Mnyika kalisahau jimbo lake la Kibamba

Mnyika kalisahau jimbo lake la Kibamba

Raimundo

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2009
Posts
13,415
Reaction score
12,627
Mimi ni Mkazi wa jimbo la Kibamba, nilimpigia kura yangu Mh Mnyika bila hata ya kuzisikia sera zake, ni moja ya wabunge vijana niliokuwa nina imani nao sana sana hasa kutokana na michango yake bungeni (Bunge lililopita), harakazi zake za kisiasa akishirikiana na wenzake kipindi hicho kabla Chadema haijamkaribisha Lowassa.

Kiukweli toka Bunge hili jipya lilivyoanza kumekuwa na tetesi mbali mbali juu mwenendo wa Mh Mnyika kisiasa, wengine wakisema hashirikiani na wenzake kwa sababu hajamkubali EL, anataka kujitoa kwenye chama etc etc, huku yeye akiwa kimya.

Sasa basi toka tumemchagua Mnyika, hajawahi hata siku moja kuja jimboni either kutoa shukran kwa kura alizopewa, au hata kuhudhuria vikao vya madiwani, kufanya mikutano ya kisiasa jimboni, kufanya mikutano na wananchi wakamweleza kero zao ili angalau hata akazisemee Bungeni.

Mnyika ni wakati sasa wa kubadilika kama kweli anataka maisha yake ya kisiasa yaendelee, au ampishe mtu mwingine anayetaka kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Mnyika popote ulipo, fanya shughuli za chama lakini kumbuka wananchi waliokuchagua ukawawakilishe, haututendei haki, sitaki kujuta kwa kutompa Dr Fenella Mkangara (CCM), lakini ninaamini kwa mwenendo huu watu tutaanza kujiuliza mara mbili mbili juu ya kama tulipoteza kura au la!
 
Next time usichague vitu vya kipuuzi,angalia kina Msigwa, prof J, Sugu wanavyojitahidi kuleta naendeleo jimboni mwao.

Yaani dah, jamaa anatulet down aisee, inakuwaje kijana wa Upinzani unatufanyia hivi?

Yaani anataka tujute kwa kutoichagua CCM?
 
So wewe ni msemaji wa wakazi wa Kibamba mbona mnapenda sana kumuandama Mnyika bila sababu za msingi.

Mkuu mimi ni mpiga kura, Mnyika nimemchagua bila kushurutishwa na mtu, ni imani niliyokuwa nayo kwake, leo hii hakanyagi jimboni hata kidogo?

Wakati wa Kampeni Mnyika alipanga nyumba Mbezi, barabara ya kwenda Malamba Mawili, uchaguzi ulivyoisha tu akaondoka na hakurudi tena, unadhani tunajisikiaje? Kwa nini tu tusinung'unike? Huhitaji kuwa msemaji wa wananchi, mimi nimelalamika kama mimi.
 
Mkuu mimi ni mpiga kura, Mnyika nimemchagua bila kushurutishwa na mtu, ni imani niliyokuwa nayo kwake, leo hii hakanyagi jimboni hata kidogo?
Wakati wa Kampeni Mnyika alipanga nyumba Mbezi, barabara ya kwenda Malamba Mawili,
uchaguzi ulivyoisha tu akaondoka na
hakurudi tena, unadhani tunajisikiaje? Kwa nini tu tusinung'unike? Huhitaji kuwa msemaji wa wananchi, mimi nimelalamika kama mimi.
Kwahiyo hoja yako ni kuwa aje ajenge Kibamba ili uwe unamuona? Unaposema toka mmchague hajawahi kuja Kibamba kuongea na wananchi una uhakika au wewe Kibamba si makazi yako ya kudumu
 
Kwahiyo hoja yako ni kuwa aje ajenge Kibamba ili uwe unamuona? Unaposema toka mmchague hajawahi kuja Kibamba kuongea na wananchi una uhakika au wewe Kibamba si makazi yako ya kudumu

Mkuu unaijua siasa?

Unazijua propaganda za siasa?

Hata kama hufanyi kitu, lakini ile kuwepo kwako, watu wakakufikishia kero zao, ukienda kuzisema bungeni wanaridhika.

BTW, nikuulize, nini kazi ya Mwakilishi wa Wananchi Bungeni?
 
Mimi ni Mkazi wa jimbo la Kibamba, nilimpigia kura yangu Mh Mnyika bila hata ya kuzisikia sera zake, ni moja ya wabunge vijana niliokuwa nina imani nao sana sana hasa kutokana na michango yake bungeni (Bunge lililopita), harakazi zake za kisiasa akishirikiana na wenzake kipindi hicho kabla Chadema haijamkaribisha Lowassa.

Kiukweli toka Bunge hili jipya lilivyoanza kumekuwa na tetesi mbali mbali juu mwenendo wa Mh Mnyika kisiasa, wengine wakisema hashirikiani na wenzake kwa sababu hajamkubali EL, anataka kujitoa kwenye chama etc etc, huku yeye akiwa kimya.

Sasa basi toka tumemchagua Mnyika, hajawahi hata siku moja kuja jimboni either kutoa shukran kwa kura alizopewa, au hata kuhudhuria vikao vya madiwani, kufanya mikutano ya kisiasa jimboni, kufanya mikutano na wananchi wakamweleza kero zao ili angalau hata akazisemee Bungeni.

Mnyika ni wakati sasa wa kubadilika kama kweli anataka maisha yake ya kisiasa yaendelee, au ampishe mtu mwingine anayetaka kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Mnyika popote ulipo, fanya shughuli za chama lakini kumbuka wananchi waliokuchagua ukawawakilishe, haututendei haki, sitaki kujuta kwa kutompa Dr Fenella Mkangara (CCM), lakini ninaamini kwa mwenendo huu watu tutaanza kujiuliza mara mbili mbili juu ya kama tulipoteza kura au la!
Nenda kawe mbunge kwa niaba yake
 
Mimi ni Mkazi wa jimbo la Kibamba, nilimpigia kura yangu Mh Mnyika bila hata ya kuzisikia sera zake, ni moja ya wabunge vijana niliokuwa nina imani nao sana sana hasa kutokana na michango yake bungeni (Bunge lililopita), harakazi zake za kisiasa akishirikiana na wenzake kipindi hicho kabla Chadema haijamkaribisha Lowassa.

Kiukweli toka Bunge hili jipya lilivyoanza kumekuwa na tetesi mbali mbali juu mwenendo wa Mh Mnyika kisiasa, wengine wakisema hashirikiani na wenzake kwa sababu hajamkubali EL, anataka kujitoa kwenye chama etc etc, huku yeye akiwa kimya.

Sasa basi toka tumemchagua Mnyika, hajawahi hata siku moja kuja jimboni either kutoa shukran kwa kura alizopewa, au hata kuhudhuria vikao vya madiwani, kufanya mikutano ya kisiasa jimboni, kufanya mikutano na wananchi wakamweleza kero zao ili angalau hata akazisemee Bungeni.

Mnyika ni wakati sasa wa kubadilika kama kweli anataka maisha yake ya kisiasa yaendelee, au ampishe mtu mwingine anayetaka kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Mnyika popote ulipo, fanya shughuli za chama lakini kumbuka wananchi waliokuchagua ukawawakilishe, haututendei haki, sitaki kujuta kwa kutompa Dr Fenella Mkangara (CCM), lakini ninaamini kwa mwenendo huu watu tutaanza kujiuliza mara mbili mbili juu ya kama tulipoteza kura au la!
hiyo ni kawaida yake mkuu. hata ubungo alifanya hivyohivyo alivoona watu wamemchoka akaakimbilia kibamba. angegombea ubungo wala asingeshinda. sasa 2020 kibamba wakimchoka nahisi atakimbilia kijijini kwa upande wa mama yake au kwa upande wa baba yake hapo miaka mitano mitano,inafika kumi. akimaliza kote atakuwa ameshazeeka na hana uhitaji tena na pesa za ubunge.
 
Mkuu unaijua siasa?

Unazijua propaganda za siasa?

Hata kama hufanyi kitu, lakini ile kuwepo
kwako, watu wakakufikishia kero zao, ukienda kuzisema bungeni wanaridhika.
BTW, nikuulize, nini kazi ya Mwakilishi wa Wananchi Bungeni?
Naijua ndo maana nikakuuliza yawezekana wewe si mkazi wa Kibamba maana nakutilia shaka..hivi madawati aliyotoa Mnyika jimbo la kibamba kupitia diwani wake hukuona na kusaidia wajasiliamali waweze kukopeshwa kupitia benki ya DCB chini ya meya wa kinondoni hujaona au una mpango mkakati wa kumuondoa 2020
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Naijua ndo maana nikakuuliza yawezekana wewe si mkazi wa Kibamba maana nakutilia shaka..hivi madawati aliyotoa Mnyika jimbo la kibamba kupitia diwani wake hukuona na kusaidia wajasiliamali waweze kukopeshwa kupitia benki ya DCB chini ya meya wa kinondoni hujaona au una mpango mkakati wa kumuondoa 2020

Mkuu kuwa specific, sema madawati yametolewa kwa shule zipi, na ni mangapi, ni diwani wa kata gani anayemwakilisha Mnyika?

Kafanya nini kuwasaidia hao wajariamali? Usizungumze juu juu, weka facts tunazoweza kuzithibitisha.
 
Kwahiyo hoja yako ni kuwa aje ajenge Kibamba ili uwe unamuona? Unaposema toka mmchague hajawahi kuja Kibamba kuongea na wananchi una uhakika au wewe Kibamba si makazi yako ya kudumu
Sisi ndo tunaofahamu huenda wewe hukai huku kibamba... mtoa mada hajakosea
 
Mkuu kuwa specific, sema madawati yametolewa kwa shule zipi, na ni mangapi, ni diwani wa kata gani anayemwakilisha Mnyika?
Kafanya nini kuwasaidia hao wajariamali? Usizungumze juu juu, weka facts tunazoweza kuzithibitisha.
Ni ndugu Mgawe Ernest kwani we mwenzetu unakaa Kibamba ipi?isije ikawa upo Mtwara
CcEh9DgWEAAn5UC.jpg
CcEh7KZWAAEjpoX.jpg
 
  • Thanks
Reactions: PNC
Mkuu hayo majibu ni ya kwako, siyo ya Mnyika.

Ninategemea kama watu wanampenda Mnyika wampe ushauri na siyo majibu ya hivyo.
Any way hoja yako ni msingi sana ila nilikuwa sijasoma btn the line. Kimsingi kuwa na viongozi wasiojitambua kwa nini walichaguwa kuwa wawakilishi wa wananchi imekuwa ni tatizo maeneo ya nchi. Kiongozi uliahidi kutatua changamoto nyingi zinazowakabili wananchi wako mwisho wa siku baada tu ya kuchaguliwa unatokomea kusikojulikana. Kiongozi unashindwa kuonesha tofauti za kimaendeleo na mtangulizi wako . Je wananchi wategeme kufanya nn?
 
Ni ndugu Mgawe Ernest kwani we mwenzetu unakaa Kibamba ipi?isije ikawa upo Mtwara

Jimbo la Kibamba lina kata sita, kuwa specific kwamba hiyo ilikuwa kata gani, madawati mangapi.

Nini kimefanyika kwenye kata zingine au hakuna huo uhitaji? BTW, kazi ya mbunge siyo kugawa madawati, ni kuhimiza serikali itimize wajibu wake wa kugawa madawati kwa kila shule.
 
Any way hoja yako ni msingi sana ila nilikuwa sijasoma btn the line. Kimsingi kuwa na viongozi wasiojitambua kwa nini walichaguwa kuwa wawakilishi wa wananchi imekuwa ni tatizo maeneo ya nchi. Kiongozi uliahidi kutatua changamoto nyingi zinazowakabili wananchi wako mwisho wa siku baada tu ya kuchaguliwa unatokomea kusikojulikana. Kiongozi unashindwa kuonesha tofauti za kimaendeleo na mtangulizi wako . Je wananchi wategeme kufanya nn?

Pamoja mkuu, unajua kumekuwa na ufinyu wa kujadili mambo kwa hoja kwa sababu ya hizi tofauti za kivyama, mtu akikosolewa, anakimbilia kusema eti aliyemkosoa chama tofauti na cha kwake, na hivyo anakuwa amekwepa hoja.

Maana ya kuwa muwakilishi wa wananchi ni kwamba matatizo yao ukayawakilishe Bungeni, serikali iyasikilize, hata kama serikali haitafanya lakini iwe imeambiwa.

Sasa kwa mtu kama Mnyika, mimi nilimchagua kwa imani kubwa sana, lakini leo hii jamaa kapotea, hakuna updates zozote za nini anachofanya jimboni wala bungeni, sina uhakika kama kuna anachofanya kwenye chama chake ila hiyo mimi kama mwananchi hainihusu, kinachonihusu ni ananiwakilisha vipi bungeni, anapeleka mawazo yangu? Kayatoa wapi wakati simwoni yeye wala muwakilishi wake jimboni?
 
Mimi ni Mkazi wa jimbo la Kibamba, nilimpigia kura yangu Mh Mnyika bila hata ya kuzisikia sera zake, ni moja ya wabunge vijana niliokuwa nina imani nao sana sana hasa kutokana na michango yake bungeni (Bunge lililopita), harakazi zake za kisiasa akishirikiana na wenzake kipindi hicho kabla Chadema haijamkaribisha Lowassa.

Kiukweli toka Bunge hili jipya lilivyoanza kumekuwa na tetesi mbali mbali juu mwenendo wa Mh Mnyika kisiasa, wengine wakisema hashirikiani na wenzake kwa sababu hajamkubali EL, anataka kujitoa kwenye chama etc etc, huku yeye akiwa kimya.

Sasa basi toka tumemchagua Mnyika, hajawahi hata siku moja kuja jimboni either kutoa shukran kwa kura alizopewa, au hata kuhudhuria vikao vya madiwani, kufanya mikutano ya kisiasa jimboni, kufanya mikutano na wananchi wakamweleza kero zao ili angalau hata akazisemee Bungeni.

Mnyika ni wakati sasa wa kubadilika kama kweli anataka maisha yake ya kisiasa yaendelee, au ampishe mtu mwingine anayetaka kuwawakilisha wananchi Bungeni.

Mnyika popote ulipo, fanya shughuli za chama lakini kumbuka wananchi waliokuchagua ukawawakilishe, haututendei haki, sitaki kujuta kwa kutompa Dr Fenella Mkangara (CCM), lakini ninaamini kwa mwenendo huu watu tutaanza kujiuliza mara mbili mbili juu ya kama tulipoteza kura au la!
Kweli Mkuu hata huku Goba kapasahau asipokuwa making 2020 atakimbia jimbo kama alivyokimbia ubungo
 
Back
Top Bottom