Mliopita JKT tunaomba mtupe ushuhuda

Mliopita JKT tunaomba mtupe ushuhuda

Mimi nafikiri huko wanafundshwa ukakamavu tu ila uzalendo hapana ni uongo kabisa.

Hebu fikiria haya majizi na mafisadi mbona sio wazalendo na wamepita huko miaka hiyo?

Uzalendo ufundishwe Kuanzia shule ya msingi, hauwezi mfundisha uzalendo mtu mzima tena kwa miezi michache tu.
 
Asubuhi chai maziwa mkate na yai au karanga, mchana ugali mkubwa na nyama, jioni wali maharage na chai ya rangi, sasa hapo unyanyasaji unatoka wapi.
Kikubwa ni kunywa maji mengi mpaka roho ielee, maana hiyo menu utailipia ni mwendo wa tizi tizi na kazi kazi haina kukata mauno.
Week tatu nne za mwanzo zinakuwaga ngumu unaweza torokea porini, ila baada ya hapo ukisha zoea asee ni patamu sana mpaka inafika siku ya kuondoka unatamani kulia, na lazima utapamisi sana
Kwa mimi, kazi nzuri sana hapa duniani kuzidi zote ni jeshi. Jeshi ni kama 'mitochondria' ya seli hai ya kiumbe hai. Jeshi linaweza kuendesha mambo yake kivyake bula kutegemea msaada mwingine, yani ni kama nchi flani hivi [emoji1][emoji1][emoji1] Kuna kila aina ya kitu kilichopo duniani na vingine vipo jeshini ila uraiani hakuna. Jeshi ni raha !

Kwa mtoto wa kike sio vyema kwenda jeshini kwa namna mazoezi yalivyo, na jinsi atakavyoombwa na kutoa mahaba kwa askari wanaume.
 
Mimi nafikiri huko wanafundshwa ukakamavu tu ila uzalendo hapana ni uongo kabisa.

Hebu fikiria haya majizi na mafisadi mbona sio wazalendo na wamepita huko miaka hiyo?

Uzalendo ufundishwe Kuanzia shule ya msingi, hauwezi mfundisha uzalendo mtu mzima tena kwa miezi michache tu.

Tatizo watu hawaelewi maana ya askari. Askari politics sio sababu ya kazi yako, kazi yako ni moja tu utii,ukakamavu na uzalendo. Ukianza kujali kuhusu politics hiyo kazi huto fanya
 
Jkt ni kichaka cha wakuu wa JW kupiga pesa we umeona kozi gan ya kijesh inachukua mienzi mitatu???
 
Mujibu wa sheria raha sana, ni mazoezi ya kawaida ila kama ww ni stubborn kidogo watakuzingua sema watoto wa kike wanautumikia vilivyo kwa ofa ya kupangiwa kazi nyepesi


Tuliopita 832kj Ruvu mlandizi, tujuane
 
Mtoto wangu wa kiume kwenda JKT ni lazima hili halina mjadala kwangu.

Mitoto ya sasa imelegea sana, lazima Jeshi litunyoshee hawa vijana otherwise ni msiba kwa Taifa.
Wa kwangu nimechemsha aisee! Amejifichia kwenye historia ya maumivu ya mgongo. Kuna kipindi alipoingia form 5 alipata shida ya mgongo sasa umekuwa wimbo kwamba bado hujapona eti akisimama muda mrefu maumivu yanarudi. Sasa nimemwambia jeshi atakutana nayo hapa hapa home. Kazi ya kwanza nimempeleka shamba kuvuna alizeti niligoma kuweka watu wa mshahara mpaka aimalize! Tunavuna na kupiga hapo hapo! Dogo namwona anajinyoshanyosha tu! Na mimi namwambia si umekimbia JKT lazima uione hapa hapa home!
 
Mujibu wa sheria raha sana, ni mazoezi ya kawaida ila kama ww ni stubborn kidogo watakuzingua sema watoto wa kike wanautumikia vilivyo kwa ofa ya kupangiwa kazi nyepesi


Tuliopita 832kj Ruvu mlandizi, tujuane
Tena hii hii Ruvu JKT ndipo dogo alikuwa amepangiwa hapo! Hebu lete ABC za hapo mkuu. Ila kijana ana shida ya mgongo sasa na mimi imebidi nimhurumie tu! Nilitamani sana aende lakini kwa hiyo shida naogopa!
 
Hawa JKT Kwa Mujibu Wa Sheria Waache Uzembe Waende Wakapate Taaluma Mbalimbali
 
Jkt hakuna mateso unafundishwa uzalendo hauandaliwi kuwa Mwanajeshi ndio maana hawafundishwi hata kuhusu mapigano wala mbinu za kivita na hata silaha wanazofundishwa JKT ni personal Weapons Kama SMG, SAR labda na hand grenade na Rocket Launcher hawafundishwi silaha zote za kivita hutaona 12mm, 14mm wala 75RR hizi zinafundishwa kwa upande wa JWTZ wanakoandaliwa kuwa wanajeshi.
 
Tena hii hii Ruvu JKT ndipo dogo alikuwa amepangiwa hapo! Hebu lete ABC za hapo mkuu. Ila kijana ana shida ya mgongo sasa na mimi imebidi nimhurumie tu! Nilitamani sana aende lakini kwa hiyo shida naogopa!
Ruvu JKT ni pazuri Kwa watu wenye baadhi ya mapungufu wao wanakua hawafanyi kazi zozote pia wanaangaliwa kwa ukaribu

Mazingira ni rafiki sana kwa wale wa mujibu.... nlikuwa pale mujibu 2020 majukumu tuliyokutana nayo;

📍Kilimo cha mpunga walikua wanaita shadidi na mahindi pale pembeni ya mto ruvu 🤔🤔 shughul yake haikua ya kitoto tulifeka tukachoma taka na tukalima, tukapanda na tulikua tunamwagilia kila siku


Kilimo Cha nyanya, hoho na vitu hapa nyuma ya Ruvu club, tuliandaaa majaruba tukapanda na kila siku tulikua tunamwagilia ukitoka hapo no erection

Kilimo cha mboga mboga mf. Chainizi na nyanya jirani na geti la kuingilia kambini kwa tuliotoka shamba haikua shida!

Ujenzi wa uwanja uliokuwa unatumiwa na club ya Ruvu shooting aisee hiyo shughul ya kubeba tofali 😁😁


Ujenzi wa baadhi ya maeneo pale Ruvu Jkt club unakua saidia fundi 😁

Usafi kwenye mabanda ya kuku, bwawa la samaki, kwa nguruwe na baadhi ya maeneo ya bustani

Kimsingi mujibu haina shida shughul ni wale wa kujitolea
 
Mkuu mimi nahitaji kufahamu tu yalipo huko kwasababu sikufanikiwa kupita huko, umri wangu kwasas sio wa kwenda huko
Nima zoezi yaliyojengwa kukupa nidhamu ya maisha na utii na uzalendo.

Ila pia kunauzalishaji Mali wa makambi kama kulima. Ila ukweli tulipita huko, hatujutii... Yametujenga kiakili hasa katika kujituma, ubunifu na kiongozi. Niseme ukweli wakati niko Nanashiriki nilikua nalaumu, ila nilipokuja mtaani na kazini nimejiona utofauti Sana na wasioenda.
 
Ruvu JKT ni pazuri Kwa watu wenye baadhi ya mapungufu wao wanakua hawafanyi kazi zozote pia wanaangaliwa kwa ukaribu

Mazingira ni rafiki sana kwa wale wa mujibu.... nlikuwa pale mujibu 2020 majukumu tuliyokutana nayo;

[emoji625]Kilimo cha mpunga walikua wanaita shadidi na mahindi pale pembeni ya mto ruvu [emoji848][emoji848] shughul yake haikua ya kitoto tulifeka tukachoma taka na tukalima, tukapanda na tulikua tunamwagilia kila siku


Kilimo Cha nyanya, hoho na vitu hapa nyuma ya Ruvu club, tuliandaaa majaruba tukapanda na kila siku tulikua tunamwagilia ukitoka hapo no erection

Kilimo cha mboga mboga mf. Chainizi na nyanya jirani na geti la kuingilia kambini kwa tuliotoka shamba haikua shida!

Ujenzi wa uwanja uliokuwa unatumiwa na club ya Ruvu shooting aisee hiyo shughul ya kubeba tofali [emoji16][emoji16]


Ujenzi wa baadhi ya maeneo pale Ruvu Jkt club unakua saidia fundi [emoji16]

Usafi kwenye mabanda ya kuku, bwawa la samaki, kwa nguruwe na baadhi ya maeneo ya bustani

Kimsingi mujibu haina shida shughul ni wale wa kujitolea

Ruvu ni kambi ambayo haina mushkeli, nenda kwa oljoro na kambi zingine. Ni kaz na mazoez juu
 
Ni adhabu au ilikuwaje mzee wa nyuzi zinazoishi?
Hapana Ilikuwa ni kipindi cha 6 weeks ilee mwishoni semaa Mgambo JkT ikapigaa bonge la mvuaaa kwabza tulikuwa tunakesha Mpakaa asubuhi jambo ambalo sio sahihi sema ndo vile ubabe tuu.. Ika kupiga mvuaa kubwa tumekaa nje maafande wamasimama hakuna kukimbia oyaa tuliala kwenye matope unasikia maji yanapita chini ndani ya nguo ila usingizi ulivyokaba unalala unaota kabisaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] Jeshi konyoo aisee nilidata.
 
Back
Top Bottom