Kongosho
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 35,987
- 24,232
Adabu za kizamani kwa baadhi ya maeneo ilikuwa ni pamoja na watoto kutokula vyakula fulani fulani
Vyakula hivyo ilikuwa ni kwa ajili ya baba mwenye nyumba au watu wazima
Kule nitokako ilikuwa paja na kuku au kichwa cha samaki ilikuwa kwa ajili ya baba mwenye nyumba
Kuna wengine paja na firigi ilikuwa ni kwa ajili ya baba mwenye nyumba pia
Nakumbuka kuna hg aliwhi fukuzwa kwa jirani kisa alionja firigisi bila kujua umuhimu wa firigisi kwa familia hiyo, aliyaaga mashindano pale pale.
Binafsi nina kijana mmoja asipokula paja hali kitu kingine, na wala halalamiki, ni kuwa anapenda paja japo ni mdogo. Na mie huwa sioni kwa nini asile apendacho. Ni kama mie nipendavyo miguu ya kuku na kwato zake, naskia kweli nimekula.
Sasa huwa napata wasi wasi, je kijana huyu siku akienda kwa watu si ataonekana hana adabu?
Labda anaweza jisahau akala paja afu ukakuta kumbe kala roho ya baba mwenye nyumba??
Hizi zile adabu za mtoto hali hiki kama wakubwa wapo au mwanamke hali hiki kama wanamme wapo, bado zinalipa kweli? Na zinaweza kukuondoa katika kundi la wastaarabu?
Hebu nisaidieni kabla sijaharibu watoto nyumbani kwa kuwapa uhuru wa kula watakavyo.
Vyakula hivyo ilikuwa ni kwa ajili ya baba mwenye nyumba au watu wazima
Kule nitokako ilikuwa paja na kuku au kichwa cha samaki ilikuwa kwa ajili ya baba mwenye nyumba
Kuna wengine paja na firigi ilikuwa ni kwa ajili ya baba mwenye nyumba pia
Nakumbuka kuna hg aliwhi fukuzwa kwa jirani kisa alionja firigisi bila kujua umuhimu wa firigisi kwa familia hiyo, aliyaaga mashindano pale pale.
Binafsi nina kijana mmoja asipokula paja hali kitu kingine, na wala halalamiki, ni kuwa anapenda paja japo ni mdogo. Na mie huwa sioni kwa nini asile apendacho. Ni kama mie nipendavyo miguu ya kuku na kwato zake, naskia kweli nimekula.
Sasa huwa napata wasi wasi, je kijana huyu siku akienda kwa watu si ataonekana hana adabu?
Labda anaweza jisahau akala paja afu ukakuta kumbe kala roho ya baba mwenye nyumba??
Hizi zile adabu za mtoto hali hiki kama wakubwa wapo au mwanamke hali hiki kama wanamme wapo, bado zinalipa kweli? Na zinaweza kukuondoa katika kundi la wastaarabu?
Hebu nisaidieni kabla sijaharibu watoto nyumbani kwa kuwapa uhuru wa kula watakavyo.