Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Mlolongo wa Ajali za Barabarani Tanzania 2007-2011

Jamani, haya mafuso yaondolewe hiyo Morogoro road..uhai wa watu ni muhimu sana, tungeweka statistics za watu waliopoteza maisha kwenye hii barabara
 
Waliokuwemo kwenye VX wanahusiana na waarabu wenye Chalinze Auto Spares wa pale Lumumba poleni sana wahanga wa hiyo ajali.
 
Poleni sana wafiwa.
Mungu awape nguvu na uponaji majeruhi wote.
 
Naogopa kwakweli. We need to thank God kila siku tukifika nyumbani salama! life is too short!! natoa pole kwa wafia..na majeruhi wapone upesi.
 
Pole kwa wafiwa, Tujitahjidi kufanya ukaguzi wa magari kila mara, Halafu hizi barabara zetu ni za ajabu sana, inakuwaje wanachimba mamitaro makubwa hivyo halafu yako wazi?kama si kutafutia watu mauti ni nini? kwa nini wasiweke mitaro ya kisasa ambayo inamifuniko ?
 
Mkuu kuwa na huruma angalau. Mnb unahukumu au we hutaonja mauti?
Inatisha, pole kwa wanaohusika
Watu wengine yani kabisa wanaombea wenzao wafe. Hii dunia bwana. Sio fresh...:A S thumbs_down:
 
Jamani siyo jambo la kusema pole tuu huku roho za watu zikiangamia kila kukicha na ajali za barabarani. Hapo Kimara Korogwe ajali nyingi za hivi karibuni zinasababishwa na matuta yaliyowekwa kwenye highway!!!Kusa issue ya uzembe wa madreva lakini pia upande wa serikali itazame kama imetekeleza wajibu wake ipasavyo,Kinyume chake kila siku tutaishia kutoa pole tuu RIP! Ajali zingine tunaweza kuziepuka pasina shaka kabisa. Rushwa ni ajali kubwa zaidi, Kwani kama hilo gari limekaguliwa tangu lilikotoka hayo ya kufail break yangetoka wapi??Jaribuni kuangalia muundo wetu wa usafiri wa nchi kavu na jinsi nzuri ya kuwatumia wataalamu katika sekta hiyo kubuni njia salama ya kuepusha ajali kuliko kuwategemea hawa askari wetu wenye njaa!!
 
poleni wafiwa hilo eneo lakuanzia resort sheli hapo mpaka korogwe ilo eneo ni hatari kwa ajali nimekulia hapo kwa wale wenyeji wa resort wanajua
 
Ajali zingine sijui tuziite zina mkono wa nani. Make hata shetani anaweza kuzikataa kuwa zina mkono wake. Poleni majeruhi na Mungu awarehemu wote waliotangulia mbele ya haki.
 
Nimepita hapo sijaona dalili za kasheshe hilo. Niliangalia sana kwani nilisoma habari hii nikiwa ofisini. Nilianza kuangalia tokea Bucha hadi Kimara Mwisho sikuona kama kuna mahali kulikuwa na ksheshe hilo
 
........Inahuzunisha kwa kweli, RIP marehemu wote.
 
Madereva wa maFUSO chanzo kikubwa cha ajali kwa kuwa si professionals! Nidhamu ya kukaa barabarani hawana, utashangaa wana overtake kwenye mpindo ulio sharp au mteremko mkali kama mto Ruvu. Udereva ni zaidi ya kukalia kiti na kushika usukani jamani!
 
Back
Top Bottom