Kuangalia JF kunawiana vipi na kuwa na post 15,000? Ili ufikishe post hizo lazima uandike na kupost kwenye thread mbalimbali.
Pia ili ufikishe posts 15,000, lazima uanze na kupost post moja. So worry not, iko siku nawe unaweza fikisha idadi hiyo ya post. Kama umejiunga JF jana au mwaka jana usijilinganishe na mtu aliyejiunga hapa mwaka 2006.
Zaidi ya hayo, kama wewe ni bank teller, na baada ya kazi unaenda kupata kilaji, usijilinganishe na mtu ambae kazi yake ni kuandika na kufanya uchunguzi, muda wake mwingi anautumia kutafuta habari na kuzianalyse, kutunga habari na kuzichapisha na mambo kama hayo.
Usiige tembo kunya, utapasuka....