Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Vijana watatu wakiwa porini kwa ajili ya kutafuta kuni,kwa bahati mbaya mmoja wao alijikata kwa panga mguuni na kuumia vibaya sana.Wakaamua kumbeba kwa zamu kurudi naye nyumbani kwa sababu alikuwa hawezi kutembea mwenyewe.Mara ghafla wakiwa njiani,simba akatokeza.Wale jamaa wakambwaga mwenzao chini,wakatoka mbio kuokoa maisha yao.Walipofika nyumbani walishangaa kumkuta yule jamaa aliyeumia mguu kwa kujikata kwa panga akiwasubiri.Jamaa akawaambia;'mliponibwaga chini na mimi nilitoka mbio kwa kutumia njia tofauti na yenu.