Nuru Ndosi
Member
- Mar 31, 2013
- 13
- 2
Poleni Mungu awafariji
Mama wa rafiki yangu wa kufa na kuzikana amefariki wapendwa. Ni my childhood best friend ambae siwezi kuelezea urafiki wetu kwa maandishi. Yani huyu mkaka ambae mama ake amefariki tulipendana sana kama ndugu wa damu, hatukuwahi hata kuwa wapenzi japo wengi walihisi sisi ni wapenzi. Naugulia tu hapa, niko mbali kwenda kuzika sitaweza nimebaki na majonzi hata kazi hazifanyiki tena. Uwiii hapa sina hata wa kunibembeleza mwenzenu, huku niliko sina hata ndugu.
Nimeona hata niandike hapa nipunguze msongo huenda nitapata ahueni.
Yes ni my brother. Kwa kweli inaumiza moyo sana hasa pale unapofikiria kuhusu mahangaiko ya maisha na suala la familia. Joseph ameenda. Mkewe na watoto wako hospital.. Tunatarajia kumpumzisha katika nyumba yake ya milele baadaye leo mchana.{Jumatano tarehe 10/04}.
Jamani asanteni
woote angalau najiona wepesi kidogo, huyu ni kama mama yangu mzazi,
imeniuma sana siwezi elezea kushindwa kuwepo na kumfariji rafiki yangu
mpendwa na kipindi hiki kigumu cha msiba wa mama.
Pole sana. Nami nipo katika wakati mgumu sana kwa wiki hii. Nimeondokewa na wapendwa wawili kuanzia jumapil had leo.
Wa kwanza ni kaka yangu Anaitwa Joseph Rweyemamu {Mtoto wa mama mkubwa}. Amefariki kwa ajali ya gari Kahama.. Mwingine ni rafiki yangu Kipenzi. Anaitwa Elizabeth {Wakyo} Mkongwe.. Kwa kweli imekuwa week ya huzuni sana kwangu.. Vifo vya vijana hao waliokuwa wanaanza kupata maendeleo ktk maisha yao vimefanya niyafikirie maisha katika namna ya tofauti na isiyoelezeka..
R.I.P Luteni Joseph Rweyemamu.
R.I.P Elizabeth 'Wakyo'Mkongwe.
I will always love and miss u wapendwa wangu..