rmashauri
JF-Expert Member
- Jan 29, 2009
- 3,011
- 462
Bunge letu kwa sasa limekuwa la hovyo sana. Na hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na upendeleo wa wazi unaofanywa na hao wanaokalia kiti cha spika cha kuwakandamiza wapinzani kiasi kwamba kimewafanya wapinzani kuwa na hasira wawapo bungeni. Nilimwona Lisu alivyokasirika pale aliponyimwa nafasi alipoomba mwongozo wa mwenyekiti/spika wakati Sugu alipotakiwa kuwataja Janjaweed. Nafikiri kuna umuhimu wa katiba mpya kutaka Spika kuwa mtu asiyekuwa na chama ili kutoa usawa kwa wabunge wa vyama vyote.