Mnatoa milio kuhusu makala za BBC?

Mnatoa milio kuhusu makala za BBC?

TheForgotten Genious

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2014
Posts
2,742
Reaction score
4,146
Hiki kikundi cha wahuni kinachojiita Serikali kumetoa tamko kuhusu mfululizo wa makala kupitia kipindi cha AFRICA EYE DOCUMENTARIES,wanalalamika kwamba BBC haizingatii weledi.

Ukiangalia na kufuatilia kwa umakini utagundua namna gani sehemu nyeti zinaongozwa na matakataka ambao wanajina maarufu chawa,ukifikia hatua yakuandaliwa documentary kupitia "AFRICA EYE" Ujue umeshatoboka kila kona,kipindi hiki mpaka kirushe makala huwa uchunguzi wa kina umefanyika na kuthibitishwa pasipo shaka,hata hivyo mashuala yaliyozungumziwa katika makala hii sio yakufanya uchunguzi deep kiasi hicho yapo wazi kila kona,waliohojiwa wamenogesha tu makala.

Kikunde cha wahuni badala yakuchukua hatua za kidiplomasia wanapiga kelele kuhusu BBC,wakifikiri BBC ni TBC,walifanya hivyo kwa CNN iliporusha mauaji ya oktoba 29.,wanarudia yaleyale na ni mtu yuleyule.

Mmesha chafuka,naweza kusema mmejiharishia na hakuna maji yakutosha kujisafisha katika safari ndefu na hamna njia mbadala ya kupunguza ama kumaliza harufu hiyo,kaeni mkao mzuri,CNN wanakuja na part two ya mauaji ya oktoba 29 na baada ya hapo wakionesha makaburi ya alaiki na miili mliyotuma mto Ruvu,Rufiji na zile sehemu mlizofukia na kwenda kuchoma.

Bichwa maji lenu limesikika likisema matamko ya Umoja wa madola yanaiweka kikundi chake katika wakati mgumu.
 
Kinachonishangaza ni kwa kiasi gani wanadamu waafrika hatuna utu hata chembe chembe.

Watu wanashangili unyama utafikiri hawana watoto ambao ipo siku watoto wao wakipata janga kama hili itakuwaj
 
Kinachonishangaza ni kwa kiasi gani wanadamu waafrika hatuna utu hata chembe chembe.

Watu wanashangili unyama utafikiri hawana watoto ambao ipo siku watoto wao wakipata janga kama hili itakuwaj
ASILI.,UTAFIKA WAKATI NAO WATAKUTWA NA HAYA NA TUTASHANGILIA
 
Naona hata kama wangepewa utetezi, mbona Iko vibaya upande wao!
 
Hiki kikundi cha wahuni kinachojiita Serikali kumetoa tamko kuhusu mfululizo wa makala kupitia kipindi cha AFRICA EYE DOCUMENTARIES,wanalalamika kwamba BBC haizingatii weledi.
Tatizo ni kuwa Wahuni wamezoea ukweli kama ule wa TBC - kupindisha ukweli, propaganda, uongo, uzushi na hadaa..

Sasa wakikutana na vyombo vyenye weledi ambavyo havipokei rushwa zao wala hawawezi kutishia na kuteka waandishi wao, wanabaki kulia lia tu
 
Tatizo ni kuwa Wahuni wamezoea ukweli kama ule wa TBC - kupindisha ukweli, propaganda, uongo, uzushi na hadaa..

Sasa wakikutana na vyombo vyenye weledi ambavyo havipokei rushwa zao wala hawawezi kutishia na kuteka waandishi wao, wanabaki kulia lia tu
Na bado,wataongea kiyunani.
 
Back
Top Bottom