Mmm, eti Paja na Firigisi Vya Baba. . .

Mmm, eti Paja na Firigisi Vya Baba. . .

pole, asante kwa kushare story hii

umeona kuwa kuna vyakula vya fulani na fulani katika sahani moja hiyo hiyo.

Haya mambo yapo bana.

kongosho, hakuna ch paja la mkubwa wala la baba...

vijana hususan wanaokuwa wanahitaji minofu kwa ukuaji wao....

umenikumbusha kipindi tukiwa wadogo...... mama alipata nafasi ya kwenda nje kuongeza elimu na kutupeleka mwanza kwa mjomba..... kwanza kule

1. watoto wote wakati wa kula tunakaa mkekani, kasoro mjomba, mkewe na watoto wao 3 wao ndo wanakaa mezani......

2. mwendo wa kula kwenye sinia finyango moja moja mapochopocho yote meza kuu, na ni marufuku kugusa... na unajua sheria ya kula kwenye sinia? spidi yako ndo kushiba kwako

3. tukila kuku ujue mwendo wa ngwala na vipapatio

4. mbaya zaidi tukapata tetekuwanga uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii tuliiba simu kumpigia mama tunaumwa karibia tutakufa....

the gud thing ni kuwa mama alipokuja kutuona tuliogeshwa, tukapakwa dawa, tukaka mezani na kupakuliwa minofuuuuuu si kujichana masamaki, kujichana mapaja ya kuku tetetete ingawa tuliambiwa firigisi ya baba, maini ya watoto mweeeh siku chache haooooooooo kwenye treni dar...ikabidi mdingi atulee mwaka mzima kwikwikwikwi

Kongosho umenikumbusha mbaaali sana yaani natabasamu mwenyewe hapa, wadau wananishangaa... sorry kwa kutoka nje ya mada
 
Last edited by a moderator:
ha ha ha ha, tena unaombea kuku awe na kichwa kikubwa kama ng'ombe.

Yaani nimecheka jamani.
Eti siku una zali ni shingo?
ndo maana siku hizi ninawamindi sana hawa viumbe ,hawakatizi mbele yangu wala siwezagi kufuga kuku siku mbili tu namchinja..yaani akikatiza katiza mbele yangu huwa nachanganyikiwa kabisa lazima nimle!
 
mie ni wa kienyeji mno kula hao vyuku.

Nataka nikila kuku, kwanza naanza kwa kumkimbizaaa hadi majirani wanione.
Baada ya hapo namchinja mwenyewe na kumnyonyoa ndio naanza kumpika.

Sio mpnzi wa bloila kabisa.

Lakini swali, je hizo adabu zina mantiki?
Naweza fika baa nikapiga kilauri na mtu asinijali?

kwa kiasi fulani zina mantiki ndugu, lakini sio wakati wote...mi nadhani dhana ya baba kula zile parts nono nono ni kwa kuwa ndiye mhangaikaji na aliyeleta chakula mezani...ni dhana iliyorithiwa kutoka tabaka za kale
 
Nani kakwambia yameisha? Mimi mwenyewe nina about 30yrs ila wife akipika cha kwanza kabisa kuniwekea ni firigisi na anajua nisipoikuta patachimbuka bila jembe...kuhusu vidali na makalio ya kuku hayo hayanisumbui kabisa. anakula watoto pamoja na mtoto mkubwa yaani my wife!

WE UTAKUWA MUME WA snowhite nini upo na ID nyingine manake lol!issue ya paja,firigisi kwa kweli ni kosa tena kosa la kuweza kabisa kununiwa na kwanza hzo guts za kulifanya hilo kosa mp-aka ununiwe unazitoa wapi!
 
Last edited by a moderator:
Haya mambo yalikuwa zamani ambapo kuku analiwa mara moja kwa mwaka, siku hizi hata kila siku home mkitaka mnakula kuku, coz gharama yake kama si chini ya kilo moja ya nyama ya ng'ombe baasi zimelingana,kama akija kwangu atakula mapaja yote coz home kwangu hakuna anayependa mapaja kama zile stake za kuku na vibawa vile
 
WE UTAKUWA MUME WA snowhite nini upo na ID nyingine manake lol!issue ya paja,firigisi kwa kweli ni kosa tena kosa la kuweza kabisa kununiwa na kwanza hzo guts za kulifanya hilo kosa mp-aka ununiwe unazitoa wapi!
Kumbe na wewe uko humu? nimeona niwe muwazi vile tunavyoishi ili kuwaweka sawa watu humu jamvini...si unajua mwenyewe bila firigisi panachimbikaga? nimekuja na ID ingine...ile nyingine niliitumia vibaya akina Paw na Buchanan wakaipiga pin!
 
Last edited by a moderator:
ha ha ha, na mie ni kidari na miguu tu.

Sasa huwa najistukia labda namzoea vibaya asije akanitia aibu ugenini.

Labda aende kijijini lakini mjini na self service sidhani.
 
Msilete mizaha!Kuku akichinjwa nyumbani watoto na mama yao wanaweza kula wooote isipokuwa FIRIGISI tu!Hiyo ndo alama kwamba baba yupo nyumbani!
 
Mimi binamu yangu mmoja aliachwa baada kumpakulia boyfriend wake kipapatio weeee alijuta...kikwetu kimatako na kichwa cha samaki cha baba mwenye nyumba....sasa mimi na mume wangu inabidi tunawekeana zamu ya kula vichwa vya sato na hicho kimatako cha kuku
 
Back
Top Bottom