Mnaangalizia wapi JF jamani?

Mnaangalizia wapi JF jamani?

Kaniki1974

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2008
Posts
352
Reaction score
22
Kazini, nyumbani, internet cafes, simu za mkononi au wapi? Ni kutaka kujua maana watu hadi posts 15,000? Inakuwaje? Wengine 24/7? Mnabalance vipi na mambo yenu mengine? Hakuna walioathirika vibaya na hii kitu? Hebu tuambiane ukweli basi..I dare to talk openly?
 
Yo-Yo: ''Wanaume wanaotumia muda mwingi JF hawana mashori wazuri''
Itabidi tuitishe FJ Bash tuone kama Yo-Yo yuko sahihi.
 
Kazini, nyumbani, internet cafes, simu za mkononi au wapi? Ni kutaka kujua maana watu hadi posts 15,000? Inakuwaje? Wengine 24/7? Mnabalance vipi na mambo yenu mengine? Hakuna walioathirika vibaya na hii kitu? Hebu tuambiane ukweli basi..I dare to talk openly?

Aisee kweli bwana, JF is as addictive as heroin! Bila dozi ya 'angalau' saa moja ya JF unaweza kosa usingizi ati!
 
sio siri mimi na jf nikama samaki na maji. kwanza ndo home page yangu.kwa kifupi mimi naangalizia kwenye ka laptonga kwangu huku mbele (oslo) ambako napiga shule.
huwa napata taarifa kibao.
Nyani ngabu wewe vp?
 
Kazini, nyumbani, internet cafes, simu za mkononi au wapi? Ni kutaka kujua maana watu hadi posts 15,000? Inakuwaje? Wengine 24/7? Mnabalance vipi na mambo yenu mengine? Hakuna walioathirika vibaya na hii kitu? Hebu tuambiane ukweli basi..I dare to talk openly?

Kuangalia JF kunawiana vipi na kuwa na post 15,000? Ili ufikishe post hizo lazima uandike na kupost kwenye thread mbalimbali.

Pia ili ufikishe posts 15,000, lazima uanze na kupost post moja. So worry not, iko siku nawe unaweza fikisha idadi hiyo ya post. Kama umejiunga JF jana au mwaka jana usijilinganishe na mtu aliyejiunga hapa mwaka 2006.

Zaidi ya hayo, kama wewe ni bank teller, na baada ya kazi unaenda kupata kilaji, usijilinganishe na mtu ambae kazi yake ni kuandika na kufanya uchunguzi, muda wake mwingi anautumia kutafuta habari na kuzianalyse, kutunga habari na kuzichapisha na mambo kama hayo.

Usiige tembo kunya, utapasuka....
 
I wonder what is your motives. At the end of the day where do you want to take us to? Worry not about statistics, mind their contributions and learnings from great JF people. One posting can mean a lot than 15,000 posts. Mind the contents rather.
 

...............
Usiige tembo kunya, utapasuka....


teh teh teh kwi kwii kwii!
kuna tofauti kubwa ya lini mtu kajiunga na idadi ya post zake, mtu wa 2006 na 2009 ni tofauti, kuna mtu mmoja wa 2006 (jina kapuni) hajafikisha hata post 500!, yupo wa March 2009 anapost zaidi ya 1000!, ukiangalia hapo utakuta wengine wanapost hata pumba tu, ili mradi aonekane ana posts nyingi, bora upost hata 2 zenye akili kuliko 100 zenye matope!

kuna wazee wa kukopi na kupaste, hawa hawafikirii kwa akili zao, bali ni kunakili what others did, wanaonekana vichwaaaaaaaaaaaa kumbe hawana lolote
 
Tumtendee haki muuliza swali. Mwenzetu anataka kujua watu wanaangalizia JF wapi? kazini, nyumbani, shuleni na wana balance vipi majukumu yao ya kila siku na JF addiction.

Kazini, nyumbani, internet cafes, simu za mkononi au wapi? Ni kutaka kujua maana watu hadi posts 15,000? Inakuwaje? Wengine 24/7? Mnabalance vipi na mambo yenu mengine? Hakuna walioathirika vibaya na hii kitu? Hebu tuambiane ukweli basi..I dare to talk openly?

Ndugu yangu... wewe angalia unataka kushiriki JF kwa lengo gani.Je ni kujifunza na kubadilishana uzoefu na wenzako? Ni njia ipi bora itakufanya ufikie azma yako?Ukiwa kazini kwa vyovyote unatakiwa ufanye kazi kwanza kabla ya kukimbilia JF vinginevyo kazi yako itaathirika kwa hasara yako mwisho wa siku.Kama wewe ni mwanafunzi, ukishinda JF ujue shule itakushinda. Kwa maneno mengine tenga ,muda wako... unaweza kutumia muda wako wa lunch au mapumziko kutembelea JF.

Kuna swala la gharama. Ukisema uende internet cafe kila siku na kila wakati, je ushiriki wako JF unalipa kiasi cha kuweza kubeba gharama za internet? Ushauri wangu ni kutumia nafasi uliyo nayo kufanya vitu kadhaa kwa wakati mmoja. Ukiwa uko kwenye internet unafanya mambo mengine yenye kukuletea pesa unaweza ukaunganisha na ushiriki wako JF. Labda uwe na budget maalum ya kujifurahisha na badala ya kwenda kwenye unywaji basi tumia budget hiyo kufanya kitu chenye manufaa zaidi kama kushiriki JF.

Aisee kweli bwana, JF is as addictive as heroin! Bila dozi ya 'angalau' saa moja ya JF unaweza kosa usingizi ati!
Kilevi chochote kinaweza kuwa na madhara. Hivyo ndugu muuliza swali ukae ukijua kuwa JF ni nzuri lakini pia inaweza kukuathiri kama laivyosema ndugu yetu SMU.

ili ufikishe posts 15,000, lazima uanze na kupost post moja. So worry not, iko siku nawe unaweza fikisha idadi hiyo ya post. , kutunga habari na kuzichapisha na mambo kama hayo.

Usiige tembo kunya, utapasuka....
uw hapa anakupa ushauri mzuri sana....usiangalie wengine wamefanya nini au wamefikisha posts ngapi.

teh teh teh kwi kwii kwii!
kuna tofauti kubwa ya lini mtu kajiunga na idadi ya post zake, mtu wa 2006 na 2009 ni tofauti, kuna mtu mmoja wa 2006 (jina kapuni) hajafikisha hata post 500!, yupo wa March 2009 anapost zaidi ya 1000!, ukiangalia hapo utakuta wengine wanapost hata pumba tu, ili mradi aonekane ana posts nyingi, bora upost hata 2 zenye akili kuliko 100 zenye matope!
kuna wazee wa kukopi na kupaste, hawa hawafikirii kwa akili zao, bali ni kunakili what others did, wanaonekana vichwaaaaaaaaaaaa kumbe hawana lolote
Kila mtu JF ana mchango wake na kwa aina tofauti. Kuna wenye kuuliza maswali kila kukicha wakitaka ushauri, kuna wenye kuleta mizaha na utani na hii pia ni muhimu kusaidia watu ku relax, kuna wenye kuleta mada moto zenye kuhitaji michango na analysis, kuna wenye kutafuta na kubandika habari kutoka vyanzo mbalimbali. Hawa tena mimi naweza kuthubutu kusema kuwa ni muhimu mno maana kuna watu hawawezi kupata habari hizo kwa urahisi. Hivyo ni makosa kubeza watu kwa michango wanayoitoa JF.

Ndugu yangu, usihofu kuchangia kwa style yoyote kwa maana kila mchango ni muhimu hapa JF.
 
sio siri mimi na jf nikama samaki na maji. kwanza ndo home page yangu.kwa kifupi mimi naangalizia kwenye ka laptonga kwangu huku mbele (oslo) ambako napiga shule.
huwa napata taarifa kibao.
Nyani ngabu wewe vp?

Nilitaka kumuuliza pia huyu mkuu....
 
Kuangalia JF kunawiana vipi na kuwa na post 15,000? Ili ufikishe post hizo lazima uandike na kupost kwenye thread mbalimbali.

Pia ili ufikishe posts 15,000, lazima uanze na kupost post moja. So worry not, iko siku nawe unaweza fikisha idadi hiyo ya post. Kama umejiunga JF jana au mwaka jana usijilinganishe na mtu aliyejiunga hapa mwaka 2006.

Zaidi ya hayo, kama wewe ni bank teller, na baada ya kazi unaenda kupata kilaji, usijilinganishe na mtu ambae kazi yake ni kuandika na kufanya uchunguzi, muda wake mwingi anautumia kutafuta habari na kuzianalyse, kutunga habari na kuzichapisha na mambo kama hayo.

Usiige tembo kunya, utapasuka....

Kwikwikwiiiiii anayemuiga tembo kufanya hivyo, mjinga sana....hope haumuigi tembo pia teh teh teh. You got it bad!
 
... ukiangalia hapo utakuta wengine wanapost hata pumba tu, ili mradi aonekane ana posts nyingi, bora upost hata 2 zenye akili kuliko 100 zenye matope!
Kweli Mkuu, wengine ni matusi tu, wanapewa ban lakini wakirudi tu post yao ya kwanza ni matusi, sasa sijui wingi wa post una maana tena hapo!
 
Ila kuna mtu alishauliza siku za nyuma swali almost similar na alilouliza Kaniki kwamba watu wanafanya kazi zao sangapi maana wanatumia muda mwingi JF? akajibiwa kuwa kuna watu ambao kukaa kwenye mtandao (kama JF) ndo kazi yenyewe. Kama ni kweli basi obviously wao watakuwa na muda mwingi na post nyingi zaidi ya wale wanao visit JF kwa kutoa/kutafuta habari, kupumzisha akili, nk
 
Ila kuna mtu alishauliza siku za nyuma swali almost similar na alilouliza Kaniki kwamba watu wanafanya kazi zao sangapi maana wanatumia muda mwingi JF? akajibiwa kuwa kuna watu ambao kukaa kwenye mtandao (kama JF) ndo kazi yenyewe. Kama ni kweli basi obviously wao watakuwa na muda mwingi na post nyingi zaidi ya wale wanao visit JF kwa kutoa/kutafuta habari, kupumzisha akili, nk
Duh,

Kwa mara ya kwanza nasikia hii... Hahahaha, yani mtu kazi yake ni kukaa JF kujibu posts?

Hata Admin au moderators JF si kazi yao rasmi (as far as I know). Kama wapo wa hivi kweli kazi ipo....
 
Duh,

Kwa mara ya kwanza nasikia hii... Hahahaha, yani mtu kazi yake ni kukaa JF kujibu posts?

Hata Admin au moderators JF si kazi yao rasmi (as far as I know). Kama wapo wa hivi kweli kazi ipo....

Ha!ha!ha! Mkuu Max.....nadhani hapa wadau watakuwa wanarefer washkaji wa UWT na kuna wale wengine ambao wanaweza kuwa sponsored just ''kuspoil mazingira'' hapa!
 
Hehehe
Maxence umeniacha hoi.
Hujui kwamba kuna viumbe humu kazi yao kutwa kuchwa ni kujua nani kapost nini na wamjibu vipi na kisha wanacompile report then haoooo wanaipeleka kunakohusika?

Mie huwa naangalia JF kila mtandao unapoconnect. I mean huwa nina mambo yangu muhimu nayafanza kisha kila nukta nikaapo net huwa nalog in ili kupata kitu kipya kwa ajili ya ufahamu na akili yangu. Yaani nikiamka manane na nikakosa usingizi huwa naingia mtandaoni na kuzungumza na wakeshaji wenzangu.

Ila kiukwelii kuna walumendago humu ni wababe hata wakanywe vipi ila kwa kuwa ndo jamii yenyewe, bila wao hakuna sisi.

niko adiktive kiukwelii
 
kuna watu humu ni kama vile hawana kazi ingine zaidi ya jf hata kama ni kutafuta habari na ku anaanalyse i think it's abit too much
 
Ni mtazamo,

Kwa kusoma replies nyingi hume ndani sijaona hata mmoja ambaye anasema yeye ni online 10 hours p.d, hii inamaanisha wengi huingia kwenye net kwa kubahatisha, pia inaashiria swala la internet penetration katika bongo bado ni ndoto.

Internet ni nzuri ila kama vitu vingine ukitumia sana unakuwa adictive, kwa wale waliojiunga na JF kwa ridhaa zao bila kushurutishwa wanaweza kuaccess pahala popote home, work place, phone just like breathing.

Kuna mtu anaitwa joyceline mhh....
 
sio siri mimi na jf nikama samaki na maji. kwanza ndo home page yangu.kwa kifupi mimi naangalizia kwenye ka laptonga kwangu huku mbele (oslo) ambako napiga shule.
huwa napata taarifa kibao.
Nyani ngabu wewe vp?

Mimi matawi ya juu. Niko wired 24/7...

Wengine tuko hapa muda mwingi na wengine wako facebook 24/7 wakianika mambo yao binafsi....
 
Back
Top Bottom