Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Maisha ya mwanadamu ni mafupi sana ,yapita kama umande jua lituapo,Mola na awe mfariji kwa ndugu ,jamaa, marafiki na wapenzi wote wa 5 star modern taarab
 
Inatisha na kutukumbusha kwamba kifo kiko nasi wakati wote. RIP marehemu wote na Mwenyezi Mungu awape faraja wafiwa,
 
RIP marehemu wote na Mungu awape speedy recovery majeruhi!. Sijui mpaka lini ndio hawa wakubwa zetu watakuwa serious na sheria za barabarani tutakufa kila siku kwa sababu ya uzembe tu malori mabovu huwa yanapakiwa hovyo bila hata signs (reflectors) za kujulisha madereva arghhh! sick!
 
R.I.P marehemu wote, na MUNGU awajalie uponyaji wa haraka majeruhi wote
 
Siku imeshaanza vibaya kwangu.
Tayari nimeshagubikwa na huzuni.
 
Raha ya milele uwape ee Bwana, uwapumzishe kwa amani yako. Wafariji wote wanaoteseka na kusononeka na msiba huu, wape moyo wa uvumilivu.

R.I.P.
 
RIP wasanii wetu. Poleni sana wafiwa.
Hii habari nilipoisikia tu nikakumbuka thread ya Mkuu Majimoto - Biashara ya Uchawi. Ilitaja matukio kama haya yanavyopikwa/tengenezwa katika ulimwengu usioonekana. Imeniuma sana.
Tunaangamia, Mungu tunusuru.
 
Yaan nimeumia sana kwa vifo hivi hasa kifo cha Issa kijoti .da,nimeguswa sana,siamini ila inabidi nikubali ukwl kuwa mmoja wa wanamziki nimzimiaye hayupo duniani na bendi niipendayo ni km imekufa
 
R.I.P
ajali za bongo zikianza ni mfululizo,hatukawii kusikia nyingine muda si mrefu,mungu tusaidie na kutulinda maisha yetu yapo hatarini sana.
 
Jana wanamziki wa 5 star modem taarabu wamepata ajali maeneo ya Moro na kusababisha umauti kwa wanamziki wapatao 13...mimi sio mpenzi wa taarabu kabisa na naichukia mno...lakini kama binadamu na mtanzania nazililia roho za ndugu na rafiki zetu tuliowapenda sana....nalo jiuliza


  1. Nani alaumiwe kwa hizi ajali za mara kwa mara zinazo maliza roho za ndugu zetu?
  2. Je hakuna njia kuwadhibiti madereva wazembe na wahuni wanaoendesha magari bila kuzingatia sheria za barabarani?
Bila kupata majibu ya maswali haya tutakufa kama kuku kila siku barabarani........

Mungu atuepushie balaa hili....
 
Back
Top Bottom