na Tatizo halitaisha, Akiamua kufatilia mambo ya Barabara atamaliza miaka yake mitano bila hiyo kero kuisha kila sehemu inahitaji madaraja

Katika majimbo yote ya Dar hili ndio jimbo gumu kuliko yote, ni eneo ambalo halijaendelezwa kabisa,
 
Hapo kwenye red unamaanisha Bunge la kipindi kipi?

Na mimi nimekuuliza kikao hichi cha kumi ...I mean bunge hili tangu lianze limekaa mikutano vingapi? kiasi cha kum judge mnyika kwamba hawakilishi kibamba? Be objective....ili kama unamkosoa mnyika ueleweke unamkosoa kwa lipi
 
Sidhani kama ni kutetea, lakini Kuna Tofauti gani ya sasa na kipindi kilichopita? Tangu achaguliwe umeshapita muda gani?, hata mwaka haujapita watu wameshaanza malalamiko,
Kaka jimbo ni kubwa na lina changamoto nyingi sana, Eneo la jimbo la Kimamba ni eneo ambalo lilikuwa ni mashamba na sehemu kubwa ni milima na mabonde, na Serikali haikuwai kutengeneza miundo mbinu ya aina yoyote katika jimbo hilo, Hakuna Barabara za maana, hakuna network ya maji, umeme watu wamejivutia wenyewe, nyumba zimejengwa kiholelaholela tu,
kwa mfano mbunge akiamua kushughulikia tatizo la maji inaweza kumchukua miaka yake yote mitano na Tatizo halitaisha, Akiamua kufatilia mambo ya Barabara atamaliza miaka yake mitano bila hiyo kero kuisha kila sehemu inahitaji madaraja

Katika majimbo yote ya Dar hili ndio jimbo gumu kuliko yote, ni eneo ambalo halijaendelezwa kabisa,

Kwa sababu hiyo unamaanisha akae tu asifanye chochote kwa sababu itamchukua muda mrefu? Sijaelewa hapa.
 
Kwa sababu hiyo unamaanisha akae tu asifanye chochote kwa sababu itamchukua muda mrefu? Sijaelewa hapa.
Wewe ndio unamuona amekaa, nimeweka hizo changamoto uone kazi aliyonayo, so ukipima matatizo yaliyoko kwenye eneo lako basi ujue jimbo zima lina shida hizohizo kwa hiyo haiwezekani akawa anashinda kwenye eneo lako tu, au amalize shida kwenye eneo lako tu, ukimuona hayuko kwenu, basi yupo eneo lingine akitatua kero kama zenu
 
Na mimi nimekuuliza kikao hichi cha kumi ...I mean bunge hili tangu lianze limekaa mikutano vingapi? kiasi cha kum judge mnyika kwamba hawakilishi kibamba? Be objective....ili kama unamkosoa mnyika ueleweke unamkosoa kwa lipi

Kama umesoma posts zangu kutoka juu, nimezungumzia habari ya Mnyika kutokanyaga jimboni, kutohudhuria mikutano ya Madiwani, kutofanya mikutano kwenye kata za jimbo lake hata ile ya shukrani kwa kuchaguliwa, kama wewe ni mwenyeji kwenye hizi siasa zetu utakubaliana na mimi kwamba mikutano ya majimboni ni kick kubwa sana kwa wabunge na inaendelea kumweka mtu juu.

Unless mnaona anachokifanya ni sawa, mimi kama mimi nakataa na msimamo wangu ni kwamba kama anaendelea namna hii kura yangu no.
 
Kama umesoma posts zangu kutoka juu, nimezungumzia habari ya Mnyika kutokanyaga jimboni, kutohudhuria mikutano ya Madiwani, kutofanya mikutano kwenye kata za jimbo lake hata ile ya shukrani kwa kuchaguliwa, kama wewe ni mwenyeji kwenye hizi siasa zetu utakubaliana na mimi kwamba mikutano ya majimboni ni kick kubwa sana kwa wabunge na inaendelea kumweka mtu juu.
wewe ongelea kata yako...Mnyika kata zingine ametembelea na huko atakuja...Mh Mnyika ni mtu makini na msikivu
 
wewe ongelea kata yako...Mnyika kata zingine ametembelea na huko atakuja...Mh Mnyika ni mtu makini na msikivu
Jamaa anahasira kisa kata yake ya Msumi mnyika hajafika....ila mnyika anasema "Ulipo atakufikia"
 
wewe ongelea kata yako...Mnyika kata zingine ametembelea na huko atakuja...Mh Mnyika ni mtu makini na msikivu

Kata zipi alizoenda?

Kuna mtu humu kasema ameenda kata ya Kibamba tu, na huyu ni mkazi wa Kibamba, wewe unaweza kutaja hizo kata zingine?
 
Mkuu Raimundo ni kweli jimbo la kibamba mnyika hana habari nalo kabisa,diwani Ernest Mgawe ndo amekuwa kama mbunge wetu,wamama walilalamika sana kuhusu soko,kibamba hakuna soko,ni magenge tu,bidhaa zinatoka mikoani zinapelekwa mabibo,halafu zinafuatwa mabibo zinarudishwa magengeni kibamba kwa bei ya juu,madiwani wapo mbunge kawa bubu.najuta kui sihi familia yangu iwapigie kura.japo mama mkandala nae hafai kabisa.mnyika badilika,wapiga kura wako warudishe imani na wewe,unawakatisha tamaa sana.barabara ya kibwegere imekuwa mahandaki,soko hakuna,mbunge kaingia mitini.
 
Mimi ni Mkazi wa jimbo la Kibamba, nilimpigia kura yangu Mh Mnyika bila hata ya kuzisikia sera zake, ni moja ya wabunge vijana niliokuwa nina imani nao sana sana hasa kutokana na michango yake bungeni (Bunge lililopita), harakazi zake za kisiasa akishirikiana na wenzake kipindi hicho kabla Chadema haijamkaribisha Lowassa.

Kiukweli toka Bunge hili jipya lilivyoanza kumekuwa na tetesi mbali mbali juu mwenendo wa Mh Mnyika kisiasa, wengine wakisema hashirikiani na wenzake kwa sababu hajamkubali EL, anataka kujitoa kwenye chama etc etc, huku yeye akiwa kimya.

Sasa basi toka tumemchagua Mnyika, hajawahi hata siku moja kuja jimboni either kutoa shukran kwa kura alizopewa, au hata kuhudhuria vikao vya madiwani, kufanya mikutano ya kisiasa jimboni, kufanya mikutano na wananchi wakamweleza kero zao ili angalau hata akazisemee Bungeni.

Mnyika ni wakati sasa wa kubadilika kama kweli anataka maisha yake ya kisiasa yaendelee, au ampishe mtu mwingine anayetaka kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Mnyika popote ulipo, fanya shughuli za chama lakini kumbuka wananchi waliokuchagua ukawawakilishe, haututendei haki, sitaki kujuta kwa kutompa Dr Fenella Mkangara (CCM), lakini ninaamini kwa mwenendo huu watu tutaanza kujiuliza mara mbili mbili juu ya kama tulipoteza kura au la!
mkuu nami ni mkazi wa kibamba ila nina uelewa tofauti na wewe Mbunge ni mwakilishi wa wananchi,Kwa upeo wangu huduma muhimu ziko barabara zimekwanguliwa vizuri na diwani alishiriki kikamilifu, barabara nyingine ziko katika ujenzi wa kiwango cha lami nadhani hapa ndo Tanroad wanahusika mradi wa maji wamepita kuandikisha watu wanaohitaji maji then umeme ulikuwa unawaka mdogo sasa wameweka mkubwa na umeme siyo shida tena. Kwa haya mengine ni wewe kujiimarisha na kuona nini unachotakiwa kufanya kama raia
 
mkuu nami ni mkazi wa kibamba ila nina uelewa tofauti na wewe Mbunge ni mwakilishi wa wananchi,Kwa upeo wangu huduma muhimu ziko barabara zimekwanguliwa vizuri na diwani alishiriki kikamilifu, barabara nyingine ziko katika ujenzi wa kiwango cha lami nadhani hapa ndo Tanroad wanahusika mradi wa maji wamepita kuandikisha watu wanaohitaji maji then umeme ulikuwa unawaka mdogo sasa wameweka mkubwa na umeme siyo shida tena. Kwa haya mengine ni wewe kujiimarisha na kuona nini unachotakiwa kufanya kama raia

Tunaongelea watu tofauti.

Anyway hope atapata ujumbe.
 
Back
Top Bottom