Mnataka kumbebesha Hayati Magufuli madhambi yenu?

Unaijua story ya Ulimboka
Mbona hakukuwa na mafanikio?
Some hitmen are incompetent...so to say

..wakati mwingine mtu anasalimika kwa bahati yake tu.

..Fidel Castro ali'survive 7 assasination attempts za CIA.

..kuna watu wamesalimika kwenye ajali za ndege, wakati inaaminika ndege ikianguka hakuna anayesalimika.

..na ukiangalia tukio la Lissu utaona kwamba his chances of surviving zilikuwa ndogo sana sana, lakini baada ya operations 20+ amesalimika.
 
Kama akili yako iko sawa usingeandika huo utumbo. Kwa taarifa yako huyu Samia akiwa VP hakuwa na nguvu yoyote kwenye utawala wa Magufuli. Kwanza mara 3 hivi alikwisha tamani kujiuzulu akazuiwa na Mzee wa Msoga.
Kumbe unajua..mtu aliyeamua kujiuzulu huwa kuna mtu anaweza mzuia akakubali km hakuna linalowaunganisha?
 
Ukitathmini rafu za uchaguzi mkuu bila kuhusisha ujinga na upumbavu unaotokea kwenye mchakato wa kura za maoni za CCM jumuisho utakalotoa litakuwa ni bandia si halisi..na hivyo kusema Magufuli pekee ndiye aliharibu uchaguzi 2020 si kweli!
Akiwa Mwenyekiti wa ccm alileta mabadiliko muhimu ndani ya ccm ikiwemo mabadiliko ya kura za maoni..lengo ni ccm kupata wagombea hodari, wenye sifa stahiki wasiohitaji uwepo wa hila na ghiliba kushinda..na hatimae waunde serikali imara..kilichotokea sote tunajua, mabadiliko mapya ya kura za maoni yalitupwa dk za mwisho na kurejeshwa ule upumbavu wa siku zote! Kwa wasiojua leo niwasaidie vitu viwili vinavyoisumbua ccm na nchi kwa ujumla..
1. ccm inaendeshwa na kusimamiwa na mercenaries kwa kushirikiana na baadhi ya viongoz wastaafu kulinda agenda zao..bahati mbaya watanzania wengi hawafahamu jambo hili hata Magufuli alikuwa mmojawapo..
2. ccm inaendesha mambo yake yote kwa cartel system..wengi hawajui na Magufuli hakujua pia..
Kama ndani ya ccm uchaguzi kuwapata wagombea ni uhuni mtupu, unaweza tarajia jema kwenye uchaguzi mkuu? Utakuwa mwendawazimu punguani wa mwisho kuamini uchaguzi mkuu utakuwa fair!
Makosa ya Magufuli..
1. Kushindwa kufanya homework yake baada ya kuapishwa ya kudeal na wastaafu na genge lao 100% amalizane nao mapema! yaliyomtokea mwishoni bora yangetokea mwaka wake wa kwanza wa urais!
2. Kutofahamu kutumia mamlaka aliyokuwa nayo vizuri na kutegemea ushauri potofu wa kuvikwa sifa bandia akalewa na kusahau hatari zilizokuwa pembeni yake, hatimaye zikagharimu maisha yake na nchi nzima kurudi nyuma zaidi kuliko hata pale tulikuwa kabla hajawa Rais!
Tusimlaumu Magufuli kwa ubovu wa uchaguzi 2020, ana sehem ndogo sana ya yaliyotokea wakati huo!
Dawa ni katiba mpya itakayompa Rais UFAHAMU wa kumaliza homework zake mapema bila kuambiwa na yeyote!
 
Hivi mnataka tuamini kuwa Uchaguzi Tanzania miaka yote ulikuwa unafanyika vizuri, kwa Amani, na bila makadokado ya Chama tawala na wapambe wake? Kwamba kufika 2020 mambo yakaharibika? Yaani, tuamini JPM na timu yake walivuruga uchaguzi ili washinde 2020? Kabla ya hapo mambo yalikuwa powa. Uchaguzi wa 2015 na ule wa 2010 hakukuwa na matatizo?

Mmesahau kabisa yaliyotokea 2010?
Arumeru Mashariki
Nyamagana
Igunga
Nzega
Mbeya Mjini
Arusha Mjini
Tarime
Ubungo
Kilombero
Bumbuli

Na kuwa matokeo ya uchaguzi wa Rais yalivyodaiwa kupikwa na kundi la vijana waliofadhiliwa data center kumanipulate data za Tume?

Au mmesahau jinsi vyombo vya Habari vilivyokatazwa kutangaza matokeo ya Urais kama yalivyo majimboni...

Najibiwa...
Mwanakijiji wewe ni sukuma gang...uchaguzi wa 2015 ndio JPM aliuharibu wa 2010 was the best election ever!!

Nawajibu
Hakuna mwaka Tanzania ilishuhudia damu kumwagika kwenye uchaguzi ili kuhakikisha utawala unabakia madarakani kama 2010. That's a fact not an opinion.

Nawauliza:

Nani alimwaga damu kuelekea uchaguzi wa 2020 au siku ya uchaguzi?

NB*: Nimesahihisha hapo juu miaka.
Katiba mpya muhimu!
 
Hakuna mwema hapa!

Hakuna was afadhali iwe kikwete,mama Wala jpm wote wanafanana tofayti ni style!!

Jpm hakuwa mnafiki.wa.kuzunguuka sana !alitumia Dola kubaki madarakani kama wenzake bila soni!!!

Hakutaka kujifanya eti anajali demokrasia alionyesha uhalisia was ccm was kuiba uchaguzi bila aibu ,sio kama kina jk na samiah wanafiki wanaita maridhiano halafu wanaudikteta chini chini!!

MWAROBAINI NI KATIBA MPYA TU BASI NA SIO HAYA MAIGIZO!!
Wewe ndo umesemq point,,Dr silaa alishainda Urais lakini akatangawazwa kikwete harafu watu wanasema etinmagufuri ailikiwa mbaya ila Hawa wengine walikuwa wazuri
 
Nimezungumzia mtazamo wangu mkuu.
Japo kiuhalisia CCM imeoza kuanzi shina mpaka matawi.
Hata jae malaika akiingia CCM atakua shetani tu.
Ila kwa marais wote bora Magufuli aisee kwanza alijitahidi kiutendaji pili alikua transparent sio kama hawa wengine UNAFIKI MWINGI MAPAMBIO KIBAO KUJIPAKA MAFUTA KWA MGONGO WA CHUPA.
Alikuwa transparent wakati wa utawala wake alizuia open government, na kuondoa uhuru wa vyombo vya habari? Hivi mkiongea haya mnadhani haya mambo yalifanyika zamani sana kiasi kwamba tutakuwa tumesahau? Au kwa kuwa alifanikiwa kupumbaza kundi kundi kubwa kwa vitisho na propaganda, basi mndhani wote tulikubali hadaa zile?
 
Mwaka 2020 hakukuwa na uchaguzi bali kulikuwa na uchafuzi. Ni aibu kwa level yako kama mwana JF mkongwe kuvaa miwani ya mbao kwenye huo uwendawazimu wa 2020
Upinzan mngeshida kwa kwa lipa la maana hapa hai tu kila mtu anajua mbowe alikuwa amechokwa hata kama wangewekeewa cdm na jiwe bado wstu wangechagua jiwe

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Umeulizwa swali; nani alimwaga damu ya nani kwenye Uchaguzi wa 2020?
Najinukuu '' Ni kweli lakini kuna udokozi na Ujambazi. Mwaka 2020 ulikuwa ujambazi''
Hili linajibu hoja ya Mzee Mwanakijiji ya kumbebesha madhambi. Hapana! anabeba madhambi yake

Dhambi yake ni Ujambazi. Nia ya Jambazi ni uovu na dhambi.
Ukifanikiwa kuruka dirisha haina maana jambazi ni zuri kwasababu hakuna aliyekufa nyumbani kwako.
The fact that Jambazi lipo kwako dhamira yake ni mbaya.

Hakuna Jambazi zuri kwasababu limevaa suti, jambazi ni jambazi tu na uovu ndio mizigo yake
Kilichofanyika 2020 ni Ujambazi tena mchana ! Tutapaka rangi, manemane na utuli mwisho Jambazi ni Jambazi tu.
 
Kama akili yako iko sawa usingeandika huo utumbo. Kwa taarifa yako huyu Samia akiwa VP hakuwa na nguvu yoyote kwenye utawala wa Magufuli. Kwanza mara 3 hivi alikwisha tamani kujiuzulu akazuiwa na Mzee wa Msoga.
Sasa wewe mwenye akili timamu ndo umeandika cha maana,kwani huyo Mama kipindi maamuzi yanafanywa hakuwa sehemu ya mfumo huo? Huwezi muweka Samia pembeni juu ya uongozi wa JPM,utakuwa haupo Sawa kichwani.

Kama ulivyo dai alitaka kuachia nafasi kwa kuona ni kama kivuli,na kuzuiwa na Mzee wa Msoga basi ni dhahiri kwamba ana akili ya kushikiwa na ndio maana madai ya kwamba remote iko Msoga ni ya kweli.
 
Hakuna mtumishi yeyote yule wa umma au taasisi yoyote ile inayoweza kumpangia Rais cha kufanya chini ya katiba hii.
Siyo kumpangia Rais cha kufanya, wanatakiwa kumshauri na pia kutekeleza maagizo yake kwa weledi.
Mara nyingine watumishi hao hufanya vitendo vyenye madhara kwa kujipendekeza tu.
 
Najinukuu '' Ni kweli lakini kuna udokozi na Ujambazi. Mwaka 2020 ulikuwa ujambazi''
Hili linajibu hoja ya Mzee Mwanakijiji ya kumbebesha madhambi. Hapana! anabeba madhambi yake

Dhambi yake ni Ujambazi. Nia ya Jambazi ni uovu na dhambi.
Ukifanikiwa kuruka dirisha haina maana jambazi ni zuri kwasababu hakuna aliyekufa nyumbani kwako.
The fact that Jambazi lipo kwako dhamira yake ni mbaya.

Hakuna Jambazi zuri kwasababu limevaa suti, jambazi ni jambazi tu na uovu nidio mizigo yake
Kilichofanyika 2020 ni Ujambazi tena mchana ! Tutapaka rangi, manemane na utuli mwisho Jambazi ni Jambazi tu.
Pole..
 
Tanzania bwana, mtu anaweza kushiriki kuwaibia wananchi kura zao lakini bado wananchi wakadanganywa kuwa mtu huyo ni mzalendo na mhadilifu...sijui wanadhani uwizi unaanzia wapi na kuishia wapi.
 
Ukitathmini rafu za uchaguzi mkuu bila kuhusisha ujinga na upumbavu unaotokea kwenye mchakato wa kura za maoni za CCM jumuisho utakalotoa litakuwa ni bandia si halisi..na hivyo kusema Magufuli pekee ndiye aliharibu uchaguzi 2020 si kweli!
Akiwa Mwenyekiti wa ccm alileta mabadiliko muhimu ndani ya ccm ikiwemo mabadiliko ya kura za zake mapema bila kuambiwa na yeyote!
Jipige kifua mara tatu sema mimi ni PIMBI. Alileta mabadiliko ya kipumbavu tu. Yaani kutumia fedha za umma kununua wabunge wa upinzani ndiyo mabadiliko ndani ya CCM??
 
Sasa wewe mwenye akili timamu ndo umeandika cha maana,kwani huyo Mama kipindi maamuzi yanafanywa hakuwa sehemu ya mfumo huo? Huwezi muweka Samia pembeni juu ya uongozi wa JPM,utakuwa haupo Sawa kichwani.

Kama ulivyo dai alitaka kuachia nafasi kwa kuona ni kama kivuli,na kuzuiwa na Mzee wa Msoga basi ni dhahiri kwamba ana akili ya kushikiwa na ndio maana madai ya kwamba remote iko Msoga ni ya kweli.
Nafuu uwe remote utawale nchi kwa amani kuliko kuitwa Jiwe halafu hushauriki, unaua wapinzani, unanyang'anya fedha za watu benki na unawatupa gerezani.

Lile DUBWASHA ndiyo maana lilikufa maana lilikuwa linaharibu nchi yetu
 
Hivi mnataka tuamini kuwa Uchaguzi Tanzania miaka yote ulikuwa unafanyika vizuri, kwa Amani, na bila makadokado ya Chama tawala na wapambe wake? Kwamba kufika 2020 mambo yakaharibika? Yaani, tuamini JPM na timu yake walivuruga uchaguzi ili washinde 2020? Kabla ya hapo mambo yalikuwa powa. Uchaguzi wa 2015 na ule wa 2010 hakukuwa na matatizo?

Mmesahau kabisa yaliyotokea 2010?
Arumeru Mashariki
Nyamagana
Igunga
Nzega
Mbeya Mjini
Arusha Mjini
Tarime
Ubungo
Kilombero
Bumbuli

Na kuwa matokeo ya uchaguzi wa Rais yalivyodaiwa kupikwa na kundi la vijana waliofadhiliwa data center kumanipulate data za Tume?

Au mmesahau jinsi vyombo vya Habari vilivyokatazwa kutangaza matokeo ya Urais kama yalivyo majimboni...

Najibiwa...
Mwanakijiji wewe ni sukuma gang...uchaguzi wa 2015 ndio JPM aliuharibu wa 2010 was the best election ever!!

Nawajibu
Hakuna mwaka Tanzania ilishuhudia damu kumwagika kwenye uchaguzi ili kuhakikisha utawala unabakia madarakani kama 2010. That's a fact not an opinion.

Nawauliza:

Nani alimwaga damu kuelekea uchaguzi wa 2020 au siku ya uchaguzi?

NB*: Nimesahihisha hapo juu miaka.
Usifananishe kabisa na miaka ya nyuma.
Magufuli alifanya ujambazi na uharamia kabisa ile 2020
 
Upinzan mngeshida kwa kwa lipa la maana hapa hai tu kila mtu anajua mbowe alikuwa amechokwa hata kama wangewekeewa cdm na jiwe bado wstu wangechagua jiwe
Unachanganya vitu viwili, kushinda uchaguzi na kutenda haki.

Hakuna anyedai Wapinzani wangeshinda au kushindwa. Kinachozungumziwa ni haki kutokuwepo, uchaguzi ulivurugwa chini ya uangalizi wa Marehemu Jambazi

Mkuu wa Polis Hai alimwambia mgombea '' Wewe hutashinda hata ukifanya nini wakati anazuia mkutano wa huyo aliyetabiriwa kushindwa'' Huyu ni Mkuu wa Polisi wa Wilaya akifanya kazi za CCM kwa kulipwa kodi zetu.

Tume ya Uchaguzi ilikaa kimya kwa kumuogopa Jambazi, na Jambazi lilikaa kimya kwasababu lilishatamka '' ole wako umtangaze mpinzani kashinda''. Huu ndio Ujambazi tunaoongelea na Jambazi lilifanya hivyo kwa uwazi na mchana.

Jambazi halisafishiki hata kwanini, mtapaka rangi lakini matendo yake yanatoa uvundo.
 
Back
Top Bottom